Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Amina Ali Mzee

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. AMINA ALI MZEE aliuliza:- Je, ni lini Mkongo wa Mawasiliano wa Taifa utapelekwa katika Wilaya 14 ikiwemo za Mjini Magharibi na Kusini Unguja?

Supplementary Question 1

MHE. AMINA ALLY MZEE: Mheshimiwa Spika, asante kwa majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, naomba kuuliza swali moja la nyongeza.

Je, Serikali haioni sasa iko haja ya kuharakisha juu ya mradi wa ujenzi wa Mkongo wa Taifa uenee nchi nzima?

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Amina Ali Mzee, Mbunge wa Viti Maalum - Zanzibar kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwanza kabisa naomba nilishukuru Bunge lako tukufu kwa kutupitishia bajeti ambayo inaenda kuhakikisha kwamba ujenzi wa Mkongo wa Taifa unakamilika. Lakini kama nilivyosema katika jibu la msingi ni kwamba tayari tuna Wilaya 43 ambazo zimeshakamilika lakini katika bajeti ya mwaka jana Wilaya 23 tena zinaenda kukamilishwa. Lakini katika bajeti ambayo imepitishwa Ijumaa Wilaya 15 zingine zinaenda kukamilika kufikisha jumla ya Wilaya 81. Hivyo tunaomba kabisa kwamba kufikia mwaka 2025 wilaya zote nchini zitakuwa zimepata huduma ya mkongo wa mawasiliano wa Taifa. Nakushukuru.

Name

Maryam Azan Mwinyi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Chake Chake

Primary Question

MHE. AMINA ALI MZEE aliuliza:- Je, ni lini Mkongo wa Mawasiliano wa Taifa utapelekwa katika Wilaya 14 ikiwemo za Mjini Magharibi na Kusini Unguja?

Supplementary Question 2

MHE. MARYAM AZAN MWINYI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, tatizo la Mkongo wa Mawasiliano lilipo Mjini Magharibi na Mkoa wa Kusini Unguja halitofautiani na tatizo la Kaskazini Pemba na Kusini Pemba. Nini kauli ya Serikali kuhusu mawasiliano katika maeneo hayo? (Makofi)

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, katika jibu langu la msingi Mkongo wa Mawasiliano wa Taifa kwa upande wa Zanzibar umeshafika katika Wilaya zote kwa upande wa Zanzibar. Kwa hiyo labda tu tutaendelea kutoa elimu na ili kuwajulisha namna gani Mkongo wa Taifa huu unatoa huduma na kuwaonyesha vituo ambavyo vinatoa huduma hiyo. Nakushukuru sana.

Name

Aleksia Asia Kamguna

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. AMINA ALI MZEE aliuliza:- Je, ni lini Mkongo wa Mawasiliano wa Taifa utapelekwa katika Wilaya 14 ikiwemo za Mjini Magharibi na Kusini Unguja?

Supplementary Question 3

MHE. ALEKSIA A. KAMGUNA: Mheshimiwa Spika, ahsante, Ofisi ya Mkurugenzi wa Wilaya ya Malinyi na Mkuu wa Wilaya ya Malinyi haina mawasiliano ya simu; je, Serikali ina mkakati gani kumaliza adha hiyo katika Wilaya hiyo?

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Aleksia Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwa bajeti ambayo Bunge lako tukufu limetupitishia jana katika kata ambazo Mheshimiwa Mbunge ameziongelea na makao makuu ya Halmashauri zote zipo katika mpango wa utekelezaji. Hivyo tuombe tu kwamba tuendelee kushirikiana kuhakikisha kwamba tutakapofikisha huduma hii basi tupate ushirikiano kutoka kwa wananchi katika maeneo yetu, ahsante.

Name

Yahya Ally Mhata

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nanyumbu

Primary Question

MHE. AMINA ALI MZEE aliuliza:- Je, ni lini Mkongo wa Mawasiliano wa Taifa utapelekwa katika Wilaya 14 ikiwemo za Mjini Magharibi na Kusini Unguja?

Supplementary Question 4

MHE. YAHYA A. MHATA: Mheshimiwa Spika, mkandarasi aliyejenga Mkongo wa Taifa kutoka Mangaka kwenda Mtambaswala kwenye kituo cha Mtambaswala imegundulika ameweka vifaa vya zamani na alitakiwa ajenge tank la maji jambo ambalo hakufanya hivyo. Nini kauli ya Serikali juu ya mkandarasi huyu?

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Ally Mhata, Mbunge wa Nanyumbu kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli kabisa tumejenga kilometa 72 kutoka Mangaka mpaka Mtambaswala na Mheshimiwa Mbunge tulikuwepo wote wakati tunafika katika kituo kile ambacho ndio kinaenda kuunganisha na Msumbiji. Changamoto ambazo zimejitokeza katika kile kituo tayari Serikali inachukua hatua ili kujiridhisha ni wapi tatizo lilianzia ili kuhakikisha kwamba kituo hiki kinaanza kufanya kazi mara moja, ahsante.

Name

Benaya Liuka Kapinga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbinga Vijijini

Primary Question

MHE. AMINA ALI MZEE aliuliza:- Je, ni lini Mkongo wa Mawasiliano wa Taifa utapelekwa katika Wilaya 14 ikiwemo za Mjini Magharibi na Kusini Unguja?

Supplementary Question 5

MHE. BENAYA L. KAPINGA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana, Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga pamoja na kwamba kata nyingi kutokuwa na mawasiliano ziko kata nne minara imekamilika sasa hivi zaidi ya miaka minne; Kata ya Muhongozi, Kipololo, Kijiji cha Lunolo, Kata ya Ukata Kijiji cha Litoho, kata hizi zimekamilisha minara. Ni lini itawashwa hii minara?

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge wa Mbinga kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, changamoto ya minara iliyopo katika Jimbo la Mbinga tayari Mheshimiwa Mbunge tumeshawasiliana na tayari hatua tumeshaanza kuchukua. Changamoto iliyokuwepo kwa kipindi kile ni kwamba mnara ukishasimama hiyo ni hatua ya kwanza ambayo ndio passive equipment. Lakini kuna hatua ya pili ambayo ni kuweka vile vifaa vya kurusha mawimbi ambayo ndio active equipment. Hapa katikati tumekuwa na changamoto kubwa sana ya covid-19, sasa hii changamoto imesababisha production ya vifaa kutoka katika nchi ambazo tunaagiza ndio imekuwa changamoto katika ukamilishaji wa vifaa hivi.

Mheshimiwa Spika, lakini mpaka sasa tayari TTCL wameshaagiza vifaa na vingine vimeshaingia nchini. Hivyo Mheshimiwa Mbunge atarajie kwamba minara hiyo ambayo tayari imeshasimama itawashwa hivi karibuni na mawasiliano yataanza kupatikana katika Jimbo la Mbinga. Ahsante.