Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

Hon. Maftaha Abdallah Nachuma

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Mtwara Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

MHE. ABDALLAH N. MAFTAHA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kunipatia nafasi hii nami niweze kuchangia mjadala huu jioni hii ya leo inayohusu Wizara ya Elimu. Naomba nianze kwa kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kuendelea kunipa afya njema na leo hii niweze kuchangia Wizara hii ipasavyo. Niseme tu kwamba ninayezungumza hapa pia ni Mwalimu, lakini bahati nzuri nimekuwa kwenye sekta hii ya elimu kama Mkuu wa Shuke kwa miaka mitano, kwa hiyo, nitakachozungumza hapa naomba kitiliwe maanani sana na Waheshimiwa Mawaziri wote wanaonisikiliza; Waziri wa TAMISEMI na Waziri wa Elimu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nianze kwa kauli ya Mwalimu Nyerere mwaka 1968 kwenye kitabu chake cha Education and Self Reliance, naomba nimnukuu, alisema hivi: “an antithesis of education is a kind of learning that enables an individual a learner to attain skills and knowledge and use that skill and knowledge to liberate himself and society in which he or she lives by participating in doing developmental actions.”
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni Mwalimu Nyerere mwaka 1968 alizungumza maneno haya, akiwa na maana ya kwamba, kinyume kabisa na mambo mengine yote, elimu ni jambo la msingi sana; na yule aliyeenda shule, lazima miaka yake yote anayosoma darasani aweze ku-acqure skills, ujuzi na knowledge ile lakini aweze kuitumia ile knowledge kujikomboa mwenyewe lakini kuikomboa jamii inayimzunguka kwa maana ya kwamba kulikomboa Taifa hili la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nazungumza haya kwa masikitiko makubwa sana. Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imekuwa ikileta danadana katika suala hili la elimu kwa miaka mingi sana. Kila Waziri anayeingia anakuja na mitaala yake, anabadilisha system ya elimu; kila Waziri anayekuja anakuja kutunga Sera za Elimu. Mwisho wa siku Taifa kama Taifa hatuna sera, hatuna mtaala mmoja; kila siku tunayumba na hatuwezi kufikia malengo haya ambayo Mwalimu Nyerere aliyazungumza ya kwamba lengo la elimu ni kumfanya aliyesoma aweze kujikomboa mwenyewe na kuikomboa jamii yake inayomzunguka. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, hawezi kuikomboa wala kujikomboa mwenyewe kwasababu elimu yenyewe anayoipata kwasababu inakuwa haina dira, haina mwelekeo kwa maana kwamba hapati elimu ile tunasema quality education, elimu bora. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nalizungumza hili kwasababu leo hii tunavyozungumza kuna Wizara mbili, zote zinashughulikia elimu. Ipo Wizara ya TAMISEMI na ipo Wizara ya Elimu. Cha ajabu kabisa, nimesikia hapa baadhi ya Waheshimiwa Wabunge wakizungumza wakisema hiki usizungumze kwenye Wizara hii ya leo kwasababu hili lipo ndani ya TAMISEMI, wakati sisi Wabunge tunafahamu ya kuwa wakati Waziri Mkuu alivyowasilisha kwa kiasi kikubwa hatuweza kujadili mambo ya elimu. Kwa hiyo, leo ni siku yetu kama Wabunge tuweze kuwaeleza Waheshimiwa Mawaziri wote wawili kwasababu nchi hii, mitaala yake na mfumo wake unayumbayumba katika elimu, lazima tuwaeleze. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, katika hili kwa mtazamo wangu na kwa uelewa wangu na kama Mwalimu mzoefu, siwezi kutofautisha kati ya Wizara ya Elimu ya Waziri Mheshimiwa Ndalichako na Wizara ya TAMISEMI inayoshughulikia elimu. Wote ni kitu kimoja!
Mheshimiwa Mwenyekiti, nizungumzie suala hili la elimu; ili tuweze kuwa na elimu bora ni lazima tuanze katika ngazi zote za elimu. Leo hatuwezi kuzungumzia suala zima la vocational training; elimu ya ufundi ambayo Mheshimiwa Profesa Ndalichako anaishughulikia na elimu ya juu kama hatujaweka misingi imara kuanzia pre-primary education. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, ili tuweze kuwa na wanafunzi wazuri ambao wakifundishwa vocational skills katika vyuo mbalimbali vya VETA Tanzania, ambao wataweza kufundishwa elimu ya juu, lazima wawe wamefundishwa vizuri kuanzia chekechea. Kwa hiyo, Serikali lazima ihakikishe kwamba inawekeza Elimu ya Msingi kuanzia pre-primary school education. Nazungumza haya kwasababu tumezungumza sana kuhusu elimu ya juu kana kwamba hii elimu ya juu inaanzia elimu ya juu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mwaka 2015 na mwaka 2014 nilikuwa nimefanya utafiti mmoja nikiwa Mwalimu; Mwenyekiti wa Wakuu wa Shule Wilaya ya Lindi, nilipewa paper ya ku-present mbele ya Mheshimiwa Kassim Majaliwa inayohusu matokeo makubwa katika elimu. Katika conclusion yangu niliweza kuzungumza baada ya utafiti wangu nilioufanya kwamba huwezi kuzungumia matokeo makubwa katika elimu and then ukaweka neno sasa hivi, kitu ambacho hakiwezekani kabisa. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kwasababu elimu kama elimu ni mchakato ambao ni endelevu. Mwanafunzi anatakiwa afundishwe kwa muda wa miaka miwili au miaka mitatu elimu ya awali. Afundishwe vizuri! Afundishwe vizuri elimu ya msingi lakini akifika sekondari afundishwe vizuri, ndiyo mwanafunzi huyu atakuwa na uwezo wa kufundishwa elimu ya ufundi kwa kufundishwa masomo ya Form Five na Six na masomo ya degree yake, ataweza kufanya vizuri na ataweza kuwa mwanafunzi ambaye atajikomboa yeye mwenyewe na kuikomboa jamii yake inayomzunguka, lakini siyo danadana na mzaha tunaoufanya leo. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwakuwa hili haliwezi kuepukika kama nilivyoeleza hatuwezi kufanya separation kati ya Elimu ya Msingi, Sekondari na Elimu ya Vyuo. Naomba nizungumzie suala zima ambalo Waheshimiwa Wabunge wengi wamezungumza, kuhusu elimu bure. Wizara kama Wizara imetoa Waraka Na. 6 na hapa Mheshimiwa Waziri amezungumza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika ule waraka kuna maelekezo Waheshimiwa Wabunge naomba myasikilize ambayo yanaeleza, nami hapa waraka wenyewe ninao hapa, huu hapa Waraka Na. 6. Imeelezwa mle ndani kwamba katika mgawanyo wa pesa zinazopelekwa shuleni inatakiwa zitumike katika muktadha ufuatao: Matumizi ya kwanza ni matumizi ya jumla ya ofisi. Hapa tunamaanisha vitambulisho, shajara, maandalio, ulinzi, umeme, maji na fedha za kujikimu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lingine (b), kuna suala zima la uendeshaji wa taaluma, kuna suala zima la mitihani endelezi, kuna suala zima la madawa baridi ya binadamu, mahitaji ya wasichana na kadhalika na matengenezo madogo madogo. Sasa jambo la kusikitisha, ukija katika utekelezaji wa hiyo sera, nilikuwa nafanya utafiti tu kwenye shule zangu kule Jimbo la Mtwara Mjini, ni jambo la ajabu sana. Shule imepelekewa shilingi 27,000/= halafu inaambiwa ifanye mgawanyo huo wote.
MHE. ABDALLAH N. MAFTAHA: Mheshimiwa Mwenyekiti, siungi mkono hoja.