Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. Dalaly Peter Kafumu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Igunga

Primary Question

MHE. DKT. DALALY P. KAFUMU aliuliza:- Mbuga ya Hifadhi ya Wembere ni mbuga iliyotelekezwa na Serikali na kupoteza sifa za kuendelea kuwa hifadhi na sasa inatumika na wafugaji kulisha mifugo na wakulima kulima alizeti na mpunga kwenye eneo hilo. Je, ni kwa nini Serikali isibadilishe matumizi ya mbuga hiyo badala yake ipimwe na kutumika kwa wafugaji na wakulima na kuondoa migogoro inayoendelea kati ya wakulima na wafugaji ambayo wakati mwingine inasababisha mauaji na uharibifu wa mali?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. DALALY P. KAFUMU: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Namshukuru Naibu Waziri kwa majibu ambayo hayatoshelezi.
Kwa kuwa mimi nimezaliwa na kukulia katika mbuga hii, ni mashahidi kwamba mbuga hii ilitelekezwa, kwa hiyo, wananchi wengi wakulima na wafugaji walihamia katika mbuga hii. Matokeo yake wanyama na hao ndege anaosema wametoweka; kama wamebaki ni sehemu ndogo sana; na kwa kuwa eneo hili mwaka 2014 lilisababisha mauji ya wakulima watano kutokana na mgogoro wa wakulima: kwa nini Serikali isikubali ombi hili? Swali la kwanza. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, kwa kuwa sasa hivi nchi inakabiliwa na migogoro ya wafugaji na wakulima, sisi sote ni mashahidi; na kwa kuwa mwaka 2011 Serikali hii ilifanya tathmini ya mbuga zile ambazo zimepoteza sifa na Wembere ilikuwa ni mojawapo; kwa nini Serikali isilitazame upya jambo hili na kuitenga mbuga hii ili wananchi wanaoishi kwenye eneo hilo waweze kulima na kufuga bila kugombana; lakini pia wanaweza kubakiza eneo dogo kwa ajili ya hawa ndege hawa anaowasema? Ahsante sana.

Name

Eng. Ramo Matala Makani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Naibu Spika, eneo hili la Wembere hivi sasa ninavyozungumza, limegawanywa katika vitalu vinne; Kitalu kinachoitwa Wembere Open Area Central One, kitalu kinachoitwa Wembere Central Area Two, Wembere Game Controlled Area upande wa Kusini, lakini pia upande wa Kaskazini kuna Wembere Open Area, vyote hivi vikiwa ni vitalu vinavyopaswa kuendesha shughuli za uwindaji wa kitalii.
Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli, mojawapo ya kitalu, kwa mfano, hiki cha upande wa Kaskazini, Wembere Open Area hakijawahi hata kupata mwekezaji kwenye shughuli hizo za uwindaji. Lakini vipo vitalu ambavyo vinafanyakazi, kwa mfano kile cha Open Area Central One, kinatumika na ndiyo hicho ambacho nimesema ni mojawapo ya vitalu vinavyoiingizia fedha Serikali.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa sababu tunazungumzia mazingira halisi ambayo Mheshimiwa Mbunge anatoka, wakati huo huo tunachokizungumzia ni suala la utaalam vilevile, basi nimwambie tu Mheshimiwa Mbunge kwamba arejee azma ya Serikali tuliyoitangaza hapo awali, kwamba sasa tunataka kufanya zoezi Shirikishi; yeye pamoja na wananchi kwenye eneo linalohusika kwenye maeneo hayo ya Wembere pamoja na timu ya wataalam ambayo tayari tumeshasema baada ya Bunge hili tunakwenda kwenye maeneo hayo kuhakiki, twende tukaoneshane.
Mheshimiwa Naibu Spika, tuchanganye utaalam na maoni ya wananchi ili tuweze kufikia muafaka sasa kujua kama kuna eneo ambalo ni sehemu ya eneo hili ambalo litaonekana halifai kuendelezwa tena kwa shughuli hii ambayo sasa hivi inaendeshwa kwa mujibu wa sheria, basi itakuwa hivyo. Kwa sasa hivi tutaendana na sheria kama ilivyo mpaka hapo mabadiliko yatakapofanyika baada ya zoezi lile la Serikali.

Name

Margaret Simwanza Sitta

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Urambo

Primary Question

MHE. DKT. DALALY P. KAFUMU aliuliza:- Mbuga ya Hifadhi ya Wembere ni mbuga iliyotelekezwa na Serikali na kupoteza sifa za kuendelea kuwa hifadhi na sasa inatumika na wafugaji kulisha mifugo na wakulima kulima alizeti na mpunga kwenye eneo hilo. Je, ni kwa nini Serikali isibadilishe matumizi ya mbuga hiyo badala yake ipimwe na kutumika kwa wafugaji na wakulima na kuondoa migogoro inayoendelea kati ya wakulima na wafugaji ambayo wakati mwingine inasababisha mauaji na uharibifu wa mali?

Supplementary Question 2

MHE. MARGARET S. SITTA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuulizwa swali la nyongeza kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, maelezo yaliyoko katika swali namba 279 yanafanana sana na hali halisi iliyoko Urambo katika Kata ya Nsenda ambako wakulima wa Lunyeta na Kangeme walichomewa mahindi yao kutokana na mgogoro wa mipaka kama ulivyoelezwa katika suala hili.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa mgogoro huu umewaacha wakulima bila kujua hatima yao na kusababisha usumbufu sana wa kupata chakula; na Serikali ilikiri kwamba ilifanya makosa kuwachomea wakulima ambao walikuwa wamelima katika eneo hilo, je, Serikali iko tayari sasa kufuatana na mimi kwenda kuangalia hali halisi ili kutafuta ufumbuzi wa kudumu?

Name

Eng. Ramo Matala Makani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwamba tunazo sheria, lakini ni kweli pia kwamba kuwa na sheria ni sehemu moja au ni jambo moja, lakini utekelezaji wa sheria ni jambo lingine. Inawezekana kabisa kwamba mahali pengine utekelezaji wa sheria unaweza kuwa ni utekelezaji wa sheria unaovunja sheria. Sasa pale ambapo tayari kuna sheria na sheria zinatakiwa kusimamiwa, Serikali itaendelea kusimamia utekelezaji wa sheria, lakini tunatoa wito kwanza kwa watu wote ambao wanatekeleza sheria, hasa zile sheria ambazo ziko chini ya Wizara ya Maliasili na Utalii, waweze kutekeleza sheria hizo bila kukiuka sheria zenyewe, lakini bila kufanya mambo ambayo yanakwenda kinyume cha kanuni na taratibu.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa suala mahsusi ambalo Mheshimiwa Mbunge ameliuliza, linalohisiana na eneo alilolitaja, napenda kumuahidi kwamba nikitoka hapa nitakwenda kulifuatilia zaidi na mimi nilifahamu kwa sababu ni mahsusi ili niweze kuona kama tunaweza kupata suluhisho katika kipindi hiki ambacho tuko Bungeni; lakini kama itabidi kwenda kuangalia, basi mara tu baada ya kumaliza Bunge la Bajeti, nitaweza kuandamana naye kwenda kuona kuna nini ili tuweze kupata ufumbuzi.

Name

Dr. Haji Hussein Mponda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Malinyi

Primary Question

MHE. DKT. DALALY P. KAFUMU aliuliza:- Mbuga ya Hifadhi ya Wembere ni mbuga iliyotelekezwa na Serikali na kupoteza sifa za kuendelea kuwa hifadhi na sasa inatumika na wafugaji kulisha mifugo na wakulima kulima alizeti na mpunga kwenye eneo hilo. Je, ni kwa nini Serikali isibadilishe matumizi ya mbuga hiyo badala yake ipimwe na kutumika kwa wafugaji na wakulima na kuondoa migogoro inayoendelea kati ya wakulima na wafugaji ambayo wakati mwingine inasababisha mauaji na uharibifu wa mali?

Supplementary Question 3

MHE. DKT. HADJI H. MPONDA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Migogoro ya ardhi ambayo inajitokeza kati ya hifadhi na wananchi nayo yanajitokeza katika Pori Tengefu la Bonde la Kilombero. Tumeiomba Serikali, naomba niwaulize hapa Serikali, ni lini sasa mtarudisha ardhi ile ya Buffer Zone katika Pori Tengefu la Kilombero?

Name

Eng. Ramo Matala Makani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kwanza niseme kwamba Buffer Zone tafsiri yake ya moja kwa moja isiyohitaji utaalam mwingi sana ni eneo ambalo linapaswa kuwa siyo la yeyote kati ya pande mbili zinazopakana. Eneo hilo kwa mujibu wa kanuni na taratibu, linapaswa kuwa ni eneo ambalo shughuli za uhifadhi zinakuwa mild, lakini pia shughuli za matumizi ya kibinadamu na zenyewe zinakuwa mild kwa maana ya kwamba siyo eneo ambalo linatumika moja kwa moja kwa asilimia mia moja na pande zote mbili zinazopakana. Kwa hiyo, kusema kwamba lirudishwe kwa wananchi, pengine inaweza kuwa siyo sahihi sana kwa sababu halijawahi kuwa kwa asilimia mia moja upande wa hifadhi.
Mheshimiwa Naibu Spika, kama nilivyotangulia kusema na ninarudia tena, mazoezi haya yote ya kupitia hifadhi baada ya hifadhi; iwe hifadhi ya misitu, iwe hifadhi ya wanyamapori au hifadhi nyingine yoyote ile chini ya Wizara ya Maliasili na Utalii; maeneo yote hayo yameorodheshwa kama sehemu ya migogoro ya ardhi na yameorodheshwa hivyo na Wizara ya Ardhi. Pia tunakwenda kufanya team work miongoni mwa Wizara ya Maliasili na Utalii, Wizara ya Ardhi yenyewe, TAMISEMI, eneo ambalo sasa Mheshimiwa Mbunge atashirikiana na Serikali ya Wilaya pale, lakini pia Wizara ya Nishati na Madini, pale patakapokuwa panahusika na mambo ya madini; lakini pia masuala ya maji kwa sababu tunahusika pia. Kwa kutunza misitu tunatunza pia vyanzo vya maji, basi pale itakapobidi kwamba kuna chanzo cha maji tunataka kukifanya kiwe endelevu, kukilinda, basi na Wizara ya Maji itahusika. Kwa kuanzia ni Wizara hizo tano.
Mheshimiwa Naibu Spika, nawaomba wananchi wote na kupitia swali hili la Mheshimiwa Mbunge, wawe wavumilivu katika kipindi hiki ambacho ni kipindi cha mpito ambapo Serikali sasa inakwenda kutafuta majibu ya kudumu kwenye migogoro hii ya mipaka na hifadhi na migogoro ya ardhi kwa ujumla.