Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 28 Works and Transport Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 244 2022-05-23

Name

Hussein Nassor Amar

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nyang'hwale

Primary Question

MHE. HUSSEIN N. AMAR aliuliza:-

Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi iliyotolewa na Waziri Mkuu Mheshimiwa Kassim Majaliwa Majaliwa ya Ujenzi wa barabara ya Kharumwa yenye urefu wa kilometa mbili kwa kiwango cha lami?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE) alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Hussein Nassor Amar, Mbunge wa Nyang’hwale kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kwa kuzingatia umuhimu wa barabara hii, Serikali kupitia Wizara yangu imeweka barabara yote ya Nyankumbu kuanzia Geita – Nyang’hwale hadi Nyang’holongo yenye urefu wa kilometa 123.11 inayojumuisha sehemu ya Kharumwa – Nyang’hwale katika mpango wa kufanyiwa upembuzi yakinifu na usanifu wa kina katika mwaka huu wa fedha wa 2022/2023 hii ikiwa ni maandalizi ya ujenzi wa kiwango cha lami ambao utahusisha pia kilometa mbili katika eneo la Kharumwa anazozizungumzia Mheshimiwa Mbunge. Ahsante.