Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Kilimo

Hon. Francis Isack Mtinga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Mashariki

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Kilimo

MHE. FRANCIS I. MTINGA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuchangia katika Wizara hii ambayo inabeba asilimia 70 ya uajiri wa Watanzania.

Mheshimiwa Spika, Wilaya yangu ya Mkalama ina wakulima wa vitunguuu takribani 250, wanaolima karibia tani kuanzia 24,000 mpaka 94,000. Wakulima hawa wanalima kwa kilimo cha mvua na sio umwagiliaji, hivyo, inapofika wakati wa mavuno vitunguu vinajaa sokoni kwa wakati mmoja na hii inapelekea sasa wanunuzi kuamua wanunue kwa bei gani. Kwa hiyo, unakuta katika kipindi cha mwaka mmoja mkulima mwingine anauza gunia Sh.250,000/= mwingine anauza Sh.20,000/= kutokana na kwamba vitunguu vimejaa sokoni. Pia hali hii inasababisha wale wanunuzi kuamua kipimo cha kununua, mwingine anajaza gunia anaweka na kilemba juu kwa sababu vitunguu vimejaa sokoni. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, naomba Wizara iwaangalie wakulima hawa wa vitunguu kwa kujenga maghala ya kutunzia vitunguu katika Kata yangu ya Mwangeza inayolima vitunguu. Hii itasaidia ili vitunguu vinapovunwa kwa wakati mmoja viwekwe kwenye maghala na viuzwe kwa utaratibu na siyo mtu auze vitunguu shilingi 20,000 kwa sababu vitunguu ni perishable, vinaoza haraka na mkulima anakuwa hana ujanja anapangiwa bei anayotaka mnunuzi.

Kwa hivyo, naomba Wizara ikajenge maghala na maghala ya vitunguu yanatakiwa yajengwe kitaalamu kwa sababu vitunguu ni perishable sio sawa na mahindi, ipeleke nguvu pale nguvu pale ijenge maghala ili kuwalinda wakulima hawa wa Mwangeza na Mkalama ambao wanalima kwa nguvu zao. Ndiyo maana tannage imeshuka kutoka 94,000 mpaka 24,000 kwa sababu hawana uhakika na soko limekuwa kama kamari, mnunuzi ndiye anaamua anunue kitunguu kwa bei gani. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, Wizara katika hotuba yao hawajaongelea kabisa kwa undani suala la kilimo cha mbogamboga na matunda. Katika kata yangu mojawapo ya Gumanga kuna kiwanda kimejengwa cha kusindika mazao ya mbogamboga kwa kutumia wananchi na shirika lisilo la Kiserikali la Helvetas, kiwanda hiki kimegharimu karibu milioni 106 hakifanyi kazi kwa sababu malighafi haipo.

Mheshimiwa Spika, niombe Wizara iwaangalie wakulima wa nyanya wa Gumanga kwa kuwawezesha kwa mbegu bora, visima vya umwagiliaji na utaalam ili kiwanda hiki kiweze kufanya kazi na kitasaidia hata mikoa ya jirani wanaolima mboga mboga na soko litapatikana hili ambalo tunahangaika kuimba sasa hivi kwa sababu kiwanda kimekaa tu hakina kazi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, nikuombe rafiki yangu Bashe pamoja na Waziri, nenda pale Gumanga ukaangalie kiwanda hiki tuwawezeshe wakulima hawa waweze ku- supply material ya nyanya ya kutosha katika kiwanda ambacho wamekijenga wao kwa nguvu zao pamoja na shirika lisilo la Kiserikali. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, vile vile niende kwenye suala la alizeti. Wote tunafahamu shida ya mafuta tuliyonayo na zao la alizeti katika hotuba ya Rais iliyopita lilitajwa kama zao la mkakati. Lakini katika hotuba sijaona huo mkakati jinsi ambavyo umeongelewa vya kutosha. Leo hii wakulima wa Mkalama analima hekari moja anapata gunia tatu. Anaona haina tija kulima kwa sababu tatizo kubwa ni mbegu, mbegu ambayo inaonekana kidogo inafanya vizuri, mbegu ya hysan inatoka nje. Kilo mbili ni 70,000, mkulima hawezi kununua mbegu hii.

Mheshimiwa Spika, niiombe Wizara, wakati mnafanya utaratibu wa kutafuta mbegu na utafiti, basi angalau mbegu hii iangizwe kwa bulk na ikibidi iondolewe kodi ili wananchi waendelee kutumia mbegu hii hysun ili kuweza kupata kipato lakini vile vile kuondoa tatizo kubwa la mafuta katika nchi yetu.

Mheshimiwa Spika, nikuombe sana Mheshimiwa waziri na Naibu Waziri mliangalie sual ahili la hii mbegu ya Hysan. Hakika mkiitupia jicho itashuka bei na itatupunguzia suala zima la tatizo la mafuta. Wakati huo huo, mkifanya utaratibu wa kutosha wa kutafuta mbegu ya kisasa ya utafiti itakayofanyika katika nchi yetu ili zao hili la alizeti liendelee kuwa zao kongwe na zao ambalo litatuondolea shida ya mafuta katika nchi yetu.

Mheshimiwa Spika, sasa hivi Singida, alizetu watu wameshaanza kuacha kulima. Mtu angaalia anapata gunia tatu, bora alime karanga apate gunia 12 au bora alime mahindi apate angalau gunia 10 kuliko analima alizeti anapoteza muda anapata gunia tatu. Tatizo ni mbegu na mbolea na mambo mengine. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, nikuombe sana Mheshimiwa Waziri na Naibu Waziri jambo hili la alizeti hamjaonesha mkakati mnaotaka kuufanya katika kulinyanyua. Hamjaliongelea vizuri katika hotuba yenu nimepitia vya kutosha, hebu mlitazame ili tuweze kuondoa tatizo la mafuta katika nchi hii.

Mheshimiwa Spika, kwa leo niliona niseme hayo. Nashukuru sana kwa nafasi hii. Naunga mkono hoja, ahsanteni sana. (Makofi)