Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo ya Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali Pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

Hon. Yahaya Omary Massare

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manyoni Magharibi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo ya Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali Pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

MHE. YAHAYA O. MASSARE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi na mimi nichangie mapendekezo haya ya Mpango ya mwaka 2019/2020.

Mimi nataka nianze na suala la umaskini ambalo limeoneshwa katika ukurasa wa nane. Jambo hili lina dhamira njema nimeona dhamira ya Serikali katika mapendekezo haya. Lakini kuna taatizo kubwa hapa riba ya mikopo hasa kwa taasisi ambazo hizi mabenki yetu imekuwa si rafiki kwa watu wetu wengi. Ni namna ngumu sana wananchiili waweze kujiwezesha hususani wajasiliamali wadogo wadogo, taasisi hizi za fedha lazima ziwe rafiki na ili uchumi wa nchi hii uweze kwenda mbele, wananchi hawa wakiweza kukopeshwa lakini tuweze ku-increase export katika mazao yetu ikiwemo mazao ya misitu, asali na mazao mengine ya kilimo ambayo yamekuwa na matatizo makubwa tumeshuhudia kuona leo mazao kama ya mbaazi yamekuwa hayauziki katika mikoa ambayo inalima mazao haya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nilikuwa napendekeza Serikali tuishauri ione namna bora ya kuwezesha wananchi wakulima hasa wadogo wadogo wa vijijini ili waweze nao kushiriki katika kujenga uchumi wa nchi hii. katika suala la kilimo limeonyeshwa ukurasa wa 17 lakini ni namna gani tunawezesha wakulima tumeshuhudia kuona matrekta yako pale Kibaha yanaunganishwa, ni kwa nini basi sasa tusijikite namna bora kama iliyofanya ile kilimo kwanza ambayo imepelekea nchi hii leo tunajitegemeakwa kiasi kikubwa sana katika uchumi hasa kilimo tumekuwa ukanda huu wa Afrika tumekuwa tunauza mazao kwa nchi za ambazo tumepatakana nazo kwa sababu mpango wa kilimo kwanza ulikuwa na tija matrekta yalikuwa vijijini na wananchi walikuwa wanalima.(Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mikopo ambayo ilikuwa ni rafiki japo wengine changamoto zilijitokeza wengine hawakuweza kulipa lakini sio iwe ndoo tatizo tu-deal na issue ya mtu ya mmoja mmoja, mpango ule wa kilimo kwanza ulifaulu sana na matrekta yanapokaa pale Kibaha sioni kama itakuwa ni faida kwa Serikali hata huyu muwekezaji tunamvunja moyo kuona matrekta badala ya kwenda kwa wakulima kule vijijini ili yaendelee kuleta mengine basi anakuwa hawezi kufanya.(Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, napendekeza katika kuboresha uchumi suala zima la gesi nalo tulione gesi iko Dar es Salaam leo makazi ya watu wa Dar es Salaam nimeona majaribio yanataka kufanyika kwa maeneo machache tu yakiwemo kwenye maeneo makazi ya watu wanene kule Masaki na maeneo mengine. Lakini maeneo ya makazi ya watu wadogo kama sisi tunaokaa pembezoni basi isaidie gesi hii iwe sehemu kubwa ya kupikia kuondokana na ukataji wa miti ambao si rafiki kwa maendeleo ya nchi yetu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la mifugo tumelina ukurasa wa 18, lakini hakuna mikakati kabisa inayoonesha kwa makusudi mazima kuona sasa mifugo hii yetu inatoka katika utaratibu ule wa kuchunga na sasa waweze kufuga. Ni vizuri tumeona kwamba mna mpango wa madume bora, lakini naona ni machache ambayo yako kwenye taasisi tu kubwa kubwa, wafugaji wadogo wadogo bado hatujawaweka wala hatujawa-accommodate kama nao wawe sehemu ya kunufaika na mapendekezo haya ambayo yanaletwa mbele ya Bunge hili tukufu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimeona katika ukurasa wa 27 na 28 barabara nyingi zinaonekana zinataka kujengwa, lakini bado barabara zinazounganisha mikoa hazijamalizika. Mikoa ya Singida kuunganisha na Mkoa wa Mbeya ambako na mimi jimbo langu limo humo, barabara yake haionekani humu katika mapendekezo ya mpango huu. Ni mpango gani upo na Serikali kwamba tunauunga Mkoa wa Mbeya kupitia Itigi? Lini sasa wataanza kuonesha katika mapendekezo yajayo?

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba Mheshimiwa Waziri uje na mapendekezo yanayoonesha utakapokuja kwenye mpango tuone ni nini dhamira ya Serikali ya kuunganisha wananchi wa mkoa mmoja na mkoa mwingine, ukiwemo Mkoa wa Singida na Mkoa wa Simiyu. Daraja la Sibiti tumeliona kwa hili nipongeze sana na juhudi za Serikali ziko wazi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukurasa wa 30 wa mapendekezo haya, nimeona nishati vijijini (REA). Bado wakandarasi wengi hawajaanza kufanya kazi, hatujui tatizo ni nini. Sasa kwenye mapendekezo haya hatuoni dhamira gani ya Serikali Mkoa wetu wa Singida mojawapo ni miongoni mwa mkoa ambao REA wamefika, lakini hawajaanza kazi, basi tunataka tuone maboresho katika sula hili.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tumeona suala la afya umelionesha katika ukurasa wa 38, lakini bado Hospitali za Rufaa ni changamoto, tumeona hospitali moja tu mmeitaja, Hospitali ya Benjamin Mkapa, lakini mikoa mingine hospitali zao za rufaa hazijaoneshwa kwamba hamjazizingatia katika mapendekezo ya mpango huu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, yako mengi ambayo tunatakiwa kuona, lakini Wabunge wanataka kuona mchakato huu wa reli unafika basi Kigoma, unakwenda hadi Mwanza, umeoneshwa tu kwa kifupi. Nichukue nafasi hii kumshauri Mheshimiwa Waziri azingatie hilo nalo na kwenda makutupora basi na kule mbele tuone basi juhudi hizi ambazo zinaendelea.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi nilikuwa na haya machache tu ya kuchangia mpango huu wa mapendekezo ambayo nimeona kwa kweli, dhamira njema ya Serikali ya kufanya maendeleo katika nchi hii. Ahsante sana, naunga mkono hoja.