Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Mifugo na Uvuvi

Hon. Emmanuel Papian John

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kiteto

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Mifugo na Uvuvi

MHE. EMMANUEL P. JOHN: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi. Kwanza naunga mkono hoja ili nisije nikasahau mwisho.

Mheshimiwa Spika, nipongeze Wizara na Waziri kwa bajeti nzuri ambayo wametuletea, lakini pia nipongeze na Kamati yangu kwa kazi kubwa ambayo tumeifanya inayoongozwa na Mwenyekiti wetu Mheshimiwa Mgimwa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lipo jambo moja ambalo naomba niseme, naipongeza Wizara kwa kazi moja ambayo wameifanya ya kupunguza migogoro ya wafugaji kwenye maeneo ya malisho, wamechukua maeneo makubwa kwenye ranchi za Taifa, wamekodishwa wafugaji, ng’ombe wamehamia mle kwa hiyo kero imepungua kwenye maeneo mengi; Kagera, Ruvu, Kalambo na mikoa mingine ambayo ina ranchi za Taifa ambazo wale wafugaji walikuwa wanazunguka na kuhangaika kwa ajili ya kutafuta malisho. Nawapongeza na nampongeza Mkurugenzi wa NARCO kwa ajili ya kuhakikisha kwamba hili jambo linafanyika na mifugo inapata maeneo ya malisho.

Mheshimiwa Spika, jambo la pili; niombe kuzungumzia suala la uvuvi haramu na stori nyingi ambazo zimeendelea kwa nchi nzima juu ya uvuvi haramu. Nikushukuru kwa sababu tulikwenda Mwanza kama Kamati, tukakutana na wadau wote; tulikutana na wadau wa viwanda, tukakutana na wavuvi wenyewe na wale madalali ambao wanauza samaki kwenye viwanda.

Mheshimiwa Spika, tulipokuwa kule Mwanza kila mtu tumempa dozi yake; Waziri amepata dozi juu ya watendaji wake ambao hawatimizi wajibu wao sawasawa, lakini na wale madalali tumewapa dozi yao kwa sababu wanafanya udalali kwa kupunguza bei ya wanaokwenda kununua samaki kwa wavuvi na ku-collude pamoja na wenye viwanda. Suala hili ni suala pana, lakini tunaamini sasa tunapokwenda kwa dozi tuliyoacha kule ndiyo maana unaona kidogo sasa hivi hakuna malalamiko kumetulia, isipokuwa yale madogo madogo tunaendelea kuyakamilisha. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, Kamati imefanya kazi kubwa, haya mambo mengi yatakwenda yanapungua pole pole na tutafika mahali ambapo tunaitendea Wizara hii haki. Tunalo tatizo kubwa, wavuvi hawasemi ukweli kwenye baadhi ya maeneo mengi na ndiyo maana kuna eneo la uharamu ambao unafanyika. Leo, tunapozungumza Wilaya ya Muleba kwa Mheshimiwa Mwijage pale, uvuvi kwenye vile Visiwa vyote vya Bumbire na wapi kote, leo wana-enjoy samaki wapo, wakienda ziwani wanarudi na samaki wa kutosha ambao wao wanaendelea ku-enjoy.

Mheshimiwa Spika, pia Halmashauri yetu ile ya Muleba nampongeza yule Mkurugenzi alikuwa anakusanya milioni nne kwa mwezi, leo anakusanya milioni 50. Kwa hiyo, Halmashauri inaendelea ku-grow, hiyo ni TAMISEMI ina-earn kutokana na effort za Wizara ya Mifugo. Haya yote twende tunayaona, ukizungumza na wale wavuvi wadogo wadogo wana-enjoy samaki wapo, wamekuwa wanavua kwa muda mfupi na wanapata samaki kuliko kushinda ziwani siku mbili, tatu.

Mheshimiwa Spika, wenye viwanda; wenye viwanda wanakwenda wana-determine price bila kushirikisha Serikali, wanashusha bei, wanadili na madalali wetu, wahuni, matapeli ambao siyo waajiriwa wa Wizara wala siyo watendaji wa Halmashauri. Wanashusha bei ya wavuvi, samaki wao wanawaingiza viwandani, wakishamaliza wale samaki wanawachakata, wakimaliza wanamwambia samaki wako bwana, hawa samaki hawako kwenye size na zile milimita zilizopangwa kwa hiyo ondoka na samaki wako, wameshawachakata mvuvi anapata hasara. Naomba hili suala sasa Wizara iliangalie kwa ukaribu sana na iweze kuona hayo.

Mheshimiwa Spika, Wizara imekuwa inabeba lawama nyingi hizi za uvuvi, lakini on the way mvuvi analeta samaki kwenye kiwanda, anakamatwa na watu wengine na watu wa ushuru ambao ni wa TAMISEMI, Polisi na watu wengine ambao ni Wizara tofauti kabisa na Wizara husika, wanapopigwa faini na kudaiwa ushuru huu mzigo unaenda unatupwa kwenye Wizara husika. Ushauri wangu juu ya hili, tunaomba hizi Wizara ziweze ku-interrupt zione solution ya pamoja juu ya kutatua huu mgogoro. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lipo jambo la mwisho kwenye uvuvi, tulitengeneza kanuni na sheria hapa juu ya uvuvi, tunaomba hizi sheria na kanuni kandamizi Mheshimiwa Waziri azilete hapa tuzifumue, tupange upya suala la utaratibu wa wavuvi uweze kukaa salama na nchi iweze kubaki salama tupunguze suala la lawama. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lipo suala la viwanda juu ya uzalishaji wa maziwa ya UHT, long life milk. Wameongeza kodi ya maziwa kwa ajili ya ku-reduce importation ya maziwa, lakini wakati huo tumepunguza hiyo, ilikuwa ni ku-promote viwanda vyetu vya ndani, kwa hiyo, viwanda vyetu vinavyozalisha kama Tanga Fresh na Asas wameshafunga mitambo ya UHT, sasa hivi wanajaribu ku-push kuona namna gani wanaweza kupanda wakitegemea wale wazalishaji wa maziwa wadogo, tukitegemea growth yao, Benki ya Kilimo na benki zote (commercial banks) zi-support hawa wakulima waweze ku-grow.

Mheshimiwa Spika, leo Waziri amekuja na suala la kupunguza tozo ya maziwa yanayokuwa imported ya unga, ukipunguza kilo moja ya maziwa ya unga yana-produce lita nane. Ukimpunguzia Azam leo, ukapunguza kwa level hii ya eighty something percent it means unakwenda kusababisha hivi viwanda vya Asas na Tanga Fresh vife asubuhi kwenye hii UHT. Wamekopa kwenye mabenki ya ndani, wana-promote wazalishaji wa maziwa wadogo which means unga unaendelea kuongezeka, maziwa ya unga yanaongezeka, una-import hiyo una impose unapunguza kodi, unasababisha watu wetu kufilisika. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, naomba nikueleze kwa hili na itatokea na utaiona, kwa hili Mheshimiwa Mpina akae chini atafute cash flow na projections za namna ya importation ya maziwa ku-protect viwanda vyetu vya ndani vya UHT kama programu ilivyokuwa. Hiyo ndiyo inayokwamisha Sekta ya Maziwa nchini kwa sababu investment ya maziwa, mradi kwenye plant ya UHT ni zaidi ya dola milioni nne au tano, sasa anapo-invest amekopa hapa, uka-import hayo ni kwamba hawezi kushindana kwenye soko, mwisho wa siku kinachotokea ni nini? Anaweza kuuza lita ya maziwa Sh.2,600, huyu mwingine ni lazima akiweka zile cost zote vyovyote vile inatozwa 18% lazima atatokea kwenye Sh.3,000. Mwisho wa siku, hakuna uwiano kwenye hili. Niombe Mheshimiwa Waziri aliangalie kwa haraka sana hili ili kuokoa na ku-allow ushindani wa ndani, tuwe kwenye balancing point, asiwepo bora na mwingine. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, niende kwenye suala lingine; kwangu kumeanzisha Hifadhi ya Olengapa, nyanda za malisho, lakini kumekuwa na migogoro mingi, watu wanalalamika. Nimefanya ziara, kipofu mmoja akanyoosha mkono anasema mimi shamba langu limekwenda, nilikuwa nalima, ni kipofu, sasa naenda kufa. Alipozungumza kwenye mkutano wenzake wakamwambia ale udongo. Mheshimiwa Waziri aje, tukae tuone hao watu wanaolalamika kwa nini Olengapi wamechukua eneo wasingeacha wale wakulima 300 na eneo lao, ime-incorporate lile eneo ikalichukua ikaacha hawa watu ikiwemo hao vipofu wanaolalamika kwamba wameambiwa na wenzao wakale udongo. Niombe kwamba sasa hilo suala Waziri atakapokuja, basi atusaidie ni namna gani ya kutatua hilo… (Makofi)

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

SPIKA: Ahsante sana Mheshimiwa Emmanuel Papian.

MHE. EMMANUEL P. JOHN: Mheshimiwa Spika, ahsante sana na naunga mkono hoja. (Makofi)