Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Maliasili na Utalii

Hon. Anthony Calist Komu

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Moshi Vijijini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Maliasili na Utalii

MHE. ANTONY C. KOMU: Mheshimiwa Naibu Spika, nianze kwa kuwapa pole sana viongozi na watendaji wa Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kazi kubwa wanayofanya pamoja na changamoto za rasilimali kidogo. Naiomba Wizara hii muhimu kwa uchumi wetu ione umuhimu wa kutembelea Jimbo la Moshi Vijijini kwa ajili ya kutambua vivutio vya utalii katika Kata za Old Moshi Mashariki na Uru Mashariki (Materuni) ambapo kuna maanguko ya maji (water falls) ya ajabu sana.

Mheshimiwa Naibu Spika, vivutio hivi havijaweza kuwa vyanzo vya maana vya mapato kutokana na miundombinu ya barabara na vyoo kuwa mbaya sana. Nikilinganisha na vyanzo vya aina hiyo mahali pengine duniani naona kinachokosekana kwetu ni matangazo na kuboresha miundombinu tu.

Mheshimiwa Naibu Spika, aidha, niombe Wizara ikaone mti ulio katika Kata ya Mbokomu ambao ni mrefu kuliko yote Barani Afrika na wa sita duniani. Watu toka sehemu mbalimbali duniani toka ugundulike wamekuwa wakiutembelea, jambo ambalo linaweza kusababisha madhara kwa mazingira ya eneo hilo, hasa uoto wa asili ikiwa hapatakuwepo na utaratibu wa kuuendea mti huo na hifadhi yake. Mti huu unaweza kuwa chanzo cha mapato pia.