Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira Kuanzia Januari, 2021 hadi Februari, 2022 pamoja na Taarifa ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji kwa Kipindi cha Januari 2021 hadi Januari 2022

Hon. Juma Usonge Hamad

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chaani

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Taarifa ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira Kuanzia Januari, 2021 hadi Februari, 2022 pamoja na Taarifa ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji kwa Kipindi cha Januari 2021 hadi Januari 2022

MHE. JUMA USONGE HAMAD: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante na mimi kunipatia fursa hii ya kusimama kwenye Bunge lako yukufu. Lakini pia na mimi niungane na wenzangu kukupongeza kwa kushinda kwa kura nyingi sana. (Makofi)

Baada ya kusema hayo naomba nijikite zaidi kwenye ripoti ambayo iliyowasilishwa na Mwenyekiti wa Kamati ya Viwanda, Biashara na Mazingira, lakini zaidi nitajikita kwenye maeneo ya mazingira.

Mheshimiwa Naibu Spika, Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ni mjumbe katika mifuko ya kimataifa yanayohusu masuala ya mazingira duniani.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba uniruhusu nitaje baadhi ya wadau ambao wanachangia sana kwa ajili ya nchi yetu ya Tanzania ikiwemo list of Development Countries Fund, kuna mfuko wa Adaptation Fund, kuna Global Environment Facility ambayo ni ikolojia hiyo kuna mfuko ambao unaitwa Green Climate Fund, kuna mfuko ambao unaitwa UN Environmental Program.

Mheshimiwa Naibu Spika, mifuko hii inapofadhili nchi zetu hizi Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa maana kwamba Zanzibar pamoja na Jamhuri ya Tanzania ambayo ni Tanzania tatizo linakuja kwenye ugawaji wa fedha. Zanzibar miaka yote fedha hizi hazifiki ipasavyo, kwa mfano na nikupe mfano mzuri kuna mradi ambao unatekelezwa wa Global Environment Facility wa ikolojia ambayo kwa ajili ya kunusuru hizi kaya maskini pamoja na vijiji ambavyo viko hatarini kwa ajili ya kuharibika na mazingira.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuna fedha ambazo zimetoka zaidi ya bilioni 17 lakini cha kushangaza Zanzibar tumepata 18% na miradi hiyo mpaka hii leo haijakamilika na mradi huu ukomo wake ni ifikapo mwezi Julai, 2022.

Mheshimiwa Naibu Spika, cha kushangaza miradi mingine ambayo tayari inafanyika huku Tanzania Bara miradi hiyo inafanyika kwenye Wilaya nne na yote tayari ishakamilika na fedha zote zimeenda lakini changamoto zile za Zanzibar mpaka leo hii miradi haijakamilika na zimetoka shilingi 402,792,000 basi hizo ndiyo ziliotoka utashangaa nini tatizo; ukiwauliza Zanzibar wanasema fedha zimeganda huko.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo lazima tuwe wa wazi kabisa Mheshimiwa Waziri nakuomba sana na Serikali yako hii miradi ya fedha zinapokuja Zanzibar tuzisimamie kwa pamoja. Leo hii kuna blah blah nyingi, leo hii tumechonganisha wananchi kati ya Serikali na wananchi wenyewe, leo hii wananchi tumewaambia fedha hizi tunaenda kununua maboti, tunaenda kuwasaidia wajasiriamali, lakini kuna miradi ambayo tayari tumeikita pale kwa ajili ya kupanda miti ya kuhimili mabadiliko ya tabianchi. Lakini leo hii miradi hii imefanyika asilimia moja asilimia 90 bado haijakamilika ukomo wa mradi huu uanenda kukamilika kesho kutwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, kama Taifa tunaenda wapi? Tukae tujitafakari hii mifuko wenzetu wanatusaidia kwa Imani. Leo hii miradi hii haikamiliki kwa muda upasavyo, tunaweka picha gani huko mbele? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, miradi hii inatekelezwa kwenye Wilaya ya Kaskazini A - Unguja kwenye vijiji zaidi ya vine, wananchi wa kule sasa hivi wameweka kasumba kubwa dhidi ya Serikali yao, Serikali ya Zanzibar ukiwauliza Zanzibar...

MHE. SOUD MOHAMED JUMAH: Mheshimiwa Naibu Spika, Taarifa.

NAIBU SPIKA: Taarifa.

T A A R I F A

MHE. SOUD MOHAMED JUMAH: Mheshimiwa Naibu Spika, ningependa kumpa taarifa mzungumzaji Mheshimiwa Juma Usonge uratibu kama alivyozungumza wa fedha ambazo zinakwenda Zanzibar ambao Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ndiyo masuuli kwa kweli haliko vizuri; kuna mradi ambao ulikuwa wa African Development Bank na ulikuwa na pesa kidogo tu just dola 350,000 lakini kutokana na uratibu mbaya mradi ule muda umemalizika na zimetumika fedha kama 30% tu na zilizobakia fedha zimeenda halijojo yaani fedha hazikutumika tena mradi umefungwa. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo tungeliomba tu uratibu huu tukaupitia na ingewezekana ukaunda tume maalum ya kuweza kuratibu hizi fedha ambazo zinakwenda Zanzibar na mifuko yote hii matumizi yakoje na changamoto ziko wapi? Ahsante. (Makofi)

NAIBU SPIKA: Ahsante endelea Mheshimiwa; taarifa umeipokea?

MHE. JUMA USONGE HAMAD: Mheshimiwa Naibu Spika, taarifa nimeipokea kwa mikono miwili. (Makofi)

Kwa hiyo, kama alivyozungumza mtoaji taarifa Mheshimiwa Waziri nakuomba sana kwenye fedha hizi ambazo zinaenda Zanzibar tuzisimamie ipasavyo lakini siyo hilo tu pia kuna Mifuko hii ya Jimbo ambayo mnayotupa kila siku tukiwaulizia wenzetu wa Tanzania Bara fedha tayari zimeshaingia, kwa Zanzibar kule kuna urasimu ambao tayari hauna majawabu. Hii ni tatizo tunaumia sana. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, ukiangalia Zanzibar kama tunafanya tathmini Zanzibar ndiyo inahitajika zaidi kupeleka zile fedha. Kuna visiwa sasa hivi vinaanza kupotea, kuna miradi mbalimbali haifanyi kazi sababu ya fedha haiziingizwi, juzi Mheshimiwa Waziri ulikuja Zanzibar umefika mpaka eneo Nungwi umeona maeneo ya beach kule yanavyoharibika na maji kupanda juu. Lakini siyo hilo tu almost Zanzibar nzima kisiwa kinapotea, fedha tunazipata lakini mwisho wa siku urasimu ndiyo ambao tayari unaofanya kazi. Kwa hiyo hatuwi wa wazi, wala hatuwi active kwa ajili ya kuisimamia hii miradi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya kusema hayo machache naunga mkono ripoti ya Kamati. (Makofi)