Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira

Hon. Issa Ally Mchungahela

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lulindi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira

MHE. ISSA A. MCHUNGAHELA: Mheshimiwa Spika, awali ya yote namshukuru Mwenyezi Mungu Mwingi wa Rehema kwa kuniwezesha kuwa hai hivi leo na kuchangia hoja hii ambayo ni hoja muhimu sana. Pia nawashukuru wale wote waliowezesha kwa namna moja ama nyingine kunifanya nikachangia hivi leo. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nataka nizungumzie hali halisi ya mazingira ambayo nafikiri kwa namna moja au nyingine Serikali haijafanya jitihada za kutosha sana kuangalia hiyo halisi na kuangalia jinsi gani ya kutatua tatizo hili la mazingira.

Mheshimiwa Spika, mfano katika mji wa Dar es Salaam, tafiti zinatuonyesha kwamba tani 5,600 za uchafu zinazalishwa; na uchafu wenyewe umejikita sana kwenye takataka za plastic. Pia tafiti hizo hizo hizo zinatuonyesha kwamba asilimia 30 mpaka 40 ya taka ngumu zinakuwa ndiyo peke yake zinaweza kupelekwa maeneo ya kutupa (dump) na dampo kwa Dar es Salaam liko moja tu, Pugu Kinyamwezi. Sasa ukiangalia asilimia iliyobakia ni takataka ambazo zenyewe hazina uhakika wa kwamba zinapelekwa wapi. Unaweza ukaona kwa jinsi gani hali ilivyokuwa ngumu hapo.

Mheshimiwa Spika, hali halisi pia inaonyesha kwamba kwenye beach za Mkoa wa Dar es Salaam kuna takataka takribani mifuko 150 mpaka mifuko 200 ambazo zinatolewa kila siku, yaani wale watu wanaojishughulisha na utoawaji wa taka, kila siku wanafanya kazi ya kutoa uchafu huo. Katika hali hiyo, tunahitaji kujielekeza sana kwenye jitihada ya kuzoa takataka. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, jitihada ambayo nayotaka ni-stick, ziko mbili ya kwanza kabisa ni kwenye suala la elimu. Tumejikita sana katika utatuzi wa kutengeneza miundombinu mikubwa mikubwa. Tnafikiria vitu vikubwa badala ya kufikiria vitu vidogo ambavyo vitatuwezesha kufanya suala hili kwa umakini kabisa. Kama tumeamua kutoa elimu, basi tuelekeze elimu yetu kwa sehemu kubwa kabisa kwa vijana, kwenye shule za msingi.

Mheshimiwa Spika, nashauri moja kwa moja tuwe na somo la mazingira. Lichukuliwe kama ni somo linafundishwa kuanzia Darasa la Kwanza, kwa sababu tunajua vijana wadogo ndio wanaoweza ku-pick suala lolote kwa uharaka zaidi. Wanajifunza kwa uharaka zaidi na kulitendea kazi; na kwa sababu wao ndio wenye nchi yao au dunia yao ya kesho; kwa sababu siyo dunia yetu, ni dunia yao wao, kwa hiyo, tukiwafundisha wao nafikiri itakuwa vizuri zaidi. Tutumie fedha nyingi katika eneo hili.

Mheshimiwa Spika, sehemu nyingine nashauri tuwamilikishe uchafu wale wanaotengeneza uchafu. Kama tutafanya jitihada hii, tutahakikisha kwamba mazingira yanakuwa safi. Hapa najaribu kuzungumzia kitu gani? Kwa mfano, tunajua kuna watu wanatengeneza maji, wanatengeneza juice, lakini kiuhalisia siyo kwamba wanatengeneza maji, isipokuwa wanatengeneza uchafu wa plastic, vile vifaa wanavyovitumia katika kuweka hayo maji au kuweka hivyo vitu vingine.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, lazima tufanye jitihada kuwamilikisha uchafu. Katika njia gani? Kuwaambia kwamba uchafu ule ni mali yao, wahakikishe kwamba kwa namna moja au nyingine, uchafu wowote utakaonekana sehemu yoyote ile unawahusu wao. Nao lazima wawajibike katika kuhakikisha uchafu ule wanauondoa. Kwa hiyo, njia mojawapo ni kuweka bei, kwa mfano bei ya maji shilingi 600, lakini iwekwe kama shilingi 100 iwe ni pesa ku-retain ule uchafu.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, mtu anayekuja kununua maji, ananunua kwa shilingi 600 lakini shilingi 100 ni gharama ya kutolea uchafu pale. Kwa hiyo, nafikiri kwa namna hiyo tunaweza kuwa na uhakika wa kuondoa uchafu ambao unazagaa kiholela.

Mheshimiwa Spika, jambo lingine ninalotaka kuzungumza ni kuhusu sera. Sera zetu lazima zihakikishe zinaangalia ajira za watu wa kutoa uchafu zinathaminiwa. Tuhakikishe kwamba kwa namna moja ama nyingine watoa uchafu wanaajiriwa kwa kuwawezesha kwenye miradi midogo midogo.

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

MHE. ISSA A. MCHUNGAHELA: Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja kwa asilimia mia moja. Ahsante. (Makofi)