Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2020 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 pamoja na Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022

Hon. Maryam Omar Said

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Pandani

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2020 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 pamoja na Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022

MHE. MARYAM OMAR SAID: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi hii kuweza kuchangia bajeti iliyopo Mbele yetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, awali ya yote nimshukuru Mwenyezi Mungu kwa kuniamsha mzima wa afya na kuweza kusimama hapa leo. Pia niipongeze Serikali kwa kuleta bajeti nzuri ila bado ninahofu na wasiwasi mkubwa, kila ninapoisoma bajeti hii nikiangalia na bajeti zilizopita, kiukweli Napatwa na wasi wasi mkubwa mno, kwa sababu ni tayari mara nyingi sana wananchi kubwa wanalolalamikia ni kupitisha bajeti zetu, ikisha baadaye zikatushinda njia tukawa hatufikii kile kiwango. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, binafsi nitachangia katika maeneo mawili makubwa. Niishukuru bajeti hii ama nimshukuru mama yetu Samia, kwa kutufanyia kazi kubwa katika sehemu ya VAT ya Jamhuri wa Muungano ya Tanzania. Kiukweli tulikuwa katika hali mbaya sana kule Zanzibar kiasi ambacho ilifikia hatuwezi kuutaja Muungano kabisa, ilikuwa tukiutaja Muungano kwa mwananchi wa kawaida anavyokuja juu, unashindwa unafikia hadi unanyamaza kimya. Tumefikia hatua nzuri lakini bado, ni wakati muafaka sasa wa kwenda kumaliza zile kero za Muungano zilizobaki hususan kwenye VAT. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Wazanzibari tunataka tukitoa bidhaa zetu kutoka Zanzibar kuja Tanzania bara basi tusiwe na vikwazo kama vile tunavyotoa Tanzania bara tukapeleka Zanzibar. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la pili, nije katika sensa. Naishukuru bajeti hii imezungumzia vizuri na imetenga pesa ya bajeti kwa ajili ya sensa. Nitakacho kiomba hapa ama nitakachoshauri hapa, ni Serikali kuzipeleka haraka fedha za bajeti ya sensa ya watu na makaazi kwa sababu, mara nyingi sana tunapokwenda kwenye sensa kutekeleza majukumu ya sensa changamoto moja tunayokutana nayo ni elimu ndogo, inafika hadi siku mdau anakwenda kukamilisha yale mahesabu ya sensa unatakiwa uanze na elimu kwanza, unamkuta mwananchi hakuna elimu yoyote aliyopatiwa juu ya sensa, vinginevyo analiingiza suala la sensa katika masuala ya dini na tamaduni, jambo ambalo haliko sawa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naiomba Serikali tujitahidi sana kuzifanyia kazi pesa za bajeti ya sensa zipatikane haraka na elimu ifike kwa usahihi kwa walengwa wahusika zaidi hususan kwa upande wetu wa Zanzibar. Kule kuna changamoto mnajua fika dini ilivyotanda kule Zanzibar, kwa hiyo kila kitu kinaingizwa katika dini, ni wakati muafaka Serikali kutoa elimu kabla ya kwenda kufanya mahesabu ya sensa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya hayo mawili niipongeze tena Serikali kwa kuleta bajeti nzuri hii, nimuombe kaka yangu Mheshimiwa Dkt. Mwigulu Nchemba, nataka uwe mfano Bunge hili la Kumi na Mbili, tukitoka tutoke na kipaumbele kizuri bajeti yetu ifikie kiwango, kile ambacho kwamba tumekipanga. Naamini kabla ya kupitisha hii bajeti ulishazungusa jicho lako Tanzania nzima na ukajua fedha ya bajeti itatokea wapi. Sitaki kwamba nikupe twakimu za kilimo za wizara moja moja hapana, ninachokiomba nataka utuwekee historia ndani ya Bunge hili la Kumi na Mbili. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, bajeti hii iende ikakamilike kwa asilimia 100, tukirudi kule majimboni tuwe tunatemebea vifua Mbele kwa ajili ya bajeti hii. Sikupi pongezi nikupongeza niatakaporu Mungu akiniweka hai, baada ya mwaka huu mmoja nikaiona bajeti hii imefikia wapi, hapo nitakuja kuleta pongezi kwa kaka yangu Mheshimiwa Dkt. Mwigulu Nchemba. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. (Makofi)