Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Kilimo

Hon. Leah Jeremiah Komanya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Meatu

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Kilimo

MHE. LEAH J. KOMANYA: Mheshimiwa Spika, nachukua nafasi hii kuipongeza Wizara ya Kilimo kwa kazi nzuri inayofanya na Mheshimiwa Waziri na Naibu Mawaziri kama timu ya pamoja wamekuwa wakifanya maamuzi yenye tija katika mazao ya chakula na kibiashara. Wilaya ya Meatu imechaguliwa kuwa Wilaya itakayozalisha mbegu mama ya pamba na tayari kazi hiyo inafanyika katika Kata ya Mwabusalu.

Mheshimiwa Spika, mnamo tarehe 5/2/2019 Baraza la Madiwani lilikataa taarifa ya Bodi ya Pamba kuwa Wilaya nzima kuwa ya kilimo cha mkataba tena Bodi ilichelewa kuwaandaa wakulima na pamba iikuwa imechanganya na magugu ya msimu uliopita.

Mheshimiwa Spika, ushauri, kwa msimu huu 2019/2020, pamba haifai kuwa mbegu mama isipokuwa ya Kata ya Mwabusali. Kuruhusu wanunuzi wanaotaka kununua pamba Wilaya ya Meatu ili kuwepo na ushindani wa bei na mkulima anufaike. Katika msimu ujao wanunuzi watakaotakiwa kununua pamba mbegu watapatiwa kwa taratibu za uzabuni, taratibu za Serikali ili kuondoa mazingira ya rushwa.

Mheshimiwa Spika, pia Serikali itengeneze mazingira ya kuwa na bei nzuri ili isitofautiane na bei ya pamba katika wilaya jirani ambayo itawafanya wakulima wasitoroshe pamba wilaya jirani, hivyo kuikosesha halmashauri ushuru wa pamba na kuwavutia wakulima katika kulima kilimo bora. Serikali itoe elimu ya kutosha kwa wakulima wa pamba Meatu kuwa wanalima pamba mbegu mama.

Mheshimiwa Spika, naomba kuwasilisha.