Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira

Hon. Omar Ali Omar

Sex

Male

Party

ACT

Constituent

Wete

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira

MHE. OMAR ALI OMAR: Mheshimiwa Spika, nipo ahsante sana na mimi kunipa fursa ya kuchangia katika Wizara hii nyeti kabisa ya Muungano. Kwanza niwapongeze wote Mheshimiwa Waziri na Naibu wako, na zaidi nakupongeza zaidi Mheshimiwa Chande kwasababu ni mwenzangu ananijua tunajuana. Tunapiga shamvi pamoja katika maeneo yetu. (Kicheko)

Mheshimiwa Spika, lakini zaidi nijikite kwenye Wizara hii inayohusiana na mambo ya Muungano kwenye sehemu zaidi ya Elimu ya juu. Kama tunavyojua kwamba Wizara hii ni Wizara nyeti sana katika kujenga mustakabali wa Taifa letu. Kwa bahati nzuri ni mwalimu ninapotokea miaka 22 nimefundisha, na nimeona matokeo mengi ambayo tunapokuja kufanya kazi inayohusiana na mambo ya Muungano zaidi katika Wizara yetu ya Muungano kwenye Sekta ya Elimu kuna vitu ambavyo kidogo vinaleta ukanganyifu kwa sababu ni Wizara ya Muungano.

Mheshimiwa Spika, maombi yangu, zaidi ni kwenye suala zima linalohusiana na watendaji, watendaji wanaotoka visiwani kuja kwa wenzetu huku bara, kuja kufanya shughuli nzima inayohusiana na shughuli za Muungano zaidi kwenye sekta hii inayohusiana na Elimu ambayo pia ni Wizara ya Muungano. Kwa kweli kwa upeo wangu nimeona kwamba mahusiano yetu yanakuja katika sekta nyingi sana zinazohusiana na Muungano. Nikiangalia katika sekta hii zaidi kwenye suala la upatikanaji wa syllabus ambazo tunakuwa tunakwenda nazo kule visiwani na bara kwa ujumla. Tukiangalia kwenye syllabus zetu tunatakiwa tuwe na ulinganifu.

Mheshimiwa Spika, ulinganifu wetu unatakiwa kwenye syllabus ziwe zinalingana tokea from standard one au darasa la kwanza mpaka darasa la saba alafu tuje tuangalie curriculum yetu iendane sambamba na curriculum ile iliyopo bara ambayo ni ya kuanzia form one mpaka kufika madarasa ya juu zaidi form six.

Sasa hii ina ukanganifu mkubwa ukiangalia kwamba matokeo yanapotolewa wanafunzi wetu wengi wanakuwa wanafeli na wanafeli kwasababu mtaala unaotumika Zanzibar na Mtaala unaotumika huku Tanzania Bara unakuwa ni tofauti. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, hii ni kuonyesha kwamba wanafunzi wetu wanaonekana kwamba siku zote wanashika nafasi ya mwisho zaidi Zanzibar, unasikia nafasi zile kumi za mwisho zinatoka Zanzibar, hii ni kwasababu kwamba sio kwamba wanafunzi hawana uwezo lakini wanauwezo mkubwa bali mitaala haiendi sambamba kwasababu kitengo kile kinachohusiana na elimu ya juu hakihusiana zaidi na kule Tanzania visiwani.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, hili naomba sasa liangaliwe kwa kina kabisa ili kwamba mitaala yetu iende sambamba, kinachofanyika Tanzania visiwani from standard one hadi standard seven na sawasawa kiendane na bara na visiwani viwe ni vitu vinalingana, huo ndio mchango wangu siku ya leo kwenye suala zima la Muungano. (Makofi)