Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira

Hon. Maryam Azan Mwinyi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Chake Chake

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira

MHE. MARYAM AZAN MWINYI: Mheshimiwa Spika, ahsnate sana kwa kunipa nafasi hii ambayo ni ya upendeleo, hasa kutoka Pemba. Kwa kuchangia hotuba ya Ofisi ya Makamu wa Rais ya Muungano, mimi hasa najikita katika mazingira.

Mheshimiwa Spika, Serikali ya Jamhuri ya Muungano imetoa mwongozo kufanya vikao katika taasisi mbili kutoka Zanzibar na kutoka Tanzania Bara ili vikao hivi viweze kuleta tija kwa Watanzania wote. Sasa tatizo ni hili ambalo vikao vinachelewa sana kufanywa katika Serikali zetu hizi mbili. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, vikao hivi vitasaidia kujadili pamoja mambo mengi na fursa nyingi za Tanzania Bara na Tanzania Zanzibar, hasa kwenye miradi ya mazingira. Pia kuwe na ushirikiano wa kupatiwa taarifa ya Tanzania Bara na Tanzania Zanzibar, vipi inanufaika katika mikataba ya mazingira inayoridhia ili taarifa hizo ziweze kuwasaidia wananchi wa Tanzania yote; Tanzania Zanzibar na Tanzania Bara.

Mheshimiwa Spika, wananchi hao waweze kufahamu fursa ambazo Serikali zetu zinaimarisha Muungano kwenye sekta ya mazingira. Kwa hiyo, tunamwomba Mheshimiwa Waziri katika Wizara hii alichukulie kuwa ni muhimu sana katika sekta hiyo ya kufanya vikao na kutoa taarifa katika nchi yetu kwa Tanzania Bara na Tanzania Visiwani ili Muungano huu uzidi kudumu na kuimarishwa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, ahsante sana na naomba kuunga mkono hoja. (Makofi)