Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2020 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 pamoja na Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022

Hon. Godwin Emmanuel Kunambi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mlimba

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2020 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 pamoja na Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022

MHE. GODWIN E. KUNAMBI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Nikupongeze kwa kweli unatuwakilisha vema sisi vijana hapo kwenye kiti chako; hongera sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze kwa kumpongeza Mheshimiwa Rais Mama yetu Samia Suluhu Hassan kwa bajeti hii nasema kwa dhati kabisa kuna msemo mmoja wa kingereza unasema all starts well ends well na katka hili niseme bila kuwa na kigugumizi ama kwa hakika legacy ya hayati Dkt. John Pombe Magufuli kamwe haitafutika kwenye ramani ya Tanzania. Kwanini haitafutika tunaye Mama yetu ambaye anakwenda kukamilisha kazi waliyoanza pamoja na hayati Dkt. John Pombe Joseph Magufuli. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, na nimpongeze kwa ubunifu mkubwa Mheshimiwa Rais na kauli yake mbiu ambayo anasema kazi iendelee. Jambo hili la msingi kabisa na kupitia bajeti hii tunaona kwamba bajeti hii imetoa taswira na dira kwa Taifa letu, inakwenda kugusa wananchi wa hali ya kipato cha chini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Lakini unapoongeza ushuru wa forodha kwa bidhaa zinazotoka nje ya nchi maana yake nini? Unalinda viwanda vya ndani lakini pia unaongeza unachagiza ujenzi wa viwanda ndani ya nchi yetu. Kwa hiyo, nampongeza Mheshimiwa Waziri kaka yangu Dkt. Lameck Mwigulu Nchemba kwa dhati kabisa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, niseme kwa dhati hapa waingereza wanasema normally people they do not care how much know until they know how much you care! Maana yake nini siku zote watu huwa hawajali jinsi gani unajua mpaka waone jinsi gani unajali. Mheshimiwa Waziri kaka yangu Mwigulu Nchemba katika hili wewe ni Daktari kweli kweli, siyo wale madaktari wengine wewe ni PHD holder wa kweli kweli. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sababu umetafsiri uchumi wa nchi yetu kwenye bajeti hii, hivi vitu siyo vya kawaida sana ndiyo maana vitu hivi lazima akili kubwa ifanye hivi kwa kweli nakupongeza na pamoja na Naibu Waziri kaka yangu Mheshimiwa Eng. Masauni mchape kazi sisi tuko nyuma yenu tutawaunga mkono. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nawapongeza kwa sababu kuu zifuatazo ya kwanza tunaona leo hii kulikuwa na ugumu wa makusanyo ya kodi ya property tax halmashauri tulipata shida kidogo huko nyuma, baadaye TRA nayo haikufanya vizuri. Lakini leo hii unapokwenda kukusanya kodi za majengo kwa kutumia bill za umeme kwa kweli tunakwenda kukusanya na naamini tunaenda kufanikiwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, na niseme kuna changamoto hapa mbili ambazo watu walikuwa wakizungumza wanasema kuna watu hatutumii umeme tunatumia solar power sijui kuna watu tunaweka umeme kabisa. Nishauri hapa katika watu wa kundi hili tuwaache halmashauri waendelee. Kada hii ya watu ambao wanatumia solar panel na watu wasiotumia umeme au hawajaunganishiwa umeme ile kodi iendelee kukusanywa na halmashauri. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini suala la mpangaji, sijui na mwenye nyumba hii hamna shida hapa ni jambo ambalo linawekwa kwenye mkataba tu na ni mahusiano kati ya mpangaji na mwenye nyumba na mlipaji na mwenye nyumba. Kwa hiyo, ni jambo ambalo yaani hatuitaji akili kubwa sana kwenye tafsiri hili kwa hiyo, nakupongeza sana kaka yangu Mheshimiwa Dkt. Mwigulu muendelee sisi tutaendelea kuwaunga mkono.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini eneo jingine niendelee nijikite kwenye sekta nyingine ni sekta ya ujenzi. Tunapozungumzia sekta ya ujenzi ni sekta muhimu sana kwa ukuwaji wa uchumi wa Taifa letu kwa sababu moja kuu kwanza inakwenda kurahisisha huduma za usafirishaji wa bidhaa, bidhaa kutoka viwandani kwenda kwa watumia lakini bidhaa hasa za kilimo kutoka mashambani kwenda kwenye masoko.

Mheshimiwa Mwenyekiti, niseme tu ninashukuru sana na ninampongeza Waziri wa Fedha lakini pia nampongeza Waziri wa Wizara ya Ujenzi, unavyozungumzia miundombinu unazungumzia pia barabara kuna suala hapa kimsingi limegusa wananchi waJimbo la Mlimba.

Mheshimiwa Mwenyekiti, itoshe tu kusema, Waheshimiwa Madiwani wa halmashauri ya Wilaya ya Mlimba wako kwenye ukumbi wa Spika na wanasikiliza na wenyewe wamekuja kupongeza Wizara hii muhimu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa nataka kuzungumzia nini? Barabara hizi kuu tunaziita barabara za Mikoa zinaunganisha makao makuu ya mikoa na mikoa faida yake ni kubwa mno. Kwa sababu kwa mfano hii barabara inayokwenda kujengwa kutoka Ifakara Mlimba, Madeke, Lupembe mpaka pale Kibena Junction, barabara hii inaunganisha Mikoa miwili, Njombe na Morogoro faida yake ni nini?

Mheshimiwa Mwenyekiti, wananchi wa Jimbo la Mlimba ambao tunatoka Morogoro sisi tunalima Mpunga, lakini wananchi wa Njombe wenzetu wanashughulika na mazao ya mbao kwa hiyo, tutakwenda comparative advantage katika uchumi, maana yake wao wanatupa mbao tunanunua sisi tunawapa mchele wanakula. Kwa hiyo, ni neema kwa wananchi Mkoa wa Morogoro na neema kwa wananchi wa Mlimba lakini haitoshi hata Jirani zetu wa Njombe. (Makofi)

Mheshimiwa mwenyekiti, niende kwenye sekta ya ardhi, nikushukuru tena kwa mara nyingine Mheshimiwa Waziri, kitendo cha kupunguza kwenye marekebisho ya Sheria ya Sekta ya Ardhi tunaona Mheshimiwa Waziri unafanya marekeabisho ya Sheria ya Ardhi Sura Na.113 na unatueleza kwamba tozo ya mbele yaani premium inakwenda kupungua kutoka asilimia 2.5 mpaka asilimia 0.5 jambo hili ni la kheri kweli kweli. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakumbuka na naomba niseme kwa dhati, Serikali hii ni Serikali sikivu katika mchango wangu wa awali nilichangia kwa habari ya eneo hili, mheshimiwa Waziri umesikia na umekwenda kupunguza leo naomba nishauri jambo lingine bajeti ijayo muliangalie hili pia. Kuna hii kodi ambayo tunaita capital gain tax yaani kodi ya ongezeko la mtaji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kodi hii inadumaza sana biashara katika sekta ya ardhi, kodi hii ya asilimia 10, Mheshimiwa Waziri bajeti ijayo nakushauri kaka Mheshimiwa Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba, bajeti ijayo tupunguze kutoka asilimia 10 ije asilimia 5 itasaidia transaction za kuuziana kwenye sekta ya ardhi na ita-bust uchumi wetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini eneo lingine naomba nishauri ni suala zima la upimaji hapa nimeona na nimeangalia takwimu hapa kwenye sekta ya ardhi mwaka wa fedha ukisoma kitabu cha Hali ya Uchumi wa Taifa ukurasa wa 203 inaeleza; Mwaka wa Fedha 2020 viwanja vilivyopimwa nchini na mashamba ni 337,970 kwa mwaka 2020 lakini kati ya hiyo viwanja 90,000 vinatoka Dodoma sawa na asilimia 40 ya upimaji kwa nchi nzima ni takwimu hizi zipo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ndio maana nikasema sasa tunaona umuhimu wa sekta binafsi ku-engage kwenye shughuli za upimaji na upangaji wa nchi yetu. Dodoma tumefikia viwanja 90,000 kwa sababu tumetumia sekta binafsi na niseme tu nitaendelea kusema sitasita kwenye eneo hili. Kwa sababu ni mafanikio kwa Dodoma nchi nzima 300,000, Dodoma 90,000 asilimia 40, kazi imefanyika, hili jambo halihitaji fikra ya juu sana ni jambo la kawaida. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, niende kidogo niguse kwenye eneo la kilimo lakini nizungumzie sana suala la masoko. Mlimba sisi tunalima mpunga sisi hatuhitaji masoko Mlimba, sisi tunachohitaji Mlimba, tunahitaji kuchakata mpunga kuwa mchele. Tufanye packaging transport tuuze Japan tuuze nchi nyingine ili tupate fedha za kigeni. Hili litatusaidia wananchi wa Mlimba sisi hatuhitaji masoko tunahitaji processing, unavyozungumzia kuchakata mpunga ukawa mchele ukafanya packaging uka-brand tutauza ndani na nje ya nchi na namna hii tu tuweze kusema tutapata fedha za kigeni na tutakuwa na favorable balance of payment ndani ya nchi yetu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nirudie kusema, baada ya kuchangia haya kwa kweli, mnyonge mnyongeni haki yake mpeni na niombe kwa Waheshimiwa Wabunge, mama yetu Samia Suluhu Hassan ameanza vizuri anahitaji tumsaidie na kimsingi tumpe ushirikiano wa kutukuka. Hoja yangu ya msingi ambayo leo ninaacha swali kwa kila mmoja wetu, Je. Are we genuine? Swali langu. Mheshimiwa Rais kwa dhati kabisa anahitaji ushirikiano wetu na kumsaidia swali langu niliache hapa leo katika Bunge letu, are we genuine? Ahsante naomba kuwasilisha. (Makofi)