Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Madini

Hon. Juma Othman Hija

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tumbatu

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Madini

MHE. JUMA OTHMAN HIJA: Mheshimiwa Spika, kwanza natoa shukrani zangu kwake kwa kunipatia fursa hii ya kutoa mchango wangu katika hotuba hii ya Wizara ya Madini.

Mheshimiwa Spika, pili, napenda kumpongeza sana Mheshimiwa Waziri kwa kuandika na hatimaye kuiwakilisha kwa ufasaha wa hali ya juu. Katika kuchangia hotuba hii napenda kuchangia katika maeneo yafuatayo:-

Mheshimiwa Spika, mchango wa Sekta ya Madini kwenye pato la Taifa; napenda kuipongeza Serikali pamoja na Wizara kwa kuweka mikakati mizuri katika Sekta ya Madini. Sekta hii ni miongoni mwa sekta muhimu sana katika Taifa letu.

Mheshimiwa Spika, ushauri wangu katika suala hili, ni kwamba Serikali iendelee kuweka mikakati ya kuimarisha sekta hii ili kuweza kuongeza pato la Taifa, ni vyema Wizara ikaweka wafanyakazi waaminifu katika sekta hii ambao watasimamia vyema mapato kwa uhakika na kwa uaminifu mkubwa. Mikakati hii iwe ya uhakika na kitaalam zaidi.

Mheshimiwa Spika, uendelezaji wa uchimbaji mdogo wa madini, naipongeza Wizara kwa kuendeleza jambo hili katika maeneo husika. Hii ni sehemu moja kubwa ambayo itaweza kuongeza ajira kwa wananchi wa maeneo husika na kuweza kupunguza umaskini.

Mheshimiwa Spika, ushauri wangu katika suala hili ni kwamba Wizara iendelee kuwasahihisha wananchi kwa kuwapa elimu na vitendea kazi vya kisasa ili waweze kumudu kazi zao na kuleta ufanisi zaidi. Aidha, Wizara iendelee kuwashirikisha wananchi wa maeneo husika kwenye sekta hii ili na wao wajihisi kama ni sehemu ya kuchochea maendeleo katika sekta hii. Wizara itakapowashirikisha kikamilifu wataweza kulinda na kuithamini sekta hii muhimu katika Taifa letu.

Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja.