Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

Hon. Abdallah Dadi Chikota

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nanyamba

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

MHE. ABDALLAH D. CHIKOTA: Mheshimiwa Spika, naipongeza Wizara kwa kazi nzuri inayofanya katika kutekeleza majukumu yake, ikiongozwa na Waziri, Mheshimiwa Kangi Lugola na Naibu wake Mheshimiwa Mhandisi Hamadi Masauni.

Mheshimiwa Spika, mchango wangu utahusu maeneo matatu. Kwanza ni nyenzo za kufanyia kazi. Kuna changomoto kubwa ya vitendea kazi kwa Majeshi yetu ya Polisi, Magereza na lile la Zima Moto. Naomba Serikali kuangalia kwa karibu suala hili kwani imefika mahali ikitokea dharura, Polisi wanategemea msaada wa vyombo vya usafiri kutoka kwa watu binafsi kwa kutokuwa na gari au gari kukosa matengenezo. Si ajabu kuona Magereza nao wanaomba kusaidiwa usafiri kutoka kwa watu binafsi ili kwenda kusaga chakula cha wafungwa. Nashauri majeshi haya yapewe fedha za kutosha kugharamia vitendea kazi, ununuzi wa mafuta, posho za askari na stahili zao zingine pamoja na sare zao.

Mheshimiwa Spika, pili, Kituo cha Polisi Nanyamba. Kituo hiki kilijengwa kama Police Post kuhudumia Tarafa ya Nanyamba miaka ya nyuma. Kwa sasa Nanyamba ni Halmashauri ya Mji na Jimbo na idadi ya watu imeongezeka na matukio ni mengi. Naomba yafuatayo yafanywe: Kituo hiki kiboreshwe ili kukidhi haja ya kuhudumia eneo husika; idadi ya askari waongezwe; na wapewe usafiri wa magari na pikipiki.

Mheshimiwa Spika, tatu, magari ya Zimamoto ni ya muda mrefu, machache na hayatoshelezi. Nashauri zitengwe fedha za kununua magari zitakazopelekwa kila Halmashauri hata kwa kununua awamu kwa awamu.

Mheshimiwa Spika, nawasilisha, naunga mkono hoja.