Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Mifugo na Uvuvi

Hon. Dr. Pudenciana Wilfred Kikwembe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Kavuu

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Mifugo na Uvuvi

MHE. DKT. PUDENCIANA W. KIKWEMBE: Mheshimiwa Spika, napenda kuchangia katika haya yafuatayo:-

Mheshimiwa Spika, Serikali ilipanga na imepanga kuendelea kujenga Mabwawa na malambo kwa ajili ya kunyweshea wanyama (Mifugo). Je, ni lini sasa mabwawa na malambo hayo yatajengwa katika Jimbo la Kavuu Halmashauri ya Mpimbwe Mkoa wa Katavi?

Mheshimiwa Spika, Serikali ina mpango gani wa kuhamisha ufugaji wa kuku wa kienyeji katika maeneo ya kijijini hasa katika maeneo ya vijijini kama maeneo ya Jimbo la Kavuu?

Mheshimiwa Spika, kupitia Wizara hii kwa kushirikiana na Wizara ya Maliasili na Wanyamapori iainishe mipaka kati ya hifadhi na matumizi ya mifugo.