Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

Hon. Shally Josepha Raymond

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

MHE. SHALLY J. RAYMOND: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa fursa ya kuchangia na uongozi mzuri huku Bungeni. Pongezi kwa Mheshimiwa Waziri, Naibu Waziri, Katibu Mkuu, IGP na Wakuu wote wa Majeshi yote, Zimamoto na Uokoaji, Magereza na Idara ya Uhamiaji kwa ufanisi mzuri.

Mheshimiwa Spika, kwa kipindi cha miaka miwili mfululizo wizi wa magari umepungua sana, ajali barabarani zimepungua na hata wizi wa kuvunjiwa nyumba. Hizi zote ni juhudi za Jeshi la Polisi, pongezi sana sana.

Mheshimiwa Spika, ombi, uongozi wa Jeshi la Polisi uone umuhimu wa kulipa deni kubwa la maji, linalodaiwa na Mamlaka ya Maji safi na Salama na Uondoaji wa Majitaka Moshi (MUWSA) Ref. Deni la CCP-MSH. Deni hili limeshahakikiwa lakini ni zaidi ya miaka saba halilipwi. Naomba sana Mheshimiwa Waziri atakapokuwa anajibu hoja alitolee maamuzi, la sivyo nitalazimika kushika shilingi kwenye mshahara wake japo sipendelei kabisa kufanya hivyo kwa Waziri makini.

Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja kwa asilimia mia moja.