Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2018 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

Hon. Dr. John Danielson Pallangyo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Arumeru-Mashariki

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2018 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

MHE. JOHN D. PALLANGYO: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi nami nichangie kidogo kwenye hii hoja iliyoko mezani. Nitangulie kwanza kumshukuru Mungu, Baba yetu wa Mbinguni ambaye ndiye ametuamsha salama na kutukutanisha hapa.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nianze kumpongeza Waziri wa Fedha na Mipango, Mheshimiwa Dkt. Mpango. Mheshimiwa Waziri nakupongeza sana pamoja na Naibu wako na Katibu Mkuu na Watendaji wote wa Wizara hii kwa kazi nzuri ambayo mmekuwa mnafanya, pia kwa bajeti nzuri ambayo mmetuleta ambayo naweza nikai-brand kwamba ni reconciliatory budget. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, bajeti hii imegusa mioyo ya wananchi wengi ambayo ilikuwa imeinama kwa kukumbana na kero nyingi katika kufanya shughuli zao kwa kuondoa tozo 54 na kuweka checks and balances kwenye kodi, kwa kweli bajeti ni nzuri na inastahili kuungwa mkono hundred percent. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, pia ukiona Wizara inafanya vizuri, ina mila ya utendaji wa mamlaka iliyoko juu. Kwa maana hiyo, nasema nampongeza sana Rais wetu, Mheshimiwa Dkt. John Joseph Pombe Magufuli ambaye amekuwa ni msukumo mkubwa kwenye utekelezaji wa mradi na mambo mengi mazuri ambayo yanaendelea hapa nchini. Amekuwa anatekeleza Ilani ya Uchaguzi kwa umahiri mkubwa, amekuwa anasukuma utekelezaji wa miradi mikubwa ambayo mwisho siku itaacha historia kubwa sana hapa nchini kwetu; Stiegler’s Gorge, SGR na ununuzi wa ndege Air Tanzania. Haya mambo siyo madogo. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nilikuwa napata shida kidogo nilipokuwa nasikia Waheshimiwa wengine wanasema kwamba haya ni maendeleo ya vitu badala ya watu. Nikajiuliza, hivi mtu ukijenga nyumba yako nzuri utasema ni maendeleo ya nyumba au ya nani? Nadhani kuna haja ya kujitathmini kidogo kwenye haya mambo kabla hatujasema. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, niseme kidogo juu ya kilimo. Kilimo bado ni mwajiri mkubwa kwa Watanzania, lakini mpaka sasa sidhani kama tumeweka nguvu ya kutosha. Tumekuwa tunategemea hali ya hewa na hali ya hewa inabadilika mara kwa mara. Matunda yake, wananchi wetu wanalima, wanapata mavuno kidogo. Basi niseme kwamba wakati umefika sasa hivi wa kuweka programu nyingine.

Mheshimiwa Naibu Spika, Programu ya mwisho kufanyika ilikuwa ni pragramu ya Kilimo Kwanza. Nadhani wakati umefika sasa wa kuanza pragramu ya Irrigation Kwanza, Kilimo cha Umwagiliaji, tuache kutazama mawingu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na mambo mengine Ilani ya Uchuguzi ya mwaka 2015 ililenga katika kukuza soko la ajira. Katika hilo ilikuwa ni kulinda taasisi zetu. Wizara hii ya fedha ina taasisi nyingi. Nilikuwa napitia makabrasha hapa nikakuta taasisi ya mamlaka ya bima (TIRA). Kazi yake hii ni kukuza soko la bima na kulinda migongano ndani ya walengwa na ndani ya wadau. Nimeshuhudia siku za karibuni na taasisi hii players wake ni mashirika ya bima, brockers, loss adjusters na mawakala.

Mheshimiwa Naibu Spika, hivi karibu nimeona kwamba hii taasisi, TIRA wanatoa leseni za u-brocker kwa mabeki. Hii nikaona kama siyo sawa, kwa sababu mabenki watafuta ma-bocker. Mabenki hawawezi wakashauri wateja kwamba ni bima ya namna gani ambayo inatakiwa ichukuliwe. Kwa ajili hiyo, namwomba Mheshimiwa Waziri regulations ziangaliwe ili benki ziwe restricted wasipewe u- brocker, waishie kwenye u-agent tu.

Mheshimiwa Naibu Spika, kabla sijamaliza, naomba, kuna somo ndani ya Biblia linamhusu mtoto mpotevu, aliomba haki yake kwa baba yake akapewa akaondoka, akaenda kuzurura mjini, akatumia ile haki yake akamaliza akafilisika, akapata shida, mwisho akaanza kushiriki chakula na nguruwe, akaamua kurudi kwa baba yake kwenda kuomba msamaha; na siku amefika alipokelewa na baba yake vizuri akachinjiwa kondoo na ng’ombe mnono sana akafanyiwa sherehe kubwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, Jimbo langu kule Arumeru Mashariki kwa muda mrefu sana barabara zake hazijatengenezwa, hazipati matengenezo stahiki na ya wakati. Kwa hiyo, matokeo yake ni kwamba yake sasa hivi hazipitiki. Naomba unipe ruhusa nimwombe Waziri wa Fedha aangalie namna atakavyomwezesha Waziri wa Ujenzi na TAMISEMI ili ifanyike pragramu ya barabara, opesheni barabara kule Arumeru Mashariki barabara zile zibadilike.

Mheshimiwa Naibu Spika, wananchi wanajisikia vibaya wakitoka pale Kibaoni King’ori wakifika Bomang’ombe kuna barabara lami inakwenda milimani, wakifika kwa Sadala kuna barabara ya lami, inakwenda milimani; wakifika Machame kuna barabara ya lami inakwenda milimani; wakija Kibosho kuna barabara ya lami inakwenda milimani; pale Meru hakuna barabara ya lami. Mheshimiwa Mpango nakuomba, nakusihi lile Jimbo sasa hivi ni Jimbo mkakati. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nimeomba kibali unipe nizungumzie hilo kwa sababu nimetoka kwenye lile Jimbo na ninajua hali yake ilivyo.

Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya hayo machache, naomba kuunga hoja mkono kwa percent mia moja. Ahsante sana. (Makofi)