Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

Hon. Anatropia Lwehikila Theonest

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

MHE. ANATROPIA L. THEONEST: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kupata hii fursa ya kuchangia katika Wizara ya Elimu. Niungane na maoni ya wasemaji wengi na mmoja wao ameongea mchana akieleza umuhimu wa Wizara ya Elimu kuondosha fedha ya mikopo ambayo ni zaidi ya shilingi bilioni 500 ambazo zinakuwa zinahesabika kama fedha ya maendeleo. Hiyo fedha inaonyesha kwamba bajeti ya Wizara inakua; bajeti ya Wizara ni kubwa, lakini katika uhalisia wake bajeti inakuwa ni ndogo.

Mheshimiwa Naibu Spika, mfano katika mwaka uliokwisha, kati ya miradi 33 ambayo mliahidi kuitekeleza, ni miradi sita tu imetekelezwa ambayo ni sawa na asilimia 18. Sasa hiyo inatosha kuona kwamba bajeti inaonekana iko kubwa, bajeti inajitosheleza lakini fedha inaenda kwenye kukopesha wanafunzi. Hiyo kwa nini haipo kwenye Wizara nyingine? Mbona tunaona hiyo fedha ya mafunzo, fedha ya kufanyia activities nyingine inakuja kama OC, lakini ikija kwenye Wizara ya Elimu, inaonyesha kwamba ni fedha ya maendeleo. Nadhani tusifanye hivyo ili tupate picha halisi, tujue kama fedha haitoshi tupambane ili tuweke fedha za kutosha. Mimi ndiyo wito ninaoutoa. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, hili suala tumekuwa tukiliongelea humu siyo mara ya kwanza. Kwa hiyo, nitapenda Wizara itueleze, hicho kigugumizi kinatoka wapi? Kwa sababu, hii siyo mara ya kwanza, wala ya pili na aliyeisema hapa alikuwa Mbunge ambaye ni mgeni. Kwa hiyo, ina maana na yeye kwake ni concern na kwetu ni concern. Ina maana Wizara haipati fedha ya kutosha. Tukija hapa tunaona kwamba fedha ya maendeleo ni shilingi bilioni 900, lakini in reality ni kama shilingi bilioni 405 ambayo ni tofauti sasa na fedha ya mikopo.

Mheshimiwa Naibu Spika, hapo hapo niungane na waliongea kwamba lazima vyuo vya kati vipewe mikopo, kwa sababu actually wale watu ndio tunaowahitaji kwa sasa. Leo nimesoma taarifa ya CAG kwamba, sokoni kwa maana ya ma-graduate, wanakuja kama 100,000 au 150,000 plus. Katika miaka hii mitano ina maana udahili umeongezeka, tunazidi kutengeneza ma- administrator badala ya kutengeneza watu wanaoenda kufanya kazi.

Mheshimiwa Naibu Spika, hebu tuwape wale vijana fedha na tunao wengi kwa sababu ya mfumo wetu wa elimu ambao sijui kama muda wangu utanitosha, lakini ningependa kuongelea mfumo wa elimu tulionao sasa. Hiyo ni ya kwanza, kuondoa kutengeneza fungu special kwa ajili ya hiyo mikopo badala ya kuiacha kwenye kifungu cha maendeleo.

Mheshimiwa Naibu Spika, kabla sijaenda mbali sana, niongelee changamoto ya Wilaya ya Kyerwa. Mimi ni Diwani katika Halmshauri ya Kyerwa na ninajua Wizara ya Elimu ndiyo ina-deal na kudhibitisha sasa kwamba shule iwe-accredited sasa iweze kuwa-admit wanafunzi na ipate usajili. Kyerwa tuna changamoto ya shule nyingi ambazo hazijawa accredited. Mfano, kuna shule inaitwa Isihoro, ipo Kata ya Mrongo. Hiyo shule wazazi wamechangishana wenyewe. Ina vyumba takribani viwili mpaka tatu na ina vyoo. Ila hiyo shule haijaweza kuanza. Watoto wa maeneo hayo wanatembea zaidi ya kilomita nane kwenda kutafuta elimu, siyo sawa.

Mheshimiwa Naibu Spika, sitaki kurudia aliyoyasema Mheshimiwa Spika; wakati wazazi sasa wanaona shule imeanza, wanapata morali ya kuendelea kujenga zaidi, lakini na Serikali itaanza kuweka jicho lake pale, lakini tukiendelea kuyaacha yale yakiwa magofu, tutakuwa tunasaidia nini? Hatupeleki walimu, hatupeleki capitation fee na majengo hayaendelei na juhudi za wananchi zinakuwa hazina maana.

Mheshimiwa Naibu Spika, siyo ya Isihoro tu, hiyo ipo pia Kashanda. Nimefanya ziara, nimefika kwenye Kata ya Kakanja. Pia kuna shule inaitwa Nyakagera, nimefika. Hiyo shule sasa wamemaliza hadi Darasa la Saba, badala ya kufanyia mtihani pale kwa sababu hajijasajiliwa, wanaenda kufanyia mtihani kwenye Kata ya Kakanja, nadhani siyo sawa.

Mheshimiwa Naibu Spika, ni lazima tutengeneze utaratibu, ambao at least ameeleza vizuri Mheshimiwa Mwalimu Tunza, kwamba hata tunavyokuwa tunasajili, basi tutengeneze standard kwamba, hii imesajiliwa lakini bado inachangamoto ABC lakini naweza kuruhusiwa kuendelea na kazi nyingine. Hiyo ipo pia huko Kata ya Kichenkura, iko Chakalisa Kata ya Kimuli, iko Kashasha, Kata ya Kibale; Muhulile, Kata ya Nkhwenda; na Chaju Kata ya Mabira. Kwa hiyo, natoa picha mwone sisi Kyerwa kama Halmashauri kama Wilaya tuna changomoto kubwa kiasi gani. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nichomekee hapo hapo, Mheshimiwa Waziri wewe ni mwanamama; unapoenda kugawa hizo sekondari za bweni 26 kwenye mikao mbalimbali, tunaomba Kagera hiyo sekondari ijengwe kule Kyerwa. Ninaomba hayo kwa sababu ukija kuangalia jiografia ya mkoa wetu Kyerwa ni kama imeachwa pembeni. Ni wakati huu tu zile shule za sekondari zimepandishwa hadhi na kuwa high school. Miaka yote hatuna Kidato cha Tano wala cha sita. Kwa hiyo, watoto wa kike wa maeneo yale ni watu ambao kama hawakupewa kipaumbele. Tuna ardhi ya kutosha, tuna eneo la kutosha, hebu tupeni hicho kipaumbele, tutawalipa matokeo ninakuomba sana.

Mheshimiwa Naibu Spika, nirudi pia kwenye ambayo wamesema wenzangu. Tuangalie dira ya elimu vis a vis output, nimepitia kama alivyoongea Mheshimiwa Askofu Gwajima na Mheshimiwa Nusrat. Wamesema Dira ya Elimu inasema ni kuwa na Mtanzania aliyeelimika na mwenye maarifa, stadi, umahiri, uwezo na mtazamo chanya ili kuweza kuchangia katika kuleta maendeleo ya Taifa. Twende kwenye dhima, kuinua ubora wa elimu na mafunzo na kuweka mfumo na taratibu zitakazowezesha kupata idadi kubwa ya wanafunzi walioelimika. Sitaki kuendelea, lakini Wabunge wengi wameongelea hapa, wanasema Sera yetu ya Elimu ya 2014 ina matatizo.

Mheshimiwa Naibu Spika, kama kila Mbunge anayesimama anaongea, Serikali inapata kigungumizi gani kurudisha mchakato na wananchi wakashiriki ili tuone aina ya elimu tunayoitaka? Mimi sioni kama sera inaongea vibaya, dhima sioni kama inaongea vibaya, lakini ukiangalia output, kwa nini hai-respond sera inasema nini? Ina maana kuna tatizo somewhere. Aidha ushiriki wa wadau au wameshindwa kuwa compatible, ina maana lazima tutafute solution ya kudumu pale. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, mfano mwingine ambao nitataka kuusemea kwa mfano mfupi tu leo, elimu yetu ya Tanzania tuliyonayo leo ni ya ku-pass mitihani. Ukiangalia humu ndani utaona watu wana ma-degree, watu wana vyeti, watu wana Ph.D, lakini anaelewa nini? Hilo ni swali kubwa ambalo huwezi kulijua.

Mheshimiwa Naibu Spika, mama ni mwalimu; mimi ni mwalimu pia, degree yangu ya kwanza nimesoma Ualimu. Tulifundishwa kwamba elimu ni kile ambacho kinabaki kichwani baada ya vile vyote ulivyofundisha kusahaulika. Sasa sisi tunaoenda kukusanya vyeti, unachokifanya ni kukariri tu; examination, examination and passing the exam. Unapewa cheti, biashara imeishia hapo. Ni lazima tuangalie sera yetu ya 2014, ni lazima tuangalie dira yetu tuweze kuvioainisha hivi vitu.

Mheshimiwa Naibu Spika, nitaongea kitu kingine. Leo tuna waandishi kadha kadha wa vitabu, lakini mmewahi kuona standard za vitabu vinavyoandikwa? Mmeshaona vitabu wanavyovisoma wanafunzi? Vitabu vingine ni matangopori, yaani matangopori pa pa pa! Nakumbuka tukiwa Advance na O’ Level tulisoma vitabu vya Nyambali Nyangwine, mwalimu anakuja anasema vyote vile mlivyosoma ilikuwa ni OP (out of point). Sasa leo tumeweka censorship ipi ya kuona vitabu wanavyovitumia wanafunzi wetu ni sahihi?

Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. (Makofi)