Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Madini

Hon. Rose Kamili Sukum

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Madini

MHE. ROSE K. SUKUM: Mheshimiwa Mwenyekiti, ushauri kwa Mheshimiwa Waziri, moja; ufunguzi wa masoko ya madini katika maeneo imejikita zaidi kufanya uzinduzi huu katika kila mkoa ambao kuna uchimbaji wa madini. Uzinduzi huu wa masoko ya madini uendane sambamba na utaratibu mzuri wenye kukidhi vigezo vyote vya usalama katika maeneo yote yenye machimbo husika nchini. Kwani maeneo mengi hayana wasimamizi au watumishi wa madini na askari ili kulinda madini hayo kwa ajili ya wachimbaji wengi kutokuwa waaminifu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pili, utoaji wa elimu kwa wachimbaji mbalimbali juu ya umuhimu wa kutumia masoko ya madini yaliyopo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tatu, tozo za madini; watendaji wa mamlaka za kiserikali wanatoza kodi za tozo zilizofutwa. Inaaminika tozo hizi zote zinafanyika kwa maslahi binafsi ya wakusanya tozo hizo. Tozo hizo zinawalenga wachimbaji wadogo wadogo wa madini wenye uelewa mdogo wa sheria, kanuni na taratibu zilizowekwa na Wizara ya Madini pamoja na Tume ya Madini. Tozo mbalimbali zinazotozwa ni ushuru wa mawe, ushuru wa karasha, ushuru wa duara, ushuru wa mwalo na ushuru wa compressor. Tozo zinazotambulika na Serikali ni kama zifuatazo:-

Moja, royalty (mrabaha), ada ya ukaguzi (service and clearance) na service levy.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni wakati sasa Serikali kusimamia sheria zilizotungwa ili kuwanufaisha pande zote za Sekta hii ya Madini hasa wachimbaji wadogo wadogo kukatwa tozo/kodi kwenye viroba vya mchanga au mawe.