Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Mohammed Maulid Ali

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kiembesamaki

Primary Question

MHE. MAULID ALI MOHAMED aliuliza:- Je, ni lini Serikali itakifanyia ukarabati Kituo cha polisi Mazizini pamoja na kukarabati nyumba za Askari?

Supplementary Question 1

MHE. MAULID ALI MOHAMED: Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Waziri naomba kumpa ushauri mmoja. Kituo hiki ni kituo chetu cha Wilaya na bahati mbaya sana kipindi cha mvua askari wetu wanalazimika kuhama kule juu kwa sababu kumekuwa na bwawa. Sasa pamoja na hiyo program ya kutengeneza nyumba zote za polisi lakini ningeomba kitu kimoja. Kama kuna uwezekano wa lile paa lifanyiwe dharura halafu masuala mengine yatafuata baadaye, ahsante.

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, napokea ushauri wake tutaufanyia kazi na mara nitakapopata nafasi ya kuja Kiembe Samaki tutapata nafasi pia ya kushauriana Mheshimiwa Mbunge.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana.

Name

Oliver Daniel Semuguruka

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MAULID ALI MOHAMED aliuliza:- Je, ni lini Serikali itakifanyia ukarabati Kituo cha polisi Mazizini pamoja na kukarabati nyumba za Askari?

Supplementary Question 2

MHE. OLIVER D. SEMUGURUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kuniona niweze kuuliza swali la nyongeza. Changamoto iliyopo Kiembe Samaki inafanana kabisa na changamoto iliyoko Wilaya ya Ngara kituo cha Polisi cha Rurenge kimchakaa kabisa mpaka kinavuja. Je, ni lini Serikali itakifanyia ukarabati kituo hicho?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimwa Oliver kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Wizara inatambua uchakavu wa Kituo cha Polisi Rurenge tena ambacho kiko karibu na mpaka. Kama nilivyoeleza katika majibu niliyomjibu hivi karibuni ni mpango wa Serikali kuvikarabati vituo vyote kikiwemo hiki cha Rurenge na hivi vituo vya mpakani Mheshimiwa Mbunge tutavipa msisitizo maalum, nashukuru.

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Primary Question

MHE. MAULID ALI MOHAMED aliuliza:- Je, ni lini Serikali itakifanyia ukarabati Kituo cha polisi Mazizini pamoja na kukarabati nyumba za Askari?

Supplementary Question 3

MHE. MWITA M. WAITARA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, naomba nimuulize swali la nyongeza Mheshimiwa Waziri kwamba kule Tarime eneo la Rorya, Sirari, Nyasicha, Muliva, Itilio, Nyanungu. Eneo hilo kuna malalamiko ya wananchi mengi kwamba wale maaskari wanatembea na marungu kwenye magari kwa hiyo, watu wakikamatwa wanapigwa sana. Nilitaka niulize utaratibu wa sheria umebadilika au huu ni mtindo wa kule Tarime ndio tu upo kwa sababu ni kanda maalum? Ahsante.

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Waitara Mbunge wa Tarime Vijijini kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, si mpango wa wizara wala Jesho la Polisi kutembea na marungu kwenye magari kwa ajili ya kupiga wananchi wake. Lakini nafahamu kwamba kuna wakati Askari wanalazimika kukamata wahalifu na wahalifu wanapofanya upinzani nguvu inayotakiwa kutumika ni ile tu inayoshabihiana na nguvu pinzani lakini si marungu kwa ajili ya kupopoa wananchi wetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru.

Name

Bakar Hamad Bakar

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

House of Representatives

Primary Question

MHE. MAULID ALI MOHAMED aliuliza:- Je, ni lini Serikali itakifanyia ukarabati Kituo cha polisi Mazizini pamoja na kukarabati nyumba za Askari?

Supplementary Question 4

MHE. BAKAR HAMAD BAKAR: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana. Nyumba za Askari katika kambi ya Askari Mfikiwa ni chakavu sana. Je, ni upi mpango wa Serikali katika kuziboresha nyumba zile?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kama nilivyojibu kwenye jibu la msingi tunatambua uwepo wa uchakavu wa vituo na makazi ya Askari. Kama nilivyokwishakusema ni mpango wa wizara kufanya ukarabati wa majengo hayo kutegemeana na uwepo wa bajeti. Mwaka huu tutaanza na yale ambayo yapo kwenye kipaumbele tutaendelea na ukarabati kadri miaka inavyokwenda kulingana na upatikanaji wa fedha nashukuru.

Name

Dorothy George Kilave

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Temeke

Primary Question

MHE. MAULID ALI MOHAMED aliuliza:- Je, ni lini Serikali itakifanyia ukarabati Kituo cha polisi Mazizini pamoja na kukarabati nyumba za Askari?

Supplementary Question 5

MHE. DOROTHY G. KILAVE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, nina swali moja nyumba za bara pale Kilwa Road. Kuna maghorofa yalitangulia kujengwa sasa sijui ndio yameishia pale pale na wale wengine bado wako kwenye zile nyumba ambazo Kilwa Road Barax. Maghorofa yale yamejengwa vizuri lakini katikati pana nafasi sijui ndio mwisho pale maana yake zile nyumba sasa ni ndogo sana na zinavuja?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge Dorothy Kilave wa Temeke kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, ujenzi wa kota za Askari kule Temeke Kilwa Road unaendelea na kama pana dosari zozote ambazo zimeoneshwa na Mbunge kama maeneo mengine yanavuja tutamwelekeza IGP ili kumsimamia mkandarasi aweze kusimamia mjenzi ahakikishe kwamba viwango vilivyowekwa vinazingatiwa ili kuondoa hizi dosari ambazo zimeonekana.