Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Maji

Hon. Hamida Mohamedi Abdallah

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Lindi Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Maji

MHE. HAMIDA M. ABDALLAH: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi niweze kuchangia hoja iliyopo mbele yetu. Kwanza nianze kwa kumpongeza Mheshimiwa Waziri na Naibu Wake na timu yake ya wizara yake kwa namna ambavyo wanachapa kazi, lakini kwa namna ambavyo wamejiandaa na bajeti hii ya 2021/2022.

Mheshimiwa Spika, bajeti hii imegusa kila eneo na imezingatia changamoto mbalimbali ambazo Waheshimiwa Wabunge tulikua tunampelekea Mheshimiwa Waziri hoja mbalimbali. Kwa hiyo, nimshukuru sana lakini nimtakie kila kheri katika utekelezaji wa kipindi hiki cha mwaka 2021/2022.

Mheshimiwa Spika, yako mambo mbalimbali ambayo yako ndani ya mpango huu wa bajeti ambayo itatekelezwa katika kipindi hiki. Naomba nishauri tunamuomba Waziri wa Fedha ajitahidi sana kutoa fedha kwa wizara hii iweze kutekeleza mipango yake ambayo himo katika mpango huu wa mwaka 2021/2022 kwasababu kuna mambo mazuri yanayokwenda kupunguza kero mbalimbali ya changamoto hii ya maji, sasa utekelezaji huu utazingatia upatikanaji wa fedha. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, ninaiomba sana Serikali kupitia Wizara ya Fedha kutoa fedha kwa wakati kuhakikisha kwamba Wizara ya Maji inapata fedha na inakwenda kuteleza miradi hii ya maji. Niishukuru Serikali kwasababu Lindi tulikuwa na changamoto kubwa ya maji katika eneo Kata ya Rasibula Mtwero, lakini tayari tuko katika mpango huo wa utekelezaji kikubwa ni upatikanaji wa fedha tukatekeleze huu mradi wa maji kuhakikisha kwamba Mitwero, Kikwetu na Mchinga changamoto ya maji inaondoka.

Mheshimiwa Spika, changamoto kubwa iliyopo Lindi Manispaa ni uwepo wa gari maji taka, lakini nimshukuru sana Waziri lakini niishukuru Serikali kwamba tayari tupo katika mpango wa utekelezaji wa ununuzi wa gari la maji taka ili kuhakikisha kwamba Lindi Mjini tunakuwa na gari la maji taka na kufanya utekelezaji wa maji taka ili kuweka mji wetu kuwa salama na wananchi wetu waendelee kuwa salama.

Mheshimiwa Spika, tunaamini kwamba uwepo wa maji duniani ni jambo kubwa ni jambo jema kwasababu mtu unaweza ukose umeme lakini usikose maji, unaweza ukose barabara lakini usikose maji, kwa hiyo, tunajua kwamba katika matumizi makubwa ya binadamu na shughuli za binadamu zinategemea sana uwepo wa maji. kwa hiyo, niitakia kila kheri Serikali yetu kuhakikisha kwamba inapata fedha za kutosha na kuweza kwenda kutekeleza miradi ya maji. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, tulikuwa na miradi ya maji ambayo ndugu zetu hawa la LUWASA walitekeleza kuweka viura katika mitaa, lakini ninajua kwamba Serikali ina nia njema ya kumtaka kila mwananchi aweze kuvuta laini ya maji nyumbani kwake ili afanye matumizi yake mwenyewe. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, changamoto iliyopo ni kwamba maeneo ambayo yamepita mainline za maji inakuwa na umbali mkubwa kiasi kwamba mwananchi anashindwa kugharamia kuvuta maji kutoka kwenye connection mpaka nyumbani kwake gharama zinakuwa kubwa mno, lakini ukiangalia mabomba ambayo yanatoa huduma na wenyewe LUWASA nayenyewe yanakuwa na gharama kubwa ukilinganisha na bei ya madukani kwa hiyo tuangalie katika eneo hili ili tuhakikishe kwamba wananchi wetu wanaweza kumudu kuvuta line za maji manyumbani kwao. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, ninaiomba Serikali kwenda kuhakikisha kwamba hasa Waziri na Naibu wake na timu yake katika utoawaji wa majisafi na salama ambayo tunapata huduma kutoka kwenye viwanda mbalimbali, maji mengine yanakua na chloride nyingi sana kiasi kwamba ukunywa yanakuwa chungu, kwa hiyo, ninamuomba Mheshimiwa Waziri aende akakaguwe ili kuangalia viwango vya ubora wa maji haya na kuweka hali za wananchi wetu ziendelee kuwa salama. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, baada ya kusema hayo niendelee kuishukuru sana Serikali lakini niendelee kuwatakia kila kheri ili mipango yetu iliyomo katika bajeti hii tuweze kutekeleza kwa kipindi hiki cha 2020/2021. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, baada ya kusema hayo nakushukuru sana ahsante sana. (Makofi)