Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Maji

Hon. Saashisha Elinikyo Mafuwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Hai

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Maji

MHE. SAASHISHA E. MAFUWE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ili niweze kuchangia kwenye Wizara hii muhimu sana. Kwanza nianze kwa kumpongeza sana Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambaye amebeba dhana hii ya mahitaji ya maji kwa Watanzania na kwenye hotuba yake akaeleza kinagaubaga kwamba ataenda kusimama kuhakikisha Watanzania wanapata maji.

Mheshimiwa Naibu Spika, kama niliwahi kusema hapa sio mzuri sana wa kusifiasifia, lakini huwa nasifia kwa sababu. Sasa naomba sana nimsifie Mheshimiwa Waziri kwa namna ambavyo anapambana na wale wazinguaji, hongera sana. Pia Naibu Waziri kwa kazi nzuri aliyoifanya wakati amekuja kwenye ziara yake pale Hai. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, pale Hai tulikuwa na watu wanaotuzingua sana kwenye zile Bodi za Maji walikuwa na utaratibu wao wamejiwekea, wanalazimisha wananchi kununua vifaa kwenye maduka yao, lakini alivyokuja pale alitoa tamko la Serikali na leo wananchi wa Hai wanafurahia, wananunua vifaa kwa bei ya soko na sehemu wanayoitaka, nipongeze sana kwa hilo. Nipongeze ziara ya Naibu Waziri pia ilinisaidia sana tukapata maji kule Rundugai. Sio hivyo tu nafahamu kwamba chanzo chetu ambacho kilikuwa kimesimama muda mrefu pale Kikapu Chini na chenyewe kimetengewa fedha. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, niombe sana pamoja na hayo mazuri machache ambayo wameyafanya ndani ya Jimbo la Hai, lakini bado tunayo changamoto kubwa ya maji. Wakati wa kampeni, Mheshimwa Hayati Dkt. Pombe John Pombe Magufuli, aliwaambia watu wa Hai wakati anaomba kura, mmenifunga kwa kipindi cha muda mrefu, naomba nileteeni Saashisha na Madiwani wake mnifungue niwaletee maji. Sauti hiyo bado ipo kwenye mwangwi wa masikio ya watu wa Hai, pale Jimbo la Hai tunashida ya maji sana nadhani na sisi tunapaswa kuingizwa kwenye maajabu ya dunia, kwa sababu tunavyo vyanzo vya maji vya kutosha.

Mheshimiwa Naibu Spika, Mlima Kilimanjaro unatiririsha maji mazuri ya kunywa lakini tunalia kwamba Jimbo la Hai hatuna maji. Chini wataalam watatuambia tuna maji ya kutosha, lakini hatuna maji, hususani kata za tambarare, kuanzia Kata ya KIA, Muungano, Bondeni, Boma Ng’ombe, Weruweru, Rundugai, mpaka Mnadani hakuna maji; nazungumza hakuna maji kabisa na Mheshimiwa Waziri anajua. Tunafahamu kulikuwa na jitihada mradi mkubwa wa Serikali wa kupeleka maji Arusha, nikawaomba jamani huwezi kupeleka maji Arusha ukaacha watu wa Hai hawana maji, kuna visima 18 vinachimbwa ndani ya Wilaya ya Hai, lakini vinapeleka maji Arusha.

Mheshimiwa Naibu Spika, tunawapenda sana ndugu zetu wa Arusha, lakini nashukuru nilizungumza na Mkurugenzi wa Mamlaka ya Maji Arusha akaniahidi kwamba vyanzo vile vya maji vitapitisha maji pale Hai. Hili ni jambo la sera ya maji kwamba maji yanapogundulika yanaanzia basi wale wanufaika wapate maji. Niiombe sana Serikali pamoja na kwamba najua ni gharama kubwa kuyaleta maji pale lakini chanzo hiki kitumike watu wa Bomba Ngombe na KIA waweze kupata maji, maana hii ndio changamoto kubwa tuliyonayo Mheshimiwa Waziri.

Mheshimiwa Naibu Spika, suluhisho lingine ambalo tunaweza kutumia tuna chanzo cha hakika na kimeshafanyiwa upembuzi yakinifu, thamani yake ni bilioni 3.5. Hii Serikali ya mama Samia Suluhu ina hela, tunaomba watusaidie pale fedha za kutosha. Nafahamu jitihada ambazo wamefanya wametutengea milioni 500, milioni 500 kwenye bilioni tatu bado ni ndogo. Niombe sana kama inawezekana kwa level ya Wizara tafuteni mkandarasi, chanzo hiki kianze kujengwa, tuna shida kubwa ya maji na kwetu kukosa maji wakati tunaona Mlima Kilimanjaro pale na tunaona vyanzo kibao vya maji kwa kweli ni aibu niombe sana Mheshimiwa Waziri atusaidie.

Mheshimiwa Naibu Spika, jambo lingine, tunazo Bodi za Maji pale. Bahati nzuri baada ya ziara ya Naibu Waziri tulifanya vizuri sana, tukarekebisha zile bodi. Niombe zile bodi zinaweza kulelewa vizuri na zikafanya vizuri sana. Kihistoria tumeanza nazo tangu tukiwa watoto. Kwa hiyo niombe Waziri asiziguse sasa hivi kwa sababu zimeanza kufanya vizuri.

Mheshimiwa Naibu Spika, eneo lingine niombe, wakati Mamlaka ya Maji Wilaya ya Hai haijaanzishwa tulikuwa na mali zetu na hapa nilizungumza na Waziri, naomba nirudie tena kusema, tuna mali zetu zilipelekwa Mamlaka ya Maji Moshi Mjini, pesa taslimu milioni 357 na ushee, lakini kulikuwa na madeni ya milioni 300 ambayo waliambiwa wakakusanye, kulikuwa na magari sita, kontena ambalo lilikuwa na vifaa vya watu wa Hai vyenye thamani ya bilioni mbili.

Mheshimiwa Naibu Spika, eneo lingine niombe, wakati Mamlaka ya Maji Wilaya ya Hai haijaanzishwa, tulikuwa na mali zetu. Na hapa Waziri nilizungumza na wewe, naomba nirudie tena kusema; tuna mali zetu ambazo zilipelekwa Mamlaka ya Maji Moshi Mjini; pesa taslimu milioni 357 na ushehe. Kulikuwa na madeni ya milioni 300 ambayo waliambiwa wakakusanye; kulikuwa na magari sita; kulikuwa na kontena ambalo lilikuwa na vifaa vya watu wa Hai vyenye thamani ya bilioni 2.

Mheshimiwa Naibu Spika, niombe Serikali itujereshee vitu vyetu, hizi ni hela za watu wa Hai na Siha ambazo waliweka ili ziweze kuwahudumia kwenye eneo la maji. Na nina wasiwasi na hizi fedha kama kweli bado zipo, kwa hiyo niombe sana Mheshimiwa Waziri utakapokuja kuhitimisha hapa utuambie hizi fedha zetu tutazipata lini. Kwako siwezi kushika shilingi kwa sababu wewe na Naibu Waziri mmetusaidia sana watu wa Hai.

Mheshimiwa Naibu Spika, eneo lingine ambalo ninataka nichangie; hivi karibuni tumepata mafuriko makubwa ndani ya Jimbo la Hai. Mafuriko haya yamesababisha maafa makubwa; tumepoteza ndugu zetu watatu, na nyumba karibu 1,500 watu wamekosa sehemu ya kuishi, kwa hiyo, sasa hivi kule tuna njaa haswa. Tunashukuru Serikali imetupelekea chakula lakini bado wananchi tathmini ya mazao yao na vitu vingine vilivyoharibika havijaguswa.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini kwenye eneo la maji tuna vyanzo ambavyo vimeharibika na hakuna maji kabisa. Mto wa Nau ambao ni chanzo cha maji hakuna maji kwasababu kimeharibiwa na mvua; Mto wa Semira chanzo kile cha maji kimekufa; Mto Alonzo chanzo cha maji kimekufa; Makoa chanzo hiki kimekufa; pale Kalali tuna chanzo chetu cha maji na chenyewe kimekufa.

Mheshimiwa Naibu Spika, ninaomba sana wananchi wanalia, shule za sekondari pale Msufini hakuna maji, pale Kalali hakuna maji, shule nyingine za Machame Girls na shule kubwa hizi zote hakuna maji kwasababu vyanzo vile vya maji vimeharibika sana.

Mheshimiwa Naibu Spika, na miundombinu hapa katikati ukiachilia kule kwenye vyanzo vya maji na vyenyewe vimeharibila kwasababu ya mvua hizi. Kwa hiyo, niombe sana Serikali iingilie kati iturejeshee maji. Ukanda huu wa juu hakuna maji, kule chini hakuna maji, lakini kama nilivyosema vyanzo vya maji ni vingi sana.

Mheshimiwa Naibu Spika, hili ni shauri, ni kwa faida ya nchi si kwa Jimbo la Hai tu. Hapa tuna mahitaji ya maji lakini vifaa vya kusababisha tupate maji ni ghali mno; tuone namna ya ku-regulate bei za hivi vitu kwa kupitia ruzuku, watu watuletee vifaa vya kuchimba kisima na mitambo hii ili tuondoe tatizo hili kwa level ya Kitaifa.

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. (Makofi)