Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Lucy John Sabu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. LUCY J. SABU K.n.y. MHE. JUDITHI S. KAPINGA aliuliza: - Je, kuna mkakati gani wa kudhibiti watoto chini ya miaka saba kusoma shule za bweni?

Supplementary Question 1

MHE. LUCY J. SABU: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa majibu mazuri ya Serikali. Ninayo maswali mawili madogo ya nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza; je, ni vigezo vipi vinatumika kwa ajili ya kibali maalum kutolewa kwa shule za bweni?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili; kwa kuwa Waraka wa Elimu Na. 2 wa mwaka 2023 umetoa maelekezo wamiliki kuwa na kibali kwa ajili ya shule za bweni: -

Je, ni hatua zipi zimechukuliwa kwa shule ambazo zimekiuka agizo hili? Ahsante. (Makofi)

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Lucy John Sabu, Mbunge Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama nilivyokwisha eleza kwenye majibu ya swali la msingi, kwamba vipo vigezo ambavyo Kamishna wa Elimu anatumia, lakini hivi sasa tunahuisha vigezo hivyo. Na nimesema kuwa Wizara kwa kushirikiana na wadau inakamilisha kuandaa vigezo vitakavyotumiwa na Kamishna wa Elimu katika kutoa vibali hivi maalum. Kwa hiyo, nimwondoe hofu Mheshimiwa Mbunge, tunaendelea kufanya uhuishaji wa vigezo hivi na mara vitakapokuwa tayari basi Umma utajulishwa juu ya vigezo hivi ili iweze kufwata wakati wa kuomba vibali hivyo maalum.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika swali lake la pili, anataka kujua hatua zipi zilizochukuliwa; naomba nimhakikihsie Mheshimiwa Mbunge wale wote ambao walikuwa wanaendesha shule hizi kinyume na utaratibu wameweza kupewa notice, lakini vilevile wadhibiti ubora wetu wameweza kutembelea maeneo hayo na kuweza kujiridhisha juu ya huduma ambazo zinatolewa hapo, na baada ya kuona hali ilivyo basi tutachukua hatua mara moja, nakushukuru sana.

Name

Dr. Thea Medard Ntara

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. LUCY J. SABU K.n.y. MHE. JUDITHI S. KAPINGA aliuliza: - Je, kuna mkakati gani wa kudhibiti watoto chini ya miaka saba kusoma shule za bweni?

Supplementary Question 2

MHE. DKT. THEA M. NTARA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru.

Je, Serikali haioni haja sasa ya kufanya utafiti kujua watoto wangapi waliopo Bwenini wanafanyiwa ukatili wa kijinsia?

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Dkt. Thea Ntara kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa vile Mheshimiwa Mbunge anaomba Serikali iweze kufanya utafiti, nimwondoe hofu Serikali iko tayari kuchukua ushauri wake tuweze kufanya utafiti wa kuweza kujua athari zinazotokea katika unyanyasaji wa watoto wetu katika maeneo aliyoyataja.