Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 28 Information, Communication and Information Technology Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari 241 2022-05-23

Name

Amina Ali Mzee

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. AMINA ALI MZEE aliuliza:-

Je, ni lini Mkongo wa Mawasiliano wa Taifa utapelekwa katika Wilaya 14 ikiwemo za Mjini Magharibi na Kusini Unguja?

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Amina Ali Mzee, Mbunge wa Viti Maalum Zanzibar, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia Wakala wa Miundombinu ya Mawasiliano Zanzibar imefikisha huduma za Mkongo wa Taifa wa Mawasiliano katika Mikoa na Wilaya zote za Zanzibar. Mjini Magharibi inapata huduma kupitia vituo vilivyopo maeneo ya Jamhuri Garden, Fumba na Ofisi za Miundombinu ya Mawasiliano Zanzibar (ZICTIA) na Kusini Unguja inapata huduma kupitia kituo kilichopo Paje.

Mheshimiwa Spika, hadi sasa jumla ya Wilaya 43 nchini zimefikiwa na Mkongo wa Mawasiliano wa Taifa. Kwa bajeti ya mwaka wa fedha 2021/2022 jumla ya Wilaya mpya 23 zitafikiwa na hivyo kuwa na jumla ya Wilaya 66 nchini zenye huduma ya Mkongo wa Taifa wa Mawasiliano.

Mheshimiwa Spika, Serikali imepanga kuwa Wilaya zote nchini zitafikiwa na huduma za Mkongo wa Taifa wa Mawasiliano ifikapo mwaka 2025. Mwaka wa fedha 2022/2023 Wilaya zingine mpya 15 zitafikiwa na hivyo kuwa na jumla ya Wilaya 81. Wilaya zinazobaki zitafikishiwa huduma za Mkongo wa Mawasiliano wa Taifa kwa kipindi kinachobaki kufikia 2025 kama ilivyopangwa. Ahsante.