Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Amb. Adadi Mohamed Rajabu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muheza

Primary Question

MHE. BALOZI ADADI M. RAJAB aliuliza:- Mji mdogo wa Wilaya ya Muheza ulianzishwa mwaka 2007 na ulihusisha Kata tatu za Muheza Mjini, Mbaramo, Majengo na Masuguru; na tangu wakati huo, umekuwa ukihudumia wananchi wake na taratibu za mapendekezo ya kuidhinisha uanzishwaji wa Halmashauri ya Mji wa Muheza tangu tarehe 10/01/2016. Je, ni kwa nini Serikali imechelewa kuiidhinisha Muheza kuwa Halmashauri ya Mji huku ikijua kuna ongezeko kubwa la watu na Kata zimeongezeka hadi kufikia sita?

Supplementary Question 1

MHE. BALOZI ADADI M. RAJAB: Mheshimiwa Naibu Spika, nina maswali mawili ya nyongeza.
Swali la kwanza, maombi ya kuanzisha Mji huo sasa hivi ni miaka tisa, tangu mwaka 2007. Nataka Mheshimiwa Waziri anihakikishie; ni lini, wataalam wake wa kwenda kuhakiki watafika Muheza?
Swali la pili, Jimbo la Muheza linaweza kuwa ni kubwa kuliko Majimbo yote hapa mjengoni, lina kata 37, vijiji 135, vitongoji 530 unafikiria ni lini Jimbo hilo linaweza kugawiwa? Ahsante

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kumbukumbu halali tulizokuwa nazo, ni kwamba kikao cha RCC kilikaa Novemba 2013; na mchakato huu maana yake ulienda kuja katika Ofisi ya Rais, lakini kipindi hicho ikiwa Ofisi ya Waziri Mkuu. Ndiyo maana hapa juzi juzi Waziri wangu mwenye dhamana, Mheshimiwa George Simbachawene, aliwaambia wataalam wetu kuleta analysis ya kila Halmashauri na kila Mkoa. Nadhani wameomba na wanaangalia iko katika status gani?
Mheshimiwa Naibu Spika, katika maeneo haya ya Jimbo lako Mheshimiwa Adadi, ni kwamba wataalamu wetu katika kipindi hiki cha hivi sasa, bajeti wanayoshughulika nayo ni kwamba maeneo ya kipaumbele cha kwanza, itakuwa kuja kwako Muheza lakini hali kadhalika kwenda katika Mji huu wa Mombo ambapo maeneo haya maombi yao yote yameletwa pamoja.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, Mheshimiwa Adadi Rajab usiwe na mashaka, hata ndugu yangu hapa Mheshimiwa Profesa Maji Marefu mambo yenu yote yakiwa yako jikoni yanaendelea kufanyiwa vizuri. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, suala la kugawanya Kata ili Jimbo la Muheza kuwa katika Majimbo mawili, naomba niseme kwamba kwa sababu jambo hili haliko kwetu, TAMISEMI, liko katika Tume ya Taifa ya Uchaguzi; ambapo ikiona kama inafaa kwa vigezo, basi labda Jimbo hili linawezekana litaweza kugawa kama Majimbo mengine yalivyogawiwa.
Kwa hiyo, nina imani Tume ya Taifa ya Uchaguzi, wataangalia kufanya analysis, kuangalia ukubwa wa Jimbo hili, kwa sababu kuna Kata 37 na vijiji zaidi ya 135 wataangalia kwamba katika uchaguzi ujao, inawezekana saa nyingine wao watakavyoona inatosha, watafanya maamuzi sahihi katika eneo hilo.

Name

George Malima Lubeleje

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpwapwa

Primary Question

MHE. BALOZI ADADI M. RAJAB aliuliza:- Mji mdogo wa Wilaya ya Muheza ulianzishwa mwaka 2007 na ulihusisha Kata tatu za Muheza Mjini, Mbaramo, Majengo na Masuguru; na tangu wakati huo, umekuwa ukihudumia wananchi wake na taratibu za mapendekezo ya kuidhinisha uanzishwaji wa Halmashauri ya Mji wa Muheza tangu tarehe 10/01/2016. Je, ni kwa nini Serikali imechelewa kuiidhinisha Muheza kuwa Halmashauri ya Mji huku ikijua kuna ongezeko kubwa la watu na Kata zimeongezeka hadi kufikia sita?

Supplementary Question 2

MHE. GEORGE M. LUBELEJE: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi, na mimi niulize swali moja dogo tu. Kwa kuwa vijiji vya Chipogolo, Mima, Pwaga, Kibakwe, Berege, Mbori na Chunyu vina idadi ya watu wengi sana, ni trading centers ambazo ni kubwa sana na kuna wafanyabiashara wengi.
Je, Mheshimiwa Naibu Waziri, atakubaliana nami kwamba sasa ipo haja kwenda kufanya utafiti kuona kwamba vinaweza kupewa hadhi ya kuwa Miji Midogo?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nikiri wazi kuwa juzi nilikwenda pale Mpwapwa, katika kuangalia ule mfumo wa maji kama vijana wa sekondari ya Mpwapwa wanapata maji na kuangalia huduma ya afya kama wanatumia mifumo ya electronic katika Hospitali ya Wilaya ya Mpwapwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli Wilaya ile ina Majimbo mawili, Jimbo la Kibakwe na Jimbo la Mpwapwa, lakini jiografia yake ni kubwa zaidi; na kwa sababu najua utaratibu wa kuomba maeneo hayo sasa kuwa Mamlaka ya Mji Mdogo, maana yake mchakato wake unaanza katika ngazi za chini, kuanzia ngazi za vijiji, katika mikutano ya Baraza la Madiwani, halikadhalika katika WDC na Baraza la Madiwani.
Mheshimiwa Naibu Spika, mtakavyoona kuwa hiyo nafasi inatosha, basi nadhani michakato hiyo itaanza na Ofisi ya Rais, TAMISEMI itafanya tathmini kuangalia kwamba, basi kama kuna hadhi ya kuipa mamlaka ya Miji Midogo hatutasita kufanya hivyo. Kuhusu kuangalia kama vile vigezo vitakuwa vimefikiwa.
Kwa hiyo, kwa kushirikiana na Mheshimiwa George Simbachawene ambaye ni Waziri wa Nchi yuko eneo hilo, halikadhalika Mheshimiwa Lubeleje ambaye ni Mbunge wa Mpwapwa aliyeleta concern hii, nadhani tunaweza kufanya mchakato huo, basi Ofisi ya Rais, TAMISEMI, haitasita ikiona kwamba pale mahitaji yanayotakiwa yaweze kufanyiwa hivyo.

Name

Venance Methusalah Mwamoto

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilolo

Primary Question

MHE. BALOZI ADADI M. RAJAB aliuliza:- Mji mdogo wa Wilaya ya Muheza ulianzishwa mwaka 2007 na ulihusisha Kata tatu za Muheza Mjini, Mbaramo, Majengo na Masuguru; na tangu wakati huo, umekuwa ukihudumia wananchi wake na taratibu za mapendekezo ya kuidhinisha uanzishwaji wa Halmashauri ya Mji wa Muheza tangu tarehe 10/01/2016. Je, ni kwa nini Serikali imechelewa kuiidhinisha Muheza kuwa Halmashauri ya Mji huku ikijua kuna ongezeko kubwa la watu na Kata zimeongezeka hadi kufikia sita?

Supplementary Question 3

MHE. VENANCE M. MWAMOTO: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa Wilaya ya Kilolo inafanana kabisa na matatizo ambayo yako hapo, na ni katika Majimbo makubwa, takriban lina kilometa za mraba takribani 21,000; na kwa kuzingatia hilo, Serikali iliamua kutoa Mji Mdogo wa Ilula, sasa ni muda mrefu.
Je, haioni sasa ni muda muafaka wa kupewa hadhi ya kuwa Halmashauri kamili?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli katika kumbukumbu zangu pale kuna barua ya tarehe 2 Juni, 2015 imetoka Kilolo iliyokuwa ikiomba uanzishaji wa Halmashauri hii. Katika maeneo ambayo Ofisi ya Rais, TAMISEMI itaenda kufanya uhakiki, eneo la Kilolo litakuwa mojawapo. Kwa hiyo, tufanye subira katika hilo.

Name

Rashid Abdallah Shangazi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mlalo

Primary Question

MHE. BALOZI ADADI M. RAJAB aliuliza:- Mji mdogo wa Wilaya ya Muheza ulianzishwa mwaka 2007 na ulihusisha Kata tatu za Muheza Mjini, Mbaramo, Majengo na Masuguru; na tangu wakati huo, umekuwa ukihudumia wananchi wake na taratibu za mapendekezo ya kuidhinisha uanzishwaji wa Halmashauri ya Mji wa Muheza tangu tarehe 10/01/2016. Je, ni kwa nini Serikali imechelewa kuiidhinisha Muheza kuwa Halmashauri ya Mji huku ikijua kuna ongezeko kubwa la watu na Kata zimeongezeka hadi kufikia sita?

Supplementary Question 4

MHE. RASHID A. SHANGAZI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kuniona. Kwa kuwa Halmashauri ya Wilaya ya Lushoto ina Majimbo mawili; Mlalo na Lushoto, na tunalo ombi katika Ofisi ya Rais, TAMISEMI la kupata Halmashauri ya Mlalo.
Je, ni lini sasa Serikali itatupatia Jimbo la Mlalo Halmashauri kamili?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, katika kumbukumbu zetu, namshukuru Mheshimiwa Mbunge alishawahi kufika mpaka ofisini na katika kufanya rejea katika documents zetu, tumeona kwamba kuna vitu fulani vilikuwa bado havijakidhi vigezo kule Mlalo; na maelekezo tuliyoyatoa ni kwamba, wafanye ule mchakato kuangalia vile vigezo viweze kukamilika, halafu maombi yale yawasilishwe rasmi katika Ofisi ya Rais, TAMISEMI, ilimradi eneo hilo sasa wataalam watakapokuja kufanya uhakiki; ikionekana eneo hilo sasa linatosha kuanzisha Halmashauri mpya, basi hakuna shaka, Ofisi ya Rais, TAMISEMI haitosita kufanya hivyo.
Mheshimiwa Naibu Spika, tumeshatoa maelekezo katika suala zima la Mlalo na Mheshimiwa Shangazi amekuwa akilifuatilia kwa ukaribu sana suala hili. Sasa naomba nitoe msukumo katika maeneo husika, ule mchakato na vile vigezo mwanzo vilikuwa havijakamilika vizuri, tuweze kuvikamilisha na maombi hayo sasa yawasilishwe katika Ofisi ya Rais, TAMISEMI kwa ufanisi wa hali ya juu katika maeneo hayo.