Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo ya Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023

Hon. Omar Ali Omar

Sex

Male

Party

ACT

Constituent

Wete

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo ya Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023

MHE. OMAR ALI OMAR: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa fursa hii ya kuchangia katika Mpango huu. Kwanza nampongeza sana Mheshimiwa Waziri kwa kutuletea Mpango huu. Kwa kweli utasaidia kujenga Taifa letu lenye uchumi utakaoendelea na kudumu katika nchi yetu na wananchi kupata manufaa zaidi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka nichangie katika maeneo mawili makubwa; eneo la kwanza nataka nichangie kwenye uvuvi wa bahari kuu na eneo la pili nitajikita kwenye kilimo cha mwani. Kwani katika Mpango huu Mheshimiwa Waziri amezungumza kwa kiwango kikubwa kuhusu habari ya uvuvi wa bahari kuu na ameonesha kwamba, mpango ule wa kupatiwa meli nane zile za uvuvi bado, Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imeuangalia kwa kina sana. Hata hivyo, bado nahisi kwamba, kutokana na mazingira ya uvuvi wa bahari kuu, basi kuna haja katika Mpango huu uelekeze zaidi kwenye hizi meli za uvuvi, basi zisiwe nane badala yake zile meli ziongezeke zaidi na zaidi zielekezwe katika maeneo ambayo yana uvuvi wa bahari.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukiangalia uvuvi ni sekta moja ambayo inatuwezesha kuishi maisha ya rah ana starehe katika maisha yetu ya kila siku. Hakuna mtu hata mmoja anayeishi bila ya kutegemea minofu ya samaki.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama unataka kujua kwamba uvuvi au samaki wana faida kubwa katika maisha ya mwanadamu, twende pale canteen tu ukawaangalie Waheshimiwa wanavyohangaika kushughulika na minofu ya samaki. Hii ni kuonesha kwamba uvuvi wa bahari kuu unaweza kutusaidia kutupatika pato la Taifa, lakini kujenga maisha yetu ya kila siku. Hata tunaweza tukampunguzia Waziri wa Afya wagonjwa wengi ambao anawatibu kwa kila siku kutokana na hali ya afya zao kutokuboreka, lakini zinaboreka kwa sababu ya minofu ya samaki. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukiangalia samaki hawa hawa ndiyo wanaowawezesha wananchi wetu wakaishi wakiwa na afya bora za kuweza kufanyakazi kwenye kilimo, kwenye viwanda na shughuli mbalimbalii tunazozitegemea za maisha yetu ya kila siku. Hii ni kuonyesha kwamba sekta ya uvuvi ni sekta ambayo inahitaji kupewa kipaumbele kama vile tunavyoipa kipaumbele sekta ya kilimo kwa sababu hizi ni sekta pacha kama unataka kuleta maendeleo katika nchi basi lazima sekta ya uvuvi uiangalie kwa kiwango kikubwa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nikiangalia kwenye sekta hii ya uvuvi lakini kwenye kilimo cha mwani, kilimo cha mwani ni kilimo ambacho kinategemewa sana katika Taifa hili kwa sababu mwani wenzetu wanasafirisha tunasafirisha mwani zaidi Zanzibar kwa matani na matani kuupeleka nje kama nchi ya Philippines, Marekani na Wachina wenzetu nchi hizi wanajikita sana kuuchukua mwani wetu kwa sababu mwani wenyewe ni ubora lakini ni mwani ambao unatengeneza vitu vingi sana na vitu vyenye thamani wanatengenezea Madawa, ni chakula pia unasaidia mwani katika mambo mbalimbali katika kukuza uchumi wao mataifa ya nje zaidi ya China na Philippines. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini pia kama ikiwa tunataka tuwatoe wananchi wetu kwenye dimbwi la umaskini kwa vile nchi tumeitangaza ni nchi ya viwanda Tanzania kwa hiyo sasa tuangalie kujenga viwanda vidogo vidogo vya kuchakata mwani. Kwa sababu kila tukichakata mwani basi mwani unapanda thamani zaidi kulikoni kuuza mwani ambao haujachakatwa. Kwa hiyo, hili tulichukue kama katika mpango wetu tuhakikishe kwamba tunajenga viwanda vidogo vidogo vitakavyoweza kuchakata mwani ambao sasa tutauongezea thamani. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tuangalie tu mwani kama utauponda ponda ukawa kama unga basi thamani yake ni tofauti na mwani unaousafirisha ukiwa katika ma-bundle ambao haujachakatwa hii ni kuonyesha kwamba huu mwani unaweza ukatusaidia sana katika kukuza uchumi na kuwapunguzia umaskini wananchi wetu wa Tanzania kwa jumla. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nikiendelea kuzungumza kilimo cha mwani kule Zanzibar mwani ndiyo kilimo ambacho kinategemewa kwa kiwango kikubwa sana ukienda kama Kisiwa cha Pemba kuna sehemu ya Kiui Minungwini, kuna Maziwa ng’ombe, kuna maeneo ya mkoani huku Kangani maeneo mengi tu ambayo yanategemewa kwa ajili ya kuzalisha huu mwani na wananchi kupata faida. Shida ni kwamba wananchi wetu wanalima kilimo cha mwani bila ya kuangaliwa soko ambalo linaweza kuwakuzisha katika kukuza uchumi wao wa kila siku. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, bahati nzuri mazao ya baharini hayahitaji msimu wa kumwagiliwa humwagilii maji, maji ndiyo wenyewe. Kwa hiyo huhitaji kwenda kumwagilia wala huwezi kusema kwamba kuna ukame bahari haina ukame kila siku inakua kwa sababu mabadiliko ya tabia nchi kila siku kina cha bahari kinaongezeka sasa hii ni kuonyesha kwamba ikiwa tutajikita kwenye kilimo hiki cha mwani na kwa kuhakikisha wananchi wetu tunawawezesha ninaimani kwamba tutaweza kufika pahala pakubwa na uchumi wetu utaweza kukua. ahsante sana. (Makofi)