Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Hussein Nassor Amar

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nyang'hwale

Primary Question

MHE. HUSSEIN N. AMAR aliuliza:- Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi iliyotolewa na Waziri Mkuu Mheshimiwa Kassim Majaliwa Majaliwa ya Ujenzi wa barabara ya Kharumwa yenye urefu wa kilometa mbili kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 1

MHE. HUSSEIN N. AMAR: Mheshimiwa Spika kwa kunipa nafasi niweze kuuliza maswali mawili madogo ya nyongeza.

Kwa kuwa Mwenyezi Mungu amefungua neema katika Wilaya ya Nyang’ahwale kuwa na machimbo mengi sana ya dhahabu na kuwa kuna mzunguko mkubwa wa kiuchumi ikiwemo ongezeko la vipando vya magari pamoja na pikipiki; pamekuwa panapitika magari zaidi ya elfu moja kwenye makao makuu ya wilaya na kutimua vumbi jingi. Kwa kuwa Serikali imesema itajenga hizo kilometa mbili; je, ni lini kwa kauli ya Serikali ujenzi huo utaanza?

Mheshimiwa Spika, swali la pili; niishukuru Serikali kwa kuweka mpango wa kujenga kilometa 123 kwa kiwango cha lami kutoka Nyankumbu – Nyalubele – Ijundu – Kharumwa - Bukwimba mpaka Nyang’holongo. Je, ni lini sasa ujenzi huo utaanza? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, ahsante, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Hussein Nassor Amar, Mbunge wa Nyang’hwale kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kama nilivyosema kwenye jibu langu la msingi kilometa hizo mbili ni sehemu ya hiyo barabara ambayo tunategemea kuifanyia upembuzi yakinifu na usanifu wa kina ili baada ya kukamilisha tuweze kuijenga kwa kiwango cha lami. Kwa hiyo, ni lini tutaanza ni pale ambapo tutakamilisha hatua za awali za kuifanyia upembuzi yakinifu na usanifu wa kina ikiwa ni hatua za awali baada ya hapo tutaanza kuijenga kwa kiwango cha lami. Ahsante.

Name

Boniphace Mwita Getere

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bunda

Primary Question

MHE. HUSSEIN N. AMAR aliuliza:- Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi iliyotolewa na Waziri Mkuu Mheshimiwa Kassim Majaliwa Majaliwa ya Ujenzi wa barabara ya Kharumwa yenye urefu wa kilometa mbili kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 2

MHE. BONIPHACE M. GETERE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza na naishukuru Serikali kwa Wizara ya Ujenzi kwa kuhangaika na ujenzi wa lami kwa barabara ya Bariri - Mgeta. Sasa kwa sababu mmekwishafanya upembuzi yakinifu na mmeshafanya tathimini ya ujenzi; ni lini sasa hii barabara ya Mgeta - Bariri itajengwa kwa kiwango cha lami? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Getere, Mbunge wa Bunda kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, barabara ya Bariri - Mgeta ni barabara ambayo inasimamiwa na Wakala wa Barabara (TANROADS) naomba nimuhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali inatafuta fedha ili ikishapata fedha basi hii barabara ambayo ni njia ya mkato kwenda Nata - Mgumu iweze kujengwa kwa kiwango cha lami. Ahsante. (Makofi)

Name

Dr. Charles Stephen Kimei

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vunjo

Primary Question

MHE. HUSSEIN N. AMAR aliuliza:- Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi iliyotolewa na Waziri Mkuu Mheshimiwa Kassim Majaliwa Majaliwa ya Ujenzi wa barabara ya Kharumwa yenye urefu wa kilometa mbili kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 3

MHE. DKT. CHARLES S. KIMEI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana, kwa vile ujenzi wa barabara ya Chekereni – Kahe - Mabogiri kwa kiwango cha lami ipo kwenye Ilani ya CCM na pia ni ahadi ya viongozi wakubwa wa kitaifa. Je, ni lini ujenzi huo utaanza?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, ahsante napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Kimei, Mbunge wa Vunjo kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, barabara aliyoainisha iPo kwenye Ilani ya Chama cha Mapinduzi na nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba katika kipindi hiki kuna hatua ambazo tutaanza kuzitekeleza kama tulivyoainisha kwenye Ilani lakini itategemea sana na kadri ya fedha itakavyopatikana. Ahsante.

Name

Mariamu Nassoro Kisangi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. HUSSEIN N. AMAR aliuliza:- Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi iliyotolewa na Waziri Mkuu Mheshimiwa Kassim Majaliwa Majaliwa ya Ujenzi wa barabara ya Kharumwa yenye urefu wa kilometa mbili kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 4

MHE. MARIAM N. KISANGI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana.

Je, Serikali lini itakamilisha kujenga barabara ya Kibamba - Kibwegere mpaka Mabwepande kwa kiwango cha lami?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, ahsante, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mariam Kisangi, Mbunge wa Viti Maalum, Dar es Salaam kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, barabara aliyoitaja ipo kwenye mpango wetu kati ya barabara ambazo zipo Dar es Salaam kwa ajili ya kupunguza misongamano ya Dar es Salaam. Kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali inaendelea kutafuta fedha ili barabara hii iweze kujengwa kwa kiwango cha lami ikiwa pia ni mkakati wa kupunguza foleni kubwa zinazotokea katika Jiji la Dar es Salaam. Ahsante.

Name

Anatropia Lwehikila Theonest

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. HUSSEIN N. AMAR aliuliza:- Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi iliyotolewa na Waziri Mkuu Mheshimiwa Kassim Majaliwa Majaliwa ya Ujenzi wa barabara ya Kharumwa yenye urefu wa kilometa mbili kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 5

MHE. ANATROPIA L. THEOENEST: Mheshimiwa Spika, nakushukuru; barabara ya Benako kuja Karagwe haina lami na hii ni barabara muhimu sana kwa sababu ya ulinzi, kule kuna utekajeji lakini pia ufanyaji wa biashara kati ya Tanzania na Rwanda. Swali ni lini hiyo barabara itajengwa kwa kiwango cha lami?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Anatropia Theonest, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, barabara aliyoitaja ambayo inaanzia Bugene kupitia Chato hadi Benako ni barabara ambayo inaunganisha pia na nchi yetu Uganda nchi yetu, lakini pia kwenda Rwanda. Barabara hii ipo mbioni kuanza kujengwa kilometa 62 kwa kiwango cha lami na ipo kwenye mpango kuanzia mwaka huu wa bajeti. Ahsante. (Makofi)