Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa

Hon. Boniphace Mwita Getere

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bunda

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa

MHE. BONIPHACE M. GETERE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi na mimi ya kuchangia hizo dakika ambazo nimepewa. Mimi nimshukuru Waziri wa Ulinzi, Waziri mwenye TBS ambaye amekaa Serikalini muda mrefu, lakini anafanya kazi iliyotukuka kwa kweli anapaswa kupongezwa. (Makofi)

Niwashukuru Wakuu wa Majeshi, Mkuu wa Majeshi aliyepo CDF na wenzake wote wanafanya kazi nzuri. Duniani tunaposema nchi, maana yake ni Jeshi hakuna kitu kingine ambacho kinakuwepo zaidi ya hapo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nilitaka nizungumze mambo tu kwamba ukiangalia kwenye maeneo mengi sasa kwenye hizi ukaguzi wa CAG, kuna suala la SUMA JKT. Mimi nilikuwa nataka kusema kitu kimoja, Jeshi ni jambo, ni kitendo, ni tukio, ni kitengo ambacho kinatakiwa kuwa kitakatifu cha kutosha, hasa ukija kwenye Jeshi ukakuta kuna vitu vidogo vidogo hivi vinazungumzwa SUMA JKT nimeona hapa ukurasa wa 34/35 kwamba wamekusanya madeni milioni 330, bilioni 1.545, wamekusanya madeni lakini kutoka kwenye deni kubwa lipi? Hapa ni madeni wamekusanya, kutokea deni kubwa lipi sasa? Maana yake tuseme kulikuwa na madeni labda bilioni mbili, wamekusanya bilioni moja tukasema labda wako afadhali. Lakini kitendo ukiangalia kwenye kitabu cha CAG kinaleta kasoro, kwa hiyo, tunaomba SUMA JKT wafanye kazi iliyotukuka kukusanya madeni na waone yale matrekta yanasaidia nini wananchi wa Tanzania. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna eneo hapo lipo Kilimo Kwanza, nilenda pale nikafikiri labda kuna matrekta kama yanauzwa. Nikaambiwa kumbe matrekta yale yalisharudishwa Serikalini, yako pale Kilimo Kwanza, yamekusanywa yalikuwa yamerudishwa ili yaweze kulipwa wale wenyewe waweze kurudisha madeni yao. Sasa yamekaa pale, ni ya Serikali, hayajaenda kwa wananchi, hayalimi, hayauzwi yapo tu. Sasa nikasema hii maana gani hii, mambo gani haya tunafanya haya. Kwa hiyo, nasema kwamba Mheshimiwa Waziri naomba mkitoka hapa bajeti ikipita najua mnapitishwa, mkaangalie utaratibu, yale matrekta chukueni. Kama hamuwezi kuyauza yana bei ndogo, warudishieni wakulima waliokopa wakafanya kazi watakuwa wanalipa kidogo kidogo ili waweze kupata hiyo ajira yao. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo muhimu sana katika nchi yetu, kama JKT na kama Jeshi la Tanzania ambalo lina maeneo makubwa sana katika nchi hii, litatumia vijana wa JKT katika mambo ya kilimo na kuajiriwa tutafanya kazi kubwa sana. Nimeenda kwenye eneo moja linaitwa Chita kama unaenda Ifakara, Morogoro, eneo kubwa, bonde kubwa kuna matrekta lakini hakuna kazi inayofanyika. Nenda maeneo yote ya makubwa ya JKT, kuna maeneo mazuri, makubwa tunaomba JKT na Jeshi kwa ujumla watumie vijana wetu wale wa JKT kuwapa ajira kwenye maeneo hayo, mbona inawezekana, shida iko wapi? Kwa sababu uwezo wa kuwapa matrekta tunao, uwezo wa kuwahimili tunao, ....kuwapa tunao, shida iko wapi.

Kwa hiyo, naomba Waziri mwenye TBS uhakikishe kwamba vijana wetu wanapata ajira kutokana na maeneo makubwa ya JKT, tunaomba utusaidie namna ya kuyafanya. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, niwapongeze tu kwa ujumla, hatuna namna yoyote ya kulaumu mambo ya Jeshi. Mtu anayezungumza Jeshi labda ana kichaa, kwa sababu hawa ndiyo wanafanya nchi inakuwepo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana, naunga mkono hoja. (Makofi)