Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Ofisi ya Waziri Mkuu

Hon. Omari Mohamed Kigua

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilindi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Ofisi ya Waziri Mkuu

MHE. OMARI M. KIGUA: Mheshimiwa Spika, ahsante. Kwanza nakushukuru sana kwa kunipa nafasi hii nami niweze kusema neno kwenye Hotuba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu juu ya bajeti yake.

Pia nampongeza Waziri Mkuu, Mheshimiwa Jenista Mhagama na Manaibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu kwa sababu wamekuwa wakifanya kazi nzuri sana kwa ajili ya maendeleo ya nchi yetu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nina mambo machache. Katika maendeleo duniani kote, tafiti na maendeleo ni kitu muhimu sana, kwa maana ya research and development. Waheshimiwa Wabunge wengi wamesimama hapa wakizungumzia kwamba, nchi yetu inaelekea kwenye maendeleo na sehemu ambayo Watanzania walio wengi wapo kwenye kilimo. Kwa hiyo, nilikuwa namwomba Mheshimiwa Waziri Mkuu kupitia Wizara ya Kilimo tuwekeze fedha nyingi sana kwenye Sekta ya Kilimo kwa sababu ndio Watanzania wengi wanaitegemea. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, suala la amani na migogoro katika nchi yetu limetapaa kila sehemu. Nami nampongeza sana Mheshimiwa Waziri Mkuu, amekuwa akisimamia maeneo haya kwa weledi wa hali ya juu sana. Mwaka 2017 Mheshimiwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania alifanya ziara kwenye mpaka wa Jimbo letu la Kilindi na Wilaya ya Kiteto. Nampongeza sana Mheshimiwa Waziri Mkuu kwa sababu alitumia saa nane kwa ajili ya kutatua mgogoro baina ya wilaya hizi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, mgogoro huu umechukua miaka takribani 30 na wananchi wamekuwa hawafanyi shughuli za maendeleo kwa sababu ya migogoro ambayo kwa kweli haiishi. Nakumbuka Mheshimiwa Waziri Mkuu alitoa maelekezo, watalaam wakaja wakapitia mpaka ule, kilichobaki ni kuweka alama.

Mheshimiwa Waziri Mkuu wananchi wa maeneo haya, mpaka huu ambao unajumuisha Kata nane wananchi hawafanyi shughuli za kilimo, hawafanyi shughuli za maendeleo; na wapo Wakuu wa Wilaya na Wakuu wa Mikoa, wanashindwa kusimamia kwamba agizo lako la kuweka alama bado halijatekelezwa.

Mheshimiwa Spika, namwomba Mheshimiwa Waziri Mkuu wakati ana-wind-up asiseme neno lolote na atoe maelekezo kwa Wakuu wa Mikoa; Mkoa wa Tanga na Manyara; na Wakuu wa Wilaya wa Kilindi na Kiteto wahakikishe kwamba wananchi wanafanya shughuli zao kwa usalama na amani. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, mgogoro huu umechukua miaka takriban 30 na wananchi wamekuwa hawafanyi shughuli za maendeleo kwa sababu ya migogoro ambayo haiishi. Nakumbuka Mheshimiwa Waziri Mkuu alitoa maelekezo wataalam wakaja, wakapitia mpaka ule kilichobaki ni kuweka alama. Wananchi wa maeneo haya katika mpaka huu ambao unajumuisha kata nane, wananchi hawafanyi shughuli za kilimo wala shughuli za maendeleo na wapo Wakuu Wilaya, Wakuu wa Mikoa wanashindwa kusimamia na kwamba agizo lako la kuweka alama bado halijatekelezwa. Namwomba Mheshimiwa Waziri Mkuu wakati ana wind-up aseme neno lolote na atoe maelekezo kwa Wakuu wa Mikoa, Mkoa wa Tanga na Manyara na Wakuu wa Wilaya ya Kilindi na Kiteto wahakikishe kwamba wananchi wanafanya shughuli zao kwa salama na amani. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, la pili, naomba nizungumzie suala la barabara ya kuanzia Handeni - Kibirashi - Kiteto hadi Singida ambapo ndipo bomba la mafuta litokalo Hoima Uganda litakwenda hadi Tanga. Sasa nafahamu fika na ndio ukweli kwamba barabara hii itakuwa na shughuli nyingi kutokana na ujenzi wa bomba la mafuta, lakini barabara hii haijajengwa kwa kiwango cha lami. Naomba sana eneo au kipande kilichobaki ni cha kilometa 460 tu kuanzia Singida - Manyara hadi Handeni, kuna umuhimu barabara hii ikajengwa kwa haraka sana ili wakati wa ujenzi wa bomba la mafuta wenzetu ambao wameamua ku-invest fedha nyingi sana, wasipate usumbufu wakati wa ujenzi huo.

Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana. (Makofi)