Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2018 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

Hon. Ally Abdulla Ally Saleh

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Malindi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2018 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

MHE. ALLY SALEH ALLY: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, mimi leo nitajikita katika mfungamanisho wa uchumi wa Tanzania (Tanzania na Zanzibar) na Inshallah tutaelewana, leo nitakuwa mtaratibu sana katika kujieleza. (Kicheko)

Mheshimiwa Naibu Spika, naanza kwa misingi minne, kwamba tatizo la Muungano ninavyoona mimi hasa ni uchumi mwanzo, siasa na madara yanakuja baadaye. Msingi wa pili kwamba fiscal and monitory policy za Tanzania au za Bara zina direct impact za Zanzibar bila ya Zanzibar kuwa na nafasi ya kujitetea au kupata afua yoyote. Tatu, kwamba Zanzibar imekuwa ikipunjwa katika Muungano na nne kwamba Serikali ya Muungano haifanyi afua yoyote Zanzibar. Haina investments, haifanyi capital investments, haifanyi fidia wala haina afua aina yoyote, imeicha Zanzibar kama ilivyo lakini bado chumi hizi zinaambiwa zimeungana.

Mheshimiwa Naibu Spika, hivi sasa Tanzania Bara inakula mikono miwili, inakula mkono wa michango au kodi ambazo au uwekezaji ambao unafanywa kwa upande wa Tanzania Bara peke yake kwa sababu Tanzania Bara kuna Tanganyika na upande wa pili ni ule ambao Serikali ya Muungano inatumia fedha ambazo zinazalishwa na taasisi za Muungano ambazo Zanzibar nayo ina sehemu yake na ndiyo hapo Zanzibar inapopunjwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, nikizungumzia taasisi hizo, zenu za ndani ziacheni, TIB, sijui kitu gani, taasisi zenu zote za ndani. Mimi nazungumzia za Muungano, TTCL, ATCL, Bima na vingine vingi kama hivyo, TCRA na nyingine kama hizo. Sasa hizi ndiyo ambazo sisi Wazanzibar tunasema kwamba tunapunjwa kwayo, maana yake zile ni zetu sote, lakini hazitumiki kama zinavyotarajiwa na nitaelezea. Hii inatokana kwamba tumepuuza msingi wa Muungano ambao tumeutengeneza kwamba tuna nchi mbili, Taifa moja na kwamba tuna chumi mbili ndani ya nchi moja. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, tulikubaliana kwamba kwa mujibu wa Katiba kifungu cha 133 na 134 tutengeneze akauti ya pamoja na tume ya pamoja ya fedha. Sitaki kwenda kwenye historia kwamba muda mrefu hizi hazifanyiwa kazi, kusema kweli inasikitisha kwamba Marais ambao tangu limeamuliwa hilo, Mawaziri ambao tangu limeamuliwa hilo, Mawaziri Wakuu tangu limeamuliwa hili, Maspika tangu limeamuliwa hilo, Wabunge tangu limeamuliwa hilo tumeipuuza Katiba yetu. Kuwepo kwa taasisi hizo mbili za Muungano lakini kwa miaka yote sitaki kutaja miaka mingapi maana yake ni aibu kwamba nchi hii inaweza kupuuza Katiba kwa miaka yote hiyo na ndiyo maana tumefika hapa tulipofika. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, hali kadhalika taasisi nyingine ambayo imepuuza Kikatiba ni kuwa na Mahakama ya Katiba ambayo pengine Zanzibar ingeweza kwenda kushtaki kama inaona inaonewa, lakini baadaye tumekwenda kup-opt na kuwa Kamati ya Kero za Muungano ambayo kusema kweli ni nje ya Katiba na hata isingestahili kuwepo. Nimesema hapa kwamba tunazungumzia juu ya taasisi za Muungano ambazo mapato yake yanapaswa yagaiwe sawasawa, kwa bahati nilikuwepo katika Tume ya Warioba.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika Tume ya Warioba tuliarifiwa, kwa sababu tulikuja mahali ule Muungano wa Serikali tatu tungeutengeneza vipi. Tukaarifiwa kwamba kwa mfumo wa Tanzania kama kungekuwa matumizi ya taasisi za Muungano kutumika kwa Muungano, basi zile fedha za kuanzisha Serikali ya tatu zingepatikana, zingepatikana fedha kwa Zanzibar na zingepatikana fedha kwa Tanganyika. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, wanaopinga Serikali tatu wapinge kwa mengine lakini wasipinge kwa kiuchumi, kwa sababu kiuchumi fedha tulizonazo zinatosha kufanya hivyo. Taasisi za Muungano zinawezakumudu kuwa na Serikali tatu.

Kwa hiyo Tume ya Warioba tuliambiwa kwamba iliundwa, ilipewa kazi (Pricewaterhousecoopers) ambao wao walihakikisha kwamba hilo linawezekana. Sasa kwa mnajili wa mgawanyo huo wa taasisi za Muungano mapato yanayokusanywa Zanzibar ni 2%, mapato yanayokusanywa Tanzania Bara ni 98%, lakini hizi zinatiwa katika kapu moja kwamba zote ni za Muungano. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, jana ACT walitoa mchanganuo ambao pengine unaweza ukabishiwa, lakini tumepata mahali pa kuanzia. Wanasema 68% ya fedha ambazo ni za Muungano zinatumiwa na Tanganyika; 32% ndiyo zinatumika kwenye taasisi za Muungano proper. Labda Wizara ya Mama Samia, Wizara gani, za Muungano tu, 68% zinatumika na Tanganyika peke yake. Kwa hiyo, tunasema kwamba kama ingekuwa nchi hii inaendeshwa sawasawa basi Zanzibar ilikuwa ipate mgao wake kutoka 68%. Hesabu zilizotolewa ambazo zinaweza zikabishaniwa lakini mwisho nita-propose kama zinabishaniwa, basi Bunge hili liunde Kamati ifanye njia yoyote ile ya kuhakikisha ukweli uko wapi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa miaka saba wamefanya utafiti ACT wanasema kwamba 2414 mpaka sasa hivi kwamba kama ingekuwa fedha zile zimegaiwa labda kwa mgao wa formula ya 4.5 ambazo ni fedha Zanzibar wanazipata kutoka mgao wake wa Benki Kuu au mgao wake wa 11% ambayo inatokana na mgawanyo wa mapato ya kibajeti kutoka nje, basi Zanzibar ingepaswa kwa formula ya 4.5, Zanzibar ingepaswa ilipwe trilioni 4.6 kwa Serikali ya Tanzania kwa Zanzibar. Kama ikitumika formula ya mchango wa Zanzibar katika kuunda Benki Kuu yaani 11% basi Zanzibar inaidai Tanganyika hivi sasa 11.1 trillion shillings. Msitupe hizo, tupeni kile ambacho mnaona tutengeneze formula nyingine, lakini lazima tulipwe chetu, kwa sababu chetu kimo katika mashirika ya Muungano. Mimi sizungumzii 4.5 ambayo inatokana hivi sasa, sizungumzii fedha zile za kibajeti, nazungumzia haki yetu ambayo mashirika yale tumeyaunda pamoja na mengi yao yalitokana na Jumuiya ya Afrika Mashariki. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo katika hali kama hii ungetarajia kwamba option zipi za Zanzibar, viongozi wetu kama nilivyosema kwa upande wa Tanzania hawajaheshimu Katiba kwa muda wote, viongozi wa Zanzibar hawajaheshimu Katiba lakini pia hawawezi kusema hadharani kama tunaidai Serikali ya Tanzania, wataishia pembeni tu. Hata juzi baada ya bajeti hapa kuambiwa kwamba 18% imeondolewa ya VAT kwamba eti tulitarajiwa tusherehekee. Wakati kitu kile tangu mwanzo hakikuwa halali kufanywa, hakikuwa halali kabisa kufanywa na katika hali kama hiyo basi, mimi nafikiri kwamba kuna haja kama tunasema kwamba uchumi wa nchi hii unataka uende sambamba na haki itendeke, kwamba lazima tufike wakati Zanzibar apate haki yake bila ya tone, bila ya shilingi kupungua. Kwa sababu kama sivyo ni kwamba uchumi wa Zanzibar sasa unadidimia, Serikali ya Muungano haiwekezi Zanzibar, haitoi afua ya aina yoyote ile, lakini fedha zote zile za Muungano zinatumika kujenga Tanzania Bara. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, siku moja nilimsikia Dkt. Shein akisema surprisingly anasema ukienda Bara siku hizi utaona barabara zinajengwa, majengo yanajengwa, hamadi; nikasema kama yeye anasema hivyo nani mwingine wa kusema. Wakati yeye alipaswa aseme kwamba hizo fedha zilizojenga barabara na sisi zetu zimo, hizo fedha zinazojenga majengo na za Zanzibar zimo. Yeye anasema kwamba Bara kunaendelea zaidi, nani wa kusema hayo sasa kama yeye mkuu wa nchi hawezi kuyasema hayo. Kwa hivyo tunasema kwamba kama hamkutengeneza mazingira haya, Muungano utaendelea tu kama ulivyo lakini hatuna mapenzi nao. (Makofi)