Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hotuba ya Mheshimiwa Rais, Dkt. John Pombe Joseph Magufuli aliyoitoa wakati wa Ufunguzi wa Bunge la Kumi na Mbili, Tarehe 13 Novemba, 2020

Hon. Francis Kumba Ndulane

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilwa Kaskazini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Hotuba ya Mheshimiwa Rais, Dkt. John Pombe Joseph Magufuli aliyoitoa wakati wa Ufunguzi wa Bunge la Kumi na Mbili, Tarehe 13 Novemba, 2020

MHE. FRANCIS K. NDULANE: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuzungumza ndani ya Bunge lako Tukufu. Kwanza, napenda kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kuniwezesha kuwa mmoja wa wajumbe wa Bunge hili tukufu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, pili, napenda niwashukuru wapiga kura wa Jimbo langu la Kilwa Kaskazini kwa kuniwezesha kuwepo ndani ya Bunge hili kwa kunipa kura nyingi wakati wa Uchaguzi Mkuu uliopita. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujikita kwenye maeneo matatu katika Hotuba ya Mheshimiwa Rais iliyosomwa wakati wa ufunguzi wa Bunge letu hili la Kumi na Mbili. Maeneo hayo ni sekta ya utalii, sekta ya afya na michezo.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika eneo hili la michezo, kwa kuwa halijazungumzwa na Mbunge yeyote ndani ya Bunge lako hili, napenda unipe upendeleo angalau wa dakika mbili za nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika ukurasa wa 23 - 25 sekta ya utalii imefanunuliwa vizuri na kwa hakika kuna malengo mengi mazuri yametolewa.

Napenda niseme tu kwamba katika Wilaya yangu ya Kilwa kuna vivutio vingi vya utalii kama magofu Kilwa Kisiwani; kumbukumbu nyingi za kale kule Songo Mnara; mapango makubwa na madogo katika Wilaya yetu ya Kilwa; mabwawa yenye viboko wengi wenye tabia tofauti na maeneo mengine katika Bwawa la Maliwe katika Kijiji cha Ngeya kule Mitole na pia Mto Nyange kule Makangaga; Kumbukumbu za Vita vya Majimaji katika Kata ya Kipatimu, Tarafa ya Kipatimu, Kijiji cha Nandete; na pango kubwa ambalo linasadikiwa kuwa ni la pili kwa ukubwa Barani Afrika linalojulikana kwa jina la Nang’oma lililopo katika Kijiji cha Nandembo. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo naiomba Wizara yetu tushirikiane kuhakikisha kwamba tunavitangaza vizuri vile vivutio ili kuongeza vivutio vya utalii katika nchi yetu ambavyo vitatuhakikishia mapato mengi kwa ajili ya Serikali yetu. Yale mapango ya Nang’oma ni mapango yana historia kubwa na watafiti wengi kutoka nchi mbalimbali kama Italia, Ujerumani na Uingereza wamekuwa wakija mara kwa mara, lakini kuna changamoto kubwa katika hivyo vivutio nilivyovitaja kwenye suala la miundombinu ya usafiri.

Mheshimiwa Naibu Spika, barabara haziko katika hali nzuri, kwa mfano ukitaka kufika kule ambako vita vya majimaji vilianzia Nandete au kule kwenye pango la Nang’oma ambako inasadikiwa kwamba wakati wa vita vya majimaji akinamama na watoto walikwenda kujificha kule wakati akinababa walipokuwa wanaendelea na vita vya majimaji. Ningeomba miundombinu iboreshwe kwa barabara ya kutoka Tingi pale Kijiji cha Njia Nne kwenda Kipatimu lakini vile vile barabara ya Nangurukuru – Liwale ambayo ipo katika Ilani ya Uchaguzi ya CCM basi ifanyiwe taratibu za haraka ili kuweza kuhakikisha kwamba inaboreshwa na vile vile barabara inayokwenda Makangaga – Nanjilinji.

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana na naomba kuunga mkono hoja. (Makofi)