Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Tatu wa Maendeleo wa Taifa kwa Miaka Mitano (2021/2022 – 2025/2026) na Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Mwaka 2021/2022 pamoja na Mapendekezo ya Muongozo wa Maandalizi ya Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka 2021/2022

Hon Ally Juma Makoa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kondoa Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

3

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Tatu wa Maendeleo wa Taifa kwa Miaka Mitano (2021/2022 – 2025/2026) na Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Mwaka 2021/2022 pamoja na Mapendekezo ya Muongozo wa Maandalizi ya Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka 2021/2022

MHE. ALI J. MAKOA: Mheshimiwa Mwenyekiti, awali ya yote, nimshukuru Mwenyezi Mungu, lakini pia nikushukuru wewe kwa kunipa nafasi ya kuchangia Mpango huu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini niishukuru Serikali ya Awamu ya Tano, chini ya Dokta John Joseph Pombe Magufuli, Mama Samia na Mheshimiwa Majaliwa Kassim Majaliwa. Pia nitoe shukrani kwa Mawaziri wa Awamu iliyopita kwa kazi kubwa waliyomsaidia Rais wa nchi katika kutekeleza shughuli mbalimbali katika nchi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na mambo mazuri yaliyofanyika awamu iliyopita, pia mimi mchango wangu katika mpango huu ni kama ifuatavyo, moja nitagusa sehemu ya kilimo. Kama tunataka tufikie malengo ya kilimo katika nchi yetu ni lazima kwanza mambo yafuatayo yafanyike. Moja, tuhakikishe ile migogoro mikubwa ya mashamba kati ya wananchi na taasisi za Serikali inamalizwa mapema ili kutoa nafasi kwa wananchi kuendelea kufanya kilimo. Iko migogoro kati ya wananchi na Jeshi la Magereza kuhusiana na mashamba na imechukua muda mrefu kiasi ambacho imekuwa ikisimamisha shughuli za kilimo kwa wananchi hasa maeneo ya Kingale kwa kule kwetu Kondoa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la pili tujikite katika mbegu. Soko la jana nilikwenda katika maduka ya mbegu, mfuko wa kilo mbili wa alizeti unauzwa kati ya Sh.15,000 mpaka Sh.16,000. Kwa hiyo, Mpango ungejiwekeza katika maeneo ya uandaaji wa mbegu ili kurahisisha upatikanaji wa mbegu kwa bei nafuu kwa wakulima wetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la tatu ni kuhusu viwanda. Tumekuwa na viwanda vingi sana katika nchi hii. Nimekuwa Mkoa wa Pwani, tumekuwa tukiuita Mkoa wa Viwanda kwa sababu viko viwanda ambavyo vinaonekana, ni kazi kubwa iliyofanyika katika Serikali hii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la nne, Mpango huu unatakiwa uendane sambamba na kuweka tahadhari ya kuilinda miundombinu pamoja na mali za wenye viwanda. Nimewahi kushuhudia kiwanda kinaungua moto mpaka kinamalizika hakuna zimamoto. Kwa hiyo, nashauri kwenye Mpango huu wakati tunaandaa mipango ya viwanda tujaribu na Wizara nyingine ziwe zinashirikiana katika kufanya ulinzi. Kiwanda cha Mafuta ya Alizeti Kondoa kiliungua mpaka kikamalizika hakuna zimamoto. Walipofanya juhudi ya kutafuta zimamoto Babati, Manyara, zimamoto linapatikana kiwanda kimeungua mpaka kimeisha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini pia wawekezaji wa mabasi, muda mfupi badaye basi la abiria pia likaungua mpaka linamalizika, hakuna zimamoto. Kwa hiyo, tunaomba katika Mpango huu pia, Wizara ya Ulinzi iangalie maeneo yale ambayo yanakosa zimamoto yatufanyie mpango wa kupata zimamoto.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la tano, Mpango huu tunaomba uimarishe uwajibikaji, uadilifu na uaminifu katika sekta zote ambazo watu wamepewa majukumu ya kumsaidia Mheshimiwa Rais ikiwepo kwenye eneo la TRA. Bado kuna mianya mingi sana ya kodi kupotea na yako maeneo mengi kabisa kodi hazilipwi. Kwa hiyo, Mpango huu uendelee kuweka mkakati kwa ajili ya kuhakikisha kodi ya Serikali inaingia hasa kwa kutumia zaidi TEHAMA katika ukusanyaji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana. (Makofi)