Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Sylivia Francis Sigula

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SYLVIA F. SIGULA aliuliza: - Je, lini SACCOS 130 za wanawake na vijana zitaanzishwa katika mikoa 16 ikiwemo Kigoma kama ilivyoainishwa katika Ilani ya 2020/2025?

Supplementary Question 1

MHE. SYLVIA F. SIGULA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Kwanza ninashukuru kwa majibu mazuri ya Serikali, lakini kutokana na majibu ya Serikali utaona kabisa bado tuko kwenye asilimia 31.5 ya utekelezaji, hii inaonesha bado kazi inatakiwa kufanyika. Nataka kujua ni nini mkakati maalum wa Serikali, kuhakikisha wanawake wengi na vijana wengi wanapata uelewa na umuhimu wa masuala haya ya SACCOS ili waweze kujiunga wajikwamue kiuchumi?

Swali la pili, kulikuwa na VICOBA vingi vya wakinamama na vijana. Je, Serikali iko tayari kuviwezesha vitambulike rasmi ili viingie kunufaika kwenye mikopo ya asilimia 10 katika mfumo huu mpya unaokuja?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEORGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Sylvia Sigula.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali lake la kwanza la mkakati maalum wa Serikali kwa ajili ya kutoa elimu kwa wingi zaidi ili kufahamu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali kupitia Halmashauri za Wilaya na Majiji na Halmashauri za Miji, zina utaratibu na watumishi waliokuwa kule Maafisa Biashara, Maafisa Maendelo ya Jamiii pamoja na Maafisa Ushirika. Ni wajibu wao kuhakikisha kwamba wanasajili vikundi vingi zaidi au SACCOS nyingi zaidi kwenye maeneo yao na kuendelea kutoa elimu juu ya umuhimu wa SACCOS hizi. Hivyo basi, nitumie Bunge lako Tukufu kuwaelekeza tena Wakurugenzi wote wa Halmashauri za Wilaya hapa nchini kuhakikisha hawa niliowataja Maafisa Biashara, Maafisa Maendeleo ya Jamii pamoja na Maafisa Ushirika wanafanya kazi kwa pamoja kwa ajili ya kuweza kutoa elimu juu ya umuhimu kuwa na SACCOS na kusajili SACCOS nyingi ambazo zinakidhi vigezo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu swali lake la pili la VICOBA kutambuliwa zaidi na kupewa mikopo. Hili linategemeana vilevile na wao VICOBA kukidhi vigezo vile vya masharti ya mikopo ile ya asilimia 10. Hata katika mapitio yanayofanyika kwa maelekezo yake Rais wetu Dkt. Samia Suluhu Hassan, juu ya utoaji wa mikopo hii bado mikopo hii itakuwa ni ya vijana, wanawake na walemavu. Kinachofanyika ni review ya namna ya utoaji wa mikopo ile, siyo ubadilishwaji wa namna mikopo ile inavyotolewa kwa watu. Kwa hiyo, kama vikundi hivi vitakuwa vinakidhi vigezo, VICOBA hivi kwamba vina vijana, vina wanawake na walemavu, vinatakiwa pia kunufaika na mikopo ile inayotolewa. Kwa hiyo, tutazingatia hili pia katika timu ile inayofanyia mapitio haya ili waweze kuongeza SACCOS nyingi zaidi. (Makofi)

Name

Josephine Johnson Genzabuke

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SYLVIA F. SIGULA aliuliza: - Je, lini SACCOS 130 za wanawake na vijana zitaanzishwa katika mikoa 16 ikiwemo Kigoma kama ilivyoainishwa katika Ilani ya 2020/2025?

Supplementary Question 2

MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa katika Halmashauri hakuna sheria inayoruhusu vikundi vya SACCOS kukopeshwa. Je, ni lini Serikali italeta sheria Bungeni ili kufanya marekebisho SACCOS ziweze kukopeshwa?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEORGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mujibu wa Sheria ile ya Fedha za Serikali za Mitaa ambayo inaelezea namna ya utoaji wa mikopo ya vikundi, tayari kama nilivyokuwa nikimjibu Mheshimiwa Sigula kwamba kama SACCOS hizi zinakidhi vile vigezo vilivyotajwa kwenye Sheria ile ya Fedha ya Serikali za Mitaa, ya kuwa ni kuna vijana kwenye SACCOS hizo, ama SACCOS hizo zinaongozwa na walemavu au wanawake watastahili kupata fedha hizi za vikundi za asilimia 10, haina haja ya SACCOS hizi tena kusajiliwa kama vikundi kwa sababu tayari ni SACCOS zilizosajiliwa na kama viongozi wao wale mwenyekiti, katibu na muweka hazina wanakidhi vigezo vya umri kwa vijana na ni wanawake au walemavu basi wanastahili kupata mikopo hii ya asilimia 10. (Makofi)