Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Madini

Hon. Mbaraka Kitwana Dau

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Madini

MHE. MBARAKA K. DAU: Mheshimiwa Spika, nianze kwa kukushukuru kwa fursa hii, sambamba na kumpongeza Mheshimiwa Waziri kwa wasilisho zuri asubuhi ya leo.

Mheshimiwa Spika, nichukue fursa hii pia kumpongeza Mheshimiwa Rais John Pombe Joseph Magufuli kwa uamuzi wake wa busara wa kujenga ukuta wa Mererani; na matunda ya kazi hiyo tumeanza kuyaona kwenye kitabu cha Mheshimiwa Waziri ukurasa wa 13 na 14. Kwa mujibu wa hotuba hii mapato yameongezeka kutoka milioni 71,861,970 mwaka 2016 mpaka kufikia shilingi 1,436,427,228. Haya ni mafanikio makubbwa sana na ya kuendelezwa ili taifa liendelee kunufaika na rasilimali zake.

Mheshimiwa Spika, kama hotuba ya Mheshimiwa ilivyoonyesha ukurasa wa 15 na 16 kuhusu mkakati wa kuongeza thamani ya madini yetu kwa kualika kampuni tisa zenye nia ya kujenga viwanda vya uongezaji wa thamani ya madini ni jambo jema. Niombe Wizara iharakishe mchakato huu wenye manufaa makubwa kwa nchi yetu.

Mheshimiwa Spika, Kuhusu Matumizi Holela ya Baruti za Kulipulia Miamba. Suala hili limekuwa ni kero kubwa kwa wananchi wanaoishi maeneo jirani na migodi mbalimbali nchini.

Mheshimiwa Spika, ni ukweli usio na shaka matumizi haya ya baruti yameleta madhara ya kiafya. Ushauri wangu ni kuwa wananchi wanaoishi jirani na machimbo haya walipwe fidia stahiki na wahame, wakaishi maeneo ya mbali na machimbo.

Mheshimiwa Spika, jambo linguine ni kwamba baruti hizi zimekuwa zikitumika nje ya matumizi ya migodi, hususan kwenye uvuvi haramu, jambo hili liangaliwe na udhibiti ufanyike.

Mheshimiwa Spika, nakushukuru na naunga mkono hoja.