Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hotuba ya Mheshimiwa Rais, Dkt. John Pombe Joseph Magufuli aliyoitoa wakati wa Ufunguzi wa Bunge la Kumi na Mbili, Tarehe 13 Novemba, 2020

Hon. Maimuna Ahmad Pathan

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Hotuba ya Mheshimiwa Rais, Dkt. John Pombe Joseph Magufuli aliyoitoa wakati wa Ufunguzi wa Bunge la Kumi na Mbili, Tarehe 13 Novemba, 2020

MHE. MAIMUNA A. PATHAN: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza, namshukuru Mwenyezi Mungu kwa kuniwezesha siku ya leo kwa kunipia pumzi ya uhai na pia kupata nafasi hii ya Ubunge. Pia nawashukuru akina mama wa Mkoa wa Lindi kwa kuniamini na kunipa nafasi hii ya Ubunge ili niweze kuwatumikia miaka hii mitano. Vilevile nakishukuru chama change, Chama cha Mapinduzi na shukrani za pekee pia ziende kwa Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli kwa kuwa alitekeleza vizuri Ilani ya chama chetu kuanzia mwaka 2015 mpaka 2020 jambo lililotopelekea kutubeba Wabunge wengi wa CCM kuingia humu ndani. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kuchangia sana kwenye suala la maji. Ukurasa wa 34 Mheshimiwa Rais alisema kwamba atalipa kipaumbele sana suala la maji na pia alisema sehemu nyingi alipokuwa anazunguka kwenye kampeni wananchi wengi sana walikuwa wanalalamika kuhusu maji hasa maeneo ya vijijini. Kwa kweli tunamshukuru sana Rais wetu Dkt. John Pombe Magufuli, amejitahidi sana kutekeleza suala la maji katika maeneo mengi. Kwa Mkoa wangu wa Lindi tunamshukuru sana ametusaidia akina mama kututua ndoo kwa asilimia kubwa sana. Sehemu zilizobakia na changamoto ya maji ni chache sana. Tunaomba Waziri wa Maji na viongozi wengine mnaohusika na suala hilo la maji mjitahidi sehemu zile chache ambazo zimebakia ili nao wanachi wa vijijini waweze kupata maji safi na salama.

Mheshimiwa Naibu Spika, sehemu nyingine ambayo napenda kuchangia ni huduma ya afya. Tunashukuru sana Serikali yetu ya Chama cha Mapinduzi imejitahidi sana kuboresha huduma ya mama na motto. Kwa kweli imejitahidi sana ukiangalia kwenye Wilaya ya Nachingwea wamefanya maboresho kwenye jengo la akina mama na watoto, wodi ya wazazi imekuwa nzuri na inahuduma nzuri sana.

Mheshimiwa Naibu Spika, suala lingine ambao napenda kuchangia ni kilimo, ukurasa wa 19. Pia nako kwenye suala la kilimo Rais wetu mpendwa amejitahidi sana kutekeleza Ilani hiyo ila kuna changamoto chache tu ambazo tunaomba na zenyewe zitiliwe mkazo ili wananchi wafaidike na Serilikali yao ya Chama cha Mapinduzi.

Mheshimiwa Naibu Spika, wananchi wa Lindi wanalima sana mbaazi, lakini bahati mbaya kidogo mwaka huu na mwaka jana bei ya mbaazi imeshuka sana na Akinamama wengi wameanzisha vikundi, wameungana na biashara yao kubwa ni kulima mbaazi kwa ajili ya biashara.

Tukifuata kwenye ukurasa wa 19, Mheshimiwa Rais amesema tufanye kilimo kiwe biashara, na akinamama wale walijitahidi sana kulima mbaazi lakini bahati mbaya soko kidogo limeshuka. Ninachoomba, Mawaziri husika wajitahidi kutafutia akinamama wa Mkoa wa Lindi masoko ya mbaazi ili na sisi tuinuke katika maisha yetu.

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana na naomba kuunga mkono hoja. (Makofi)