Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 52 Education, Science,Technology and Vocational Training, Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia 691 2023-06-21

Name

Judith Salvio Kapinga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. LUCY J. SABU K.n.y. MHE. JUDITHI S. KAPINGA aliuliza: -

Je, kuna mkakati gani wa kudhibiti watoto chini ya miaka saba kusoma shule za bweni?

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, naomba sasa kujibu swali la Mheshimiwa Judith Salvio Kapinga, Mbunge Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali iliandaa Mwongozo wa Uanzishaji na Usajili wa Shule uliotolewa mwezi Novemba, 2020. Mwongozo huo umeelekeza bayana kuwa kibali cha kutoa huduma ya kulaza wanafunzi wa bweni kitatolewa kuanzia darasa la tano na kuendelea. Aidha, huduma ya bweni itatolewa kwa kibali maalum kwa wanafunzi wanaosoma chini ya darasa la tano.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na kutolewa kwa mwongozo huo, pia, Serikali imetoa Waraka wa Elimu Na. 2 wa Mwaka 2023 unaowaelekeza wamiliki wa shule wasiokuwa na kibali maalum cha kutoa huduma ya bweni kwa wanafunzi waliochini ya darasa la tano wasiendelee kutoa huduma hiyo. Aidha, kwa kushirikiana na wadau wa elimu, Wizara inakamilisha kuandaa vigezo vitakavyotumiwa na Kamishna wa Elimu katika kutoa kibali maalum.

Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kulijulisha Bunge lako Tukufu kuwa Serikali itaendelea kudhibiti tatizo la watoto chini ya darasa la tano kusoma shule za bweni kwa kuhakikisha kuwa inafanya ufuatiliaji wa mara kwa mara na shule itakayobainika kukiuka maelekezo hayo itachukuliwa hatua za kinidhamu, na kisheria ikiwemo kufutiwa usajili, nakushukuru.