Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari

Hon. Tumaini Bryceson Magessa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busanda

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari

MHE. TUMAINI B. MAGESSA: Mheshimiwa Mwenyekiti, awali ya yote nikupongeze sana kwa kuchaguliwa na kuteuliwa kuwa Mwenyekiti wa Bunge. Pia nimshukuru sana Mwenyezi Mungu kwa nafasi hii ambayo amenipatia kuweza kuchangia Wizara hii. Wizara hii ni nyeti na yenye mambo ya kisasa nafikiri kuliko Wizara zote. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nitajikita kwenye mambo machache sana, kwanza ni tower sharing, co-location. Nilitegemea kabisa kwa sababu tumeingia kwenye tower sharing au co-location hiyo basi hatuna haja ya kuwa na minara mingi nchini. Kwa mfano, Kiyegeya kuna minara nane, tunategemea minara hii ipungue kwa sababu tunaweza ku- co-locate tukawa na minara miwili ikafanya kazi yote ya minara nane iliyopo na tukaokoa mazingira yetu badala ya kuwa na minara mingi ndani ya nchi ambayo haina kazi kubwa sana tuwe na minara michache na co-location iipunguze hiyo minara.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama tukiipunguza minara hiyo basi tutoe hizo structures huko milimani zisiendelee kuharibu mazingira tuliyonayo na hayo ma-dishes ambayo yanaonekana yatakuwa hayana kazi. Toka tumeanza kufanya co-location ni karibu miaka saba, nane, sina uhakika Wizara ina minara mingapi ambayo imei-demolish na sasa tunajua imepungua kiasi fulani na hali yetu ya mazingira kwenye milima yetu imekuwa bora, sina uhakika sana. Nishauri Serikali tupunguze idadi ya minara kwa sababu tunaweza kufanya co-location au sharing. Sharing itiliwe mkazi ili minara isiendelee kusambaa kila mahali a ku-pollute mazingira yetu, kila mtu anaonekana ana mnara wake na anataka kuwasiliana na wananchi walewale. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini la pili ambalo nataka nilichangie hapa ni mkongo huu, nimesikia unaongelewa sana. Ukienda kule wilayani baada ya teknolojia kuongezeka tunatumia mifumo kulipa, mifumo mingi ya Serikali sasa inatakiwa iwalipe wakandarasi na wananchi, mkongo unapokuwa una shida maana yake ni kwamba kwenye wilaya kule kila anayeenda kufanyiwa malipo anaambiwa leo mfumo hauko vizuri, lakini shida yetu ni huu Mkongo wa Taifa. Inaonekana kabisa inter-connections imeshafanyika mahali pakubwa sana, lakini kuna udhaifu mkubwa sana kwenye maeneo ya vijijini kwa sababu ya uhakika wa hiyo bandwidth ambayo inaenda huko.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tuna maneno mazuri sana tumeyataja, lakini ukienda kwenye wilaya kabisa kule ndani ndani kule ambako ndiyo tunasema Mkongo wa Taifa umefika tumefanya hiyo inter-connection utagundua kuna wakati wanashindwa kufanya shughuli zao kwa sababu leo mtandao uko chini. Niiombe sana na niishauri Serikali ifanye ukaguzi wa kutosha kwenye maeneo hayo ili wananchi waweze kuhudumiwa na teknolojia hii kwa urahisi zaidi badala ya kuingia kwenye tatizo ambalo inaonekana malipo hayawezi kufanyika na vitu vingine vinakuwa vimesimama.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini nirudi sasa Busanda jimboni kwangu, tuna kata 22. Kila nikikimbia kilometa mbili- tatu mtandao unapotea, maana yake coverage yetu ya mtandao ni dhaifu, hiyo radius ya coverage itakuwa ni dhaifu. Niombe sana huu Mfuko wa Mawasiliano (UCSAF) ambapo kazi kubwa nimesoma hapa kwenye hotuba hii inaonesha ni kuimarisha na kuongeza mtandao wa mawasiliano kule vijijini, vijijini mawasiliano bado yana shida.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimesikia wenzangu wanasema wanaomba hata wachangie mafuta ili Mawaziri waweze kwenda, mimi sitachangia. Niombe tu mje muangalie uhalisia kwamba kuna zaidi ya kata 11 mawasiliano yake yana matatizo. Naamini kabisa mkifika huko tuna-test wote tutajua kabisa mahali fulani hakuna mawasiliano na mtaweza kutusaidia. Kwa hiyo, Mheshimiwa Waziri nishauri sasa mizunguko yenu ifike kwenye maeneo yetu ambayo tunawakilisha wananchi waweze kupata kupata mawasiliano, wakipata mawasiliano tutakuwa na uhakika wa mambo kdhaa ambayo sasa hivi hayapo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukiwa kijijini leo, kwa mfano niko Kata ya Nyakagomba ambako natoka mimi, kuna walimu wanataka kufanya application nikimwambia fanya application halafu unirushie hapa, hawezi kurusha. Kwa sababu akifanya application anagundua hakuna 3G kuna 2G, kama kuna 2G maana yake kile anachofanya hakiwezi kuingia kwenye data. Kwa hiyo, tuna shida hiyo kwamba,iko minara ilikwenda vijijini kule, lakini iko kwenye 2G hawajaingia kwenye 3G na huku mbele kwenye 4G na huku tunakokwenda kwenye 5G sasa hivi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, niombe sana mpite kwenye maeneo ya vijijini. Namuona Ndugu yangu hapa Burongwa anagonga mkono, anajua kabisa Burongwa kule 2G ndio iko 3G hakuna. Kwa hiyo, niombe sana tutembeleeni huko tuliko ili matatizo haya ambayo tumeyata hapa tukayaseme na nyie mkiwa mnaona. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi nina kata 13 zinachimba dhahabu. Wanachimba dhahabu, pesa wanayo, hawawezi kuwasiliana vizuri. Nilifikiri ukiwa na pesa inabidi maisha yako yawe rahisi kidogo, unakuwa na pesa lakini na maisha yako yanaendelea kuwa magumu. Niombe sana tufanyiwe huduma hii kama ni UCSAF, kama ni hawa vendors wengine waweze kuja kwenye maeneo yetu kuhakikisha kwamba tunapata mawasiliano. Tukishayapata hii kasi ya maendeleo na mchango wa sekta hii ambayo najua unaendelea kukua haraka kwenye pato la Taifa, niwaombe sana tuweze kuweka mchakato wa kutosha kuhakikisha kwamba wananchi wote wanaweza kupata mawasiliano na mwisho wa siku tutaona maendeleo yetu yanakwenda kasi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, wenzetu kwenye mawasiliano sasa hivi wanaweza kufanya operation, mtu akiwa South Africa anaweza kufanya operation Benjamin Mkapa akiwa kwenye mfumo huu. Sasa kama tutaonekana kwamba sisi mawasiliano yetu ni dhaifu maana yake akianza kufanya operation kuna mahali patakatika na huyu mgonjwa atafia kitandani huyu. Kwa hiyo, niombe sana tuwe na stable communication, lakini coverage yetu sasa iongezeke. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya maneno haya, naomba kuunga mkono hoja. (Makofi)