Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mpango wa Tatu wa Maendeleo wa Taifa kwa Kipindi cha Miaka Mitano kuanzia mwaka 2021/2022 – 2025/2026

Hon. Rose Cyprian Tweve

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Mpango wa Tatu wa Maendeleo wa Taifa kwa Kipindi cha Miaka Mitano kuanzia mwaka 2021/2022 – 2025/2026

MHE. ROSE C. TWEVE: Mheshimiwa Spika, nikushukuru sana kwa kunipa nafasi. Nianze kwa kumshukuru na kumpongeza kaka yangu Mheshimiwa Waziri wa Fedha, Mheshimiwa Dkt. Mwigulu kwa namna ambavyo ameandaa na kuwasilisha huu mpango hapa Bungeni, ili na sisi tuweze kutoa mapendekezo yetu.

Mheshimiwa Spika, nitajikita kwenye vipaumbele vitano ambavyo Mheshimiwa Waziri alivielekeza hapa Bungeni kuwa ambavyo, ndivyo vitakavyotusaidia kuhakikisha sisi kama Watanzania tutakuwa na uchumi endelevu na shindani na tutoke sasa kwenye hii asilimia sita tuweze kufika kwenye asilimia nane. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, na nita-zero in kwenye kile kipaumbele namba tano ambacho umehakikisha kama Taifa tutahakikisha tunaendeleza hii rasilimali watu. Na issue hapa Mheshimiwa Waziri wa Fedha umeeleza kuwa unataka kufanya maboresho kwenye sekta ya elimu. Mheshimiwa Waziri maboresho peke yake hayawezi kutusaidia sisi kufikia yale malengo yetu, we need total transformation kwenye sekta ya elimu, tunahitaji mapinduzi makubwa hapa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, katika nchi zilizobarikiwa Tanzania is one of them. Tuna natural resources za kutosha, tuna ardhi ya kutosha na hii rasilimali watu ambayo Mheshimiwa Waziri wa Fedha anaiongelea ndipo hapa kwenye changamoto. Tuna vijana ambao zaidi ya asilimia 65 wangetumika kama nguvukazi ya kuja kuboresha uchumi wetu. Hapa ndipo tunapotaka kuanza. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, hata nchi za wenzetu ambazo zimepiga hatua, let say China, wao tayari wapo juu, lakini na wao wameamua kufanya total transformation kwenye mfumo wao wa elimu kuhakikisha vyuo hivi vikuu wamebadilisha vyuo vikuu 600, ili vije kuwa vyuo vya kati; vyuo vya ufundi kuhakikisha wanazalisha vijana ambao wana skills za kuajiriwa kwenye viwanda vyao na pia thinking. Wana critical thinking ya kuhakikisha wanatumia mazingira ya kujianzishia biashara na kufanya shughuli zao. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, twende Singapore. Wao kuanzia mwaka 1997 mpaka 2012…

SPIKA: Waheshimiwa Wabunge nawaombeni sana, hata ninyi wenyewe mkikaa mnaona masikio yenu jinsi yanavyokataa hizi kelele ambazo mnapiga. Na hizi five minutes ambazo kila Mbunge anaongea hapa ni very critical ni vizuri ukasikiliza argument ya mtu anasema nini. Mkitaka kuongea mnakwenda canteen pale mnapiga na kahawa kidogo, mnapiga story zenu zote mnamaliza. Tupeane nafasi tusikilize watu wanaongea kitu gani, kuna hoja muhimu sana zinazoongelewa humu ndani.

Endelea Mheshimiwa Rose Tweve!

MHE. ROSE C. TWEVE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru, nilikuwa natoa mfano wa Singapore wenzetu kwa miaka 15 walihakikisha wanabadilisha mfumo wao wa elimu wakajikita focus yao ikawa kwenye skill development na kuhakikisha watoto na vijana wao mashuleni wana uwezo wa kufikiri, critical thinking. Sasa sisi hapa Tanzania it is opposite, tuna human resources, tuna ardhi, tuna natural resources, lakini mfumo wetu wa elimu, tume-focus sasa kwenye vyuo vikuu kuzalisha degree ambapo mmekuja kutueleza hapa hazina tija hata kwenye soko letu la ajira. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, Mheshimiwa Waziri wa Fedha ndipo hapa ningeomba kama Taifa tufanye total transformation. Mdogo wangu pale Viti Maalum kutoka Mwanza alisema tuwe na agenda za kitaifa; hii ndio iwe agenda yetu sasa kuhakikisha hawa vijana wetu wanaweza kuwa na uwezo wa kufikiri na kuwa na skills za kuweza kuajiriwa. Tuhakikishe hivi vyuo vya kati ndio vinapewa msukumo na vyuo vya ufundi. Sasa hivi funding zote zinakwenda kwenye elimu ya juu, hii ndio iwe think tank yetu, moja tutakuwa na vijana ambao wanajitambua, tutaongeza wigo wa walilipa kodi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, sasa hivi as of today number ya walipa kodi ni 3,985,493 out of 60 million people. Hata tukisema tutoe hao wazee na vijana bado tungekuwa na milioni 23 ya Watanzania ambao wangekuja kuongeza pato la Taifa. Hata tuweke mazingira mazuri kiasi gani kwa hawa watu less than four million hatuwezi kufikia malengo yetu ya kuhakikisha tunakuwa na uchumi endelevu na shirikishi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Waziri nakuomba tuhakikishe sasa hata hivi viwanda tunavyoajiri tukiweka msukumo huku kwenye mfumo wetu wa elimu hata hawa investors wanaokuja watakuwa attracted kuja Tanzania kwasababu watakuwa na guarantee na vijana ambao wapo much skilled. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, hata hizi nchi zinazokwenda ku- invest China kama Marekani wanakwenda kule sio kwasababu kuna cheap labor, wanakwenda kule kwasababu wana vijana ambao wako much skilled. Anaweza akafanya na akawa mchango kuhakikisha wanaendeleza viwanda vilivyopo. Kwa hiyo, Mheshimiwa Waziri hapa ndipo tunapotakiwa kuanza. This is a piece of the puzzle ambayo ina-miss kwenye mfumo wetu wa elimu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, baada ya kusema hayo nimtakie heri Mheshimiwa Waziri katika utekelezaji wa majukumu yake natuhakikishe tunaanza hapo. Nashukuru sana kwa kunipa nafasi. (Makofi)