Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

Hon. Hussein Mohamed Bashe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

MHE. HUSSEIN M. BASHE: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kunipa fursa. Jambo la kwanza nitumie nafasi hii kwanza kwa dhati kabisa kulipongeza Jeshi la Polisi na nawapongeza tukiwa honest sasa hivi katikaTaifa letu wamefanya kazi kubwa sana ya kudhibiti uhalifu na ujambazi mkubwa hasa katika maeneo ambayo yalikuwa yanaathirika ya pembezoni mwa nchi na ambayo yamezungukwa na nchi ambazo zina instability. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, Jeshi la Polisi wamefanya kazi kubwa sana ya kudhibiti na kuleta utulivu na amani hasa sisi tunaotoka Mikoa ya Kanda ya Magharibi, zamani ilikuwa ukifikiria kusafiri kukatiza kutoka Dodoma hapa ukaseme ukalale Bukoba, ilikuwa ni mtihani. Kwa hiyo wamefanya kazi kubwa sana tunawashukuru na Mwenyezi Mungu awajalie kwa kazi hii wanayoifanya. (Makofi)

MBUNGE FULANI: Amina.

MHE. HUSSEIN M. BASHE: Mheshimiwa Spika, nataka niongee mambo machache kuhusiana na polisi. Polisi wetu wanafanya kazi katika mazingira magumu, ni muhimu sana ndani ya Serikali kuangalia ni namna gani stahiki za polisi na majeshi mengine zinakuwa harmonized, kwa sababu suala la usalama linaanza na intelligence kwa maana ya kukusanya taarifa, lakini suala la kuzuia, suala la ku-enforce, hizi ni kazi ambazo zinashabihiana. Kwa hiyo, kuna umuhimu sana wa kuangalia ni namna gani stahiki za askari wa Jeshi la Polisi zinakuwa harmonized na majeshi mengine ili kuleta uwiano ulio sawa kwa sababu majukumu yao yanategemeana. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, leo askari wetu wanafanya kazi over time, hawapati kulipwa over time, wanafanya kazi masaa 12, akiingia kwenye lindo ni masaa 12 na hii ni kutokana na uchache wa askari katika maeneo yao. Kwa hiyo ni muhimu sana Serikali iangalie. Nataka niishauri Serikali, watafakari, mfano, sasa hivi huwa tunasikia kwenye TV kwamba kutokana na makosa ya barabarani askari wamekusanya bilioni 700, hivi is it not possible ndani ya Serikali wakatengeneza utaratibu katika kila kituo angalau twenty percent ya hizi fedha wanazokusanya zibaki kituoni. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nataka nitoe mfano, pale Nzega kwangu leo ni mwaka wa tatu askari wamekatiwa maji, Jeshi la Polisi. Pale Nzega kwetu LUKU wanaweka kutoka mfukoni kwao na it’s an average ya shilingi laki moja kwa mwezi wanayotumia. Kwa hiyo wananchi wanachanga changa na wenyewe saa nyingine wanatoa fedha zao mfukoni, Mkuu wa Kituo hawezi kukubali usiku pasiwe na taa katika kituo chake cha polisi na ni kwa sababu ya ukata.

Mheshimiwa Spika, pale Nzega tuna household za askari familia 17, leo sisi katika halmashauri tumeamua kuanza kutafuta fedha ili tuanze kujenga makazi ya askari, tunaiomba Serikali iangalie, ni vizuri sana kuangalia hawa watu kazi wanayoifanya ilivyo ngumu iweze kwenda na stahiki zao. Tunaweza tukaja hapa ndani tukawalaumu kuwa wanachukua rushwa, je, tumeangalia, nimemsikia Haonga rafiki yangu amesema tuwape two million, nadhani tusingeanzia kwenye two million, tungeanzia namna gani tunatengeneza uchumi imara ambao utakuwa na mapato imara ili tuwalipe vizuri askari wetu. Hili ndiyo jambo la msingi kabisa, lazima tuanze na kutazama haya mambo in a broader perspective, itatusaidia kama nchi kwenda mbele. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, jambo lingine ambalo nataka niongelee, ni vizuri Serikali ikaangalia custodian wa border control ni migration. Je, equipments tunazowapa watu wa Uhamiaji, kwa sababu ndiyo mwenye jukumu la kuangalia mipaka, wanaoingia na kutoka, ni vizuri hili Jeshi la Uhamiaji likawa a unit inayojitegemea, inayojiendesha, iwe na resources zake, iwe na proper plan tujue ndani ya miaka mitano border control zetu zitaendeshwa namna gani. Hii ni muhimu sana ili kuweza kuingiza efficiency katika kazi wanazofanya. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nataka niongelee jambo lingine mahsusi. Kwa miaka mitatu ambayo nimekuwa humu ndani ya Bunge na kabla sijaja Bungeni, kumekuwa na mjadala mkubwa sana juu ya suala la Masheikh waliowekwa magereza. Leo ni mwaka karibu wa sita, nataka niiombe Serikali kwa heshima kabisa na mwaka jana walitoa ahadi hapa, hawa watu kama wana makosa wapelekeni mahakamani dunia ijue kwamba hawa watu wana tuhuma moja, mbili, tatu kuliko kuendelea kuwa-hold ndani with no clarity, inaleta maswali mengi, ina distort image, inasababisha watu wengine kupata hoja ya kujadili jambo ambalo halina sababu. Nataka nimwombe Mheshimiwa Waziri atakapokuja kufanya wind up, hebu tuelezeni faits na direction ya suala la Mashekh walioko magereza. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, jambo la pili nataka niliombe Jeshi la Polisi na Mheshimiwa Rais alisema hili, alisema Watanzania siyo wajinga, Watanzania wanaona, nami nitaongea kuhusu hili ninalolisema na lingine linaloitwa la task force. Kuna mambo yanasemwa halafu response inayopatikana kutoka kwenye authority is just a political response, kuna mambo ambayo yanatajwa ya ki-criminal yanatakiwa yapate majibu complete. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, mfano, imesemwa sana hapa na Mheshimiwa Bwege amewahi kuisema mara nyingi, nataka nimwombe Mheshimiwa Kangi hebu wamwambie Mheshimiwa Bwege awasaidie. Kuna hoja inayosemwa sana sana na inaenda kwa umma, inayozungumzia Masheikh wa Tablih waliopigwa risasi inayosemwa huko Kilwa sijui, this things need answers. Kama ni taarifa za uongo, wanaotengeneza taarifa hizi za uongo wachukuliwe hatua, we should not allow mambo ya uongo yanasemwa semwa, yanaachwa, halafu siku ya mwisho yana-distort heshima na image ya Taifa hili. This country imejengwa katika misingi imara ya utu, hili ni muhimu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, jambo lingine, nataka niseme kuhusu minority society, nataka niiombe Serikali, pale Uhamiaji waanzishe dawati maalum linalohudumia wahamiaji katika nchi hii. Community ambazo ni minority, Idara ya Uhamiaji zimegeuka ni mradi, halafu jambo la kushangaza anakwenda mtu akionekana Msomali anaambiwa wewe siyo raia, leta cheti cha bibi na bibi yako watano, anatoa wapi? Kwa sababu hata huyo Afisa yeye ukimuuliza cheti cha bibi yake wa nne hana, basi fanyeni audit. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, Nzega kuna familia tano za Wasomali zinajulikana ambao familia ile hawako watu hata arobaini. Suala la uhamiaji jamani siyo dhambi, today Rais wa Taifa kama Ireland ni Mhindi, kwa hiyo Uhamiaji na migration nataka niwaambie, hivi mnajua neno sukuma! Hawa Wasukuma ni wahamiaji kwenye nchi hii, ni Northerner. Neno sukuma, kisukuma maana yake ni Kaskazini. (Makofi/ Kicheko)

SPIKA: Ilikuwa ni Mheshimiwa Ndassa au nani alisimama! (Kicheko)

MHE. HUSSEIN M. BASHE: Yupo. (Kicheko)

SPIKA: Au Mheshimiwa Chegeni!

MHE. HUSSEIN M. BASHE: Wote.

SPIKA: Nilisikia kama taarifa hivi, Mheshimiwa Bashe endelea. (Kicheko)

MHE. HUSSEIN M. BASHE: Mheshimiwa Spika, ninachotaka niseme ni hivi, dunia leo you cannot restrict migration, tengeneza proper administrative measures zitakazokusaidia wewe migrants kukusaidia kwenye nchi, because the world is village, hili ni muhimu sana. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, jambo lingine ambalo nataka niongelee, Mheshimiwa Kangi nitampa majina. Sasa hivi kuna watu wanahama nchi yetu especially business community na wanasumbuliwa na watu wanaoitwa task force. Kinachotokea na nitampa Mheshimiwa Kangi majina hapa, transporters walioko Wilaya ya Temeke ambao wana asili ya Kisomali na ni Watanzania, mfano mtu anaitwa Abdigul Abdi Kulane ambaye ana kampuni inaitwa Kulane and Sons Company Limited alifuatwa nyumbani kwake Kinondoni akachukuliwa, leo ni miezi miwili hajulikani alipo. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kuna mtu anaitwa Abushir Ally, huyu mtu kachukuliwa, leo hayupo, walichukuliwa wane, wenzao wawili wameachiwa baada ya kutoa fedha na wao walichokifanya, angalia hiki kitu, wametoka wamehamisha Transport Company yao wamehamia Zambia.

Mheshimiwa Spika, kuna mtu anaitwa Abushir Ally, huyu mtu kachukuliwa leo hayupo. Walichukuliwa wanne, wenzao wawili wameachiwa baada ya kutoa fedha na wao walichokifanya, angalia hiki kitu, wametoka wamehamisha Transport Company yao kwenda Zambia. This is happening. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, wafanyabiashara hawa wakubwa kwa hizi task force wanachokifanya sasa hivi, wengi wanahamisha biashara. Nakuomba Mheshimiwa Waziri, tazameni hizi task force zinavyoundwa na bahati mbaya Kituo cha Polisi mtu akienda anaambiwa huyo wala usihangaike yuko chini ya task force, wala sisi hatuna control naye. Sasa hizi task force ambazo hazina controls zitaathiri image ya nchi yetu, kazi kubwa inayofanywa image yake itakuwa distorted. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, namwomba Mheshimiwa Kangi, angalieni hizi task force zinazoundwa, lazima ziwe zina TOR, majibu. Watu wasipokuwa na majibu juu ya family members wao, inaleta shida na ukakasi mkubwa sana katika community.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, nataka ni-conclude kwa kuiomba Wizara ya Mambo ya Ndani, mnafanyna kazi kubwa sana ya kulinda usalama wa raia. Niwaombe, moja, angalieni maslahi ya askari kuya-harmonize na majeshi mengine, ni muhimu sana ili kuwajengea confidence askari wetu.

Mheshimiwa Spika, la pili, naomba Idara ya Migration waache kugeuza minority society mradi. Tengenezeni Dawati Maalum litakalohudumia na ikiwezekana familia zilizoko hapa nchini ambazo ni migrants, minority zinaweza kujulikana, it’s easy kuwa na database ambayo itaondoa hii shida. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, mfano mdogo wangu mimi kaenda siku ya kwanza kapata shida, siku ya pili mmoja kaangalia jina la mwisho alivyoona Bashe akasema wewe ni mdogo wake na Mbunge. Sasa yule ana privilege ya mdogo wake na Mbunge, wangapi hawana? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, mimi nataka niiombe Serikali, ni vizuri sana haki za raia zilindwe na mwenye wajibu wa kutoa majibu juu ya masuala yenye ukakasi ni Wizara ya Mambo ya Ndani, toeni majibu juu ya haya mambo yanayosemwa.

Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja, ahsante sana. (Makofi)