Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Viwanda na Biashara

Hon. Lucia Ursula Michael Mlowe

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Viwanda na Biashara

MHE. LUCIA M. MLOWE: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuchangia katika hoja hii kama ifuatavyo.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza, napenda kuchangia kuhusu matatizo ya wafanyabiashara. Watu wengi wamefunga biashara zao kutokana na manyanyaso wanayoyapata kutoka kwa watu wa TRA. Wafanyabiashara wengi kabla ya kuanza biashara anapitia hatua nyingi ambazo zote ni za tozo mbalimbali. Kabla mtu hajaanza kuuza biashara yake anaanza kutoa fedha za kodi na wakati huo makadirio ya TRA yanakuwa makubwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuishauri Serikali kwamba watu wanapofungua biashara wasikadiriwe tozo hadi wafanye biashara zao kwanza waone mapato wanayoyapata ndipo waanze kutozwa kodi. Ndiyo maana watu wanafungua biashara kwa kodi hiyo kubwa, mwisho wa siku wanaona ni gharama wanaamua kufunga biashara zao.

Mheshimiwa Naibu Spika, pili, SIDO. Naomba viwanda vidogovidogo viimarishwe kwani ni muhimu sana. Vimekuwa vikiwasaidia wajasiriamali wadogowadogo lakini SIDO haichukuliwi kama ni muhimu. SIDO inaweza kuajiri wanawake na vijana wengi nchini lakini hata bajeti ya kutosha haitengwi. Naitaka Serikali ilichukue suala hili la SIDO kwa umakini na kutenga bajeti ya kutosha kwa ajili ya SIDO.

Mheshimiwa Naibu Spika, tatu, Liganga na Mchuchuma. Sijui ni kwa nini mradi wa Liganga na Mchuchuma unasuasua wakati sisi kama Wabunge wa Mkoa wa Njombe tumehamasisha wananchi kufanya maandalizi ya mradi huo kwa kilimo cha mazao mbalimbali yakiwemo matunda na mbogamboga. Wananchi wamefanya bidii kulima lakini mazao yao hayana soko kwa kuwa walikuwa wanategemea mradi wa Liganga na Mchuchuma. Niitake Serikali iharakishe mradi huo.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuwasilisha.