Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Mifugo na Uvuvi

Hon. Zuberi Mohamedi Kuchauka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Liwale

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Mifugo na Uvuvi

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Spika, kwa mara nyingine tena leo nianze mchango kwa kumpongeza Mheshimiwa Waziri na Naibu wake kwa kazi nzuri ya kusimamia Wizara hii. Niwapongeze pia watendaji wote ktika Wizara hii na niwatie moyo kwani changamoto ni sehemu ya kazi yao.

Mheshimiwa Spika, Mkoa wa Lindi ndio mkoa uliopokea wafugaji waliohamishwa toka Ihefu, walipokelewa katika Wilaya za Liwale na Kilwa. Lakini hapakuwa na maandalizi yoyote ya kupokea mifungo. Mfano katika Wilaya ya Liwale vijiji vilivyopangiwa kupokea mifugo ni vijiji vya Kimambi, Ndapata na Lilombe. Lakini sasa mifugo imesambaa kila kijiji, mbaya zaidi vijiji hivyo havijafanyiwa upimaji wa matumizi bora ya ardhi, hivyo kusababisha migogoro mingi ya ardhi inayosababishwa na kutokuwa na mipaka halisi inayoeleweka kisheria.

Jambo lingine hapakuwa na ushirikishwaji wa kutosha kwa jamii hasa katika nyanja za elimu juu ya namna ya kukaa na wafugaji, ukizingatia kwa asili watu wa Kusini si wafugaji. Palihitajika maandalizi mahususi namna ya kupokea mifugo. Hadi leo sisi wakazi wa Kusini hatuoni faida ya kuwa na mifugo kwani hatuna minada, majosho wala malambo.

Hivyo basi naiomba sana Serikali kuleta wataalam wa ufugaji ili kuelimisha wananchi juu ya faida za mifugo, lakini kama haitoshi tunaomba tupatiwe wataalam wa minada ili kufungua minada ambayo itaweza kukuza kipato cha wafugaji na hata Halmashauri yetu ya Liwale.