Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 3 Sitting 34 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 275 2016-06-01

Name

Amb. Adadi Mohamed Rajabu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muheza

Primary Question

MHE. BALOZI ADADI M. RAJAB aliuliza:-
Mji mdogo wa Wilaya ya Muheza ulianzishwa mwaka 2007 na ulihusisha
Kata tatu za Muheza Mjini, Mbaramo, Majengo na Masuguru; na tangu wakati
huo, umekuwa ukihudumia wananchi wake na taratibu za mapendekezo ya
kuidhinisha uanzishwaji wa Halmashauri ya Mji wa Muheza tangu tarehe
10/01/2016.
Je, ni kwa nini Serikali imechelewa kuiidhinisha Muheza kuwa Halmashauri
ya Mji huku ikijua kuna ongezeko kubwa la watu na Kata zimeongezeka hadi
kufikia sita?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA
alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais
TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Balozi Adadi Mohamed Rajab,
Mbunge wa Muheza, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli mapendekezo ya kupandisha hadhi
Mamlaka ya Mji Mdogo wa Muheza, kuwa Halmashauri ya Mji wa Muheza,
yalifanyika na kupitishwa katika vikao vyote vya kisheria, vikiwemo Baraza la
Madiwani, Kamati ya Ushauri ya Wilaya na Mkoa. Maombi haya tayari
yamepokelewa na Ofisi ya Rais, TAMISEMI baada ya kupitishwa na RCC. Hatua
itakayofuata ni kwenda kufanya uhakiki wa vigezo vinavyozingatiwa katika
kuanzisha Halmashauri za Miji nchini.