Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Viwanda Na Bishara

Hon Lucy John Sabu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Viwanda Na Bishara

MHE. LUCY J. SABU: Mheshimiwa Mwenyekiti, nichukue nafasi hii kuipongeza Serikali ya Awamu ya Tano na ya Sita kwa kazi nzuri katika Mpango wa Pili wa kuimarisha uchumi wa viwanda ambapo viwanda vingi vimejengwa kati ya mwaka 2015 - 2020 vikiwemo viwanda vidogo, vya kati na vikubwa. Tuna imani kwa dhamira ya Rais wetu wa Awamu ya Sita, Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan, kazi iendelee.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nina imani kubwa ataendelea kuweka mkazo mkubwa kwenye ujenzi wa viwanda hasa viwanda vinavyotumia malighafi zinazopatikana nchini Tanzania. Tunaunga mkono viwanda kwa sababu vinasaidia kuongeza thamani ya mazao yanayopatikana hapa nchini mfano; pamba, alizeti, katani na kadhalika, lakini pia kuboresha bei ya mazao kwa wakulima, kwani inaondoa gharama za usafirishaji kwenda nje ya nchi ambapo fedha inakwenda kumlipa mkulima, lakini pia ajira za wananchi za moja kwa moja na zisizo za moja kwa moja.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na pongezi hizo nina mambo machache ya kuishauri Serikali, Simiyu ni mkoa unaoongoza kwa kilimo cha pamba, kutokana na ubunifu wa viongozi wa Simiyu, wakiongozwa na Mheshimiwa Anthony Mtaka na wasaidizi wake waliweza kubuni na kuishawishi Mifuko ya Hifadhi ya Jamii, NHIF, WCF pamoja na Benki ya Uwezeshaji (TIB), TBS, TIRDO, TMDA kuanzishwa kwa kiwanda cha vifaatiba vitokanavyo na pamba; zaidi ya bidhaa 19 vikiwemo taulo za kike. Mkoa na Wilaya ya Bariadi ilitoa eneo lililoko kwenye maeneo yanayofikika na miundombinu ya maji, umeme, mawasiliano na barabara.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Wizara iliunda kampuni na Bodi ya Wakurugenzi, Serikali iliteua wataalamu waanzilishi wa kiwanda hicho na Serikali iligharamia safari za wataalamu kwenda nje kujifunza teknolojia stahiki kwa ajili ya kiwanda hicho na upembuzi yakinifu ulishafanyika, na gharama zote zilizokwisha kutumika ni shilingi milioni 915.98. Michakato yote ilianza toka mwaka 2016/2017 mpaka sasa hamna kinachoendelea.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya wananchi wa mkoa wa Simiyu tungependa kufahamu maelezo ya kina kwa nini kiwanda hicho na ujenzi wake haujaanza?