Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 30 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 265 2022-05-25

Name

Mohammed Maulid Ali

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kiembesamaki

Primary Question

MHE. MAULID ALI MOHAMED aliuliza:-

Je, ni lini Serikali itakifanyia ukarabati Kituo cha polisi Mazizini pamoja na kukarabati nyumba za Askari?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimwa Maulid Ali Mohamed Mbunge wa Kiembe samaki kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imefanya tathmini ya uchakavu wa kituo na nyumba za makazi za askari polisi Mazizini na kubaini kuwa kiasi cha fedha shilingi 64,484,700 zinahitajika kugharamia ubadilishaji paa, dari, mfumo wa umeme, maji safi, maji taka na kupaka rangi. Ukarabati huo utafanyika kulingana na mpango wa ukarabati kutegemea na upatikanaji wa fedha.