Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 52 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 683 2023-06-21

Name

Sylivia Francis Sigula

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SYLVIA F. SIGULA aliuliza: -

Je, lini SACCOS 130 za wanawake na vijana zitaanzishwa katika mikoa 16 ikiwemo Kigoma kama ilivyoainishwa katika Ilani ya 2020/2025?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEORGRATIUS J. NDEJEMBI) alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais - TAMISEMI, ninaomba kujibu swali Mheshimiwa Sylvia Francis Sigula, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali kwa kushirikiana na wadau mbalimbali imewezesha kuanzishwa kwa jumla ya SACCOS 41 kwenye Mikoa 16 zikiwemo SACCOS 03 za Mkoa wa Kigoma. SACCOS hizo ni Kasulu Women SACCOS yenye wanachama 100 ikiwa na mtaji wa milioni 44, Vijana Kidahwe SACCOS yenye wanachama 20 ikiwa na mtaji wa milioni 14, na Amani Wanawake SACCOS yenye wanachama 33 ikiwa na mtaji wa milioni 21.

Mheshimiwa Spika, Serikali inaendelea kuhamasisha Mikoa ikiwemo Mkoa wa Kigoma na Mamlaka za Serikali za Mitaa kuendelea kuanzisha na kuzisimamia SACCOS kama ilivyoainishwa kwenye Ilani ili ziendelee kutoa huduma inayokusudiwa.