Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

Hon. Omari Mohamed Kigua

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilindi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

MHE. OMARI M. KIGUA: Mheshimiwa Spika, pamoja na kwamba nimechangia, lakini naomba tena kuchangia kwa maandishi hoja yangu ya mwisho ambayo sikutaka sana kuisemea kwa upana nilitaka kuandikia hapa na naomba Mheshimiwa Waziri anipatie majibu.

Mheshimiwa Spika, hoja yangu ni kwamba, Mzee Ally Mwegango mkazi wa Kibirashi, Wilaya ya Kilindi ambaye alinunua gari kwa bwana Karl Muller kwa Sh.23,000,000 tarehe 7/7/2015 kwa akaunti namba 9120000187753 Benki ya Stanbic na gari hii kukabidhiwa kwa Mzee Ally Mwegango . Tarehe 12/12/2017 gari hili lilikamatwa na Kampuni ya COPS Auction Mart & Court Brokers kwa maelekezo ya Benki ya Redstone Financial Services. Kimsingi muuzaji Mzee Karl Muller aliuza gari hili huku akijua amechukua mkopo kwenye Financial Services, kimsingi ni tapeli au mwizi. Jeshi la Polisi limeshindwa kuchukua hatua kwa mtu huyu na kumnyima haki Mzee Ally.

Mheshimiwa Spika, Mzee Ally huu ni mwaka wa pili sasa anafuatilia gari lake na lipo barabarani linafanya kazi. Nina imani kubwa sana na jeshi hili na pia naamini Mheshimiwa Waziri na wote waliopo chini yake wanalijua vema suala hili, hivi kama mimi Mbunge na mlalamikaji sote hatusikilizwi, hivi wanataka tuamini kwamba mhalifu huyo ana nguvu au yupo juu ya sheria?

Mheshimiwa Spika, ili kutenda haki kwa mlalamikaji Mzee Ally ambaye aliamini kabisa gari alilonunua lingemsaidia kujipatia riziki yake na familia, leo hii gari hili lipo kwenye mikono ya mtu mwingine, nina imani kubwa na nina uhakika suala hili linaweza kumalizika kwa kumkamata huyu tapeli au mwizi ambaye anafahamika wazi.

Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja.