Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira

Hon. Eng. Mwanaisha Ng'anzi Ulenge

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira

MHE. ENG. MWANAISHA N. ULENGE: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa nafasi hii ya kuchangia katika Wizara hii ya Makamu wa Rais, (Mazingira na Muungano). Awali ya yote nichukuwe fursa hii kuwapongeza Mheshimiwa Waziri kwa hotuba nzuri, pamoja na Mwenyekiti wa Kamati husika. Naomba nichangie kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kuna suala zima disaster preparedness. Tumesikia sasa hivi kwenye mitandao wakizungumzia suala nzima la Cyclone ya Jobo, lakini hii inatokana na sawa sawa na yaliyosemwa kwenye ripoti ya Intergovernmental Panel on Climate to Change (IPCC) ambayo inazungumza suala zima la ongezeko la joto pamoja na ambazo zinaleta mvua nyingi, lakini imekuwa ni Mamlaka ya Hali ya Hewa peke yake inayoonekana inashikilia kidedea suala hili.

Mheshimiwa Spika, upande huu wa athari za mazingira zinazotokana na mvua nyingi na kupelekea mafuriko, upande huu wa Wizara hii ya Mazingira haitoi ushirikiano wa bega kwa bega na hali ya hewa kuhakikisha kwamba wananchi wanaandaliwa kwa hali kama hizi za mabadiliko ya hali ya nchi ili kuendelea kuishi salama hasa wananchi wanaoishi pembezoni mwa Bahari za Hindi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, jambo hili ni la muhimu sana kwa sababu imeshatokea, maeneo ya karibu na bahari yanamomonyoka. Kwa mfano, Chuo cha Mwalimu Julius Nyerere pale Kigamboni, ilitokea ndani ya Dar es Salaam Road mpaka kile chuo kikataka kuezuliwa. Kwa hiyo, suala hili ni muhimu kabisa, kuandaa wananchi waishio pembezoni mwa bahari ili kuweza kujikinga na vimbunga hivyo vinavyoweza kutokea.

Mheshimiwa Spika, naomba pia kuchangia kuhusiana na kumomonyoka kwa Kisiwa cha Toten kilichopo Mkoani Tanga. Tanga tumebarikiwa, tuna kisiwa kizuri na Mamlaka ya Bandari wanakitumia kisiwa kile, wametengeneza mnara unaoongoza meli unaoitwa mnara wa Ulenge juu ya kisiwa kile, lakini kisiwa kile kina erode na hakuna measures zozote ambazo zinachukuliwa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, naiomba Sekta ya Mazingira ikashirikiane na Mamlaka ya Bandari itengeneze shoreline protections kwenye bahari zetu ili kuendelea kuvikinga visiwa vyetu pamoja na maeneo yaliyoko kwenye mwambao wa bahari. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, naomba pia nichangie kuhusiana na suala nzima la asbestos. NEMC walishaweka hii sheria ya kwamba asbestos ni harmful kwa maisha ya binadamu, lakini mpaka sasa yapo majengo mengi ambayo yameezekwa na asbestos na hata kwenye mabomba, underground utilities zipo ambazo ni za asbestos. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, naishauri Serikali ifanye survey ya kutosha ili kuweza kubaini majengo yote ambayo mpaka sasa yameezekwa na asbestos na itoe tamko rasmi kwa wanaoyamiliki ili kuweza kuezuliwa na kuangamiza asbestos zote nchini ili tuendelee kuishi tukiwa na afya njema. Ma-technician wetu, wahandisi wetu, wanakwenda kufanya kazi katika mazingira ambayo asbestos bado zipo. Ni hatari sana kwa afya zao. Naomba sana Waziri na Serikali ichukuwe hatua muhimu kwa ajili ya jambo hili. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, jambo lingine, naomba kuishauri sana Wizara ya Mazingira katika suala zima la ukataji miti ovyo. Tutafute njia mbadala ya kutengeneza mkaa. Zipo research nyingi ambazo zinaonyesha tunaweza kutumia sold waste kutengeneza mkaa, kama briquette. Hizi sold waste zitakapoondolewa kwenye miji yetu, maana yake bado Sekta ya Mazingira inanufaika kwa miji yetu kuwa misafi na salama, lakini wakati huo huo tunapata energy mbadala ya kuzalisha moto badala ya kukata miti ovyo. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, pia umuhimu wa sisi kutengeneza mkaa kwa kutumia sold waste, itawapelekea wanaweke wetu wa vijijini waendelee kupika hali ya kuwa wako watanashati kwa sababu kuni zinawafanya wawe wachafu kutokana na moto. Kwa hiyo, naomba sana tufike wakati tutengeneze mkaa kutokana na takataka tunazozizalisha katika majumba yetu.

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

SPIKA: Ahsante sana.

MHE. ENG. MWANAISHA N. ULENGE Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Naunga mkono hoja. (Makofi)